Lowassa awapasha akina Nape na Mangula...

Lowassa awapasha akina Nape na Mangula...

Sijuhi huyu mzee akitemwa na kamati kuu ya CCM katika mchujo wa awali wa wagombea Urais atakuwaje? pressure na kisukali zitapanda sana!

Nani wa kumtema? yeye ndo mwenye uwezo wa kuwatema kama alivyofanya majaribio kwenye kura za marohani baada ya kupata mafanikio sana alitoa suluhisho la kusitisha uasi na ukafanikiwa !
 
jan 8th 2014

waziri mkuu aliyejiuzulu, brother edward lowassa, ametembelea miradi ya maji katika kata ya selela iliyopo jimbo lake la mondul na kuongea na wapiga kura wake na kuwapiga vijembe viongozi wa chama chake waliomwambia watamchukulia hatua kali kwa sababu ya kutangaza nia ya kugombea kiti cha urais mwanzoni mwa mwezi hata kwa chama jiwe atakuwa rais 2015.

Brother lowasa aliwakumbusha akina nape na mangula kwamba yeye uwezo a
nao, nia anayo, wananchi wananipenda wakanitangazia siyo mimi nimetangaza na kuhusu harambee nimechangia kama wenzangu wanavyochangia, au nikiitwa kwenye harambee nisishiriki mpaka uchaguzi wa rais 2015 upite? Hiyo ni adhabu. Tuwe wangalifu na kuchambua maneno, tusiwe wepesi kulaumu na kuhukumu na pia kuwa kiongozi siyo kutisha na kuogopesha wanachama, wote tuna haki sawa katika chama chetu.

Ni hivi majuzi viongozi wa juu wa ccm walimuonya lowasa na wananchama wengine wa chama hicho kuacha kujitangazia kuwania urais kupitia ccm kwa vile muda wake rasimi bado na pia kutoa michango ya harambee mbali mbali, na kwa kufanya hivyo ni kuvunja kanuni, sheria za mwongozo wa chama na adhabu yake ni ku-jiqualify automatically wenyewe kwenye kuwania urais. Hata kinana mmoja ndugu sebastiani kiondo wa sanawari arusha alisema vyama siasa nchini vyote lao moja kupigania maslahi yao badala ya wananchi,...ebu niambe ndugu mwandishi brother lowasa anakosa gani kama siyo fitina za viongozi wakuu wa ccm?, ukiona hivyo wana mgomea wao tayari na tayari ameshajaza fomu ya kugombea kinachosubiliwa ni siku ya kumtangaza, alimaliza ndugu kiondo kwa masikitiko. —

in magu kahangara.







edo boy kamua baba kamua wata kupiga ndui tu ewe rais mtarajiwa.............
 
Wanabadili majina tu ya wamiliki lkn mitambo ni ile ile ya Ubungo!

Sisi watz nahisi tumelaaniwa na Mungu;umeme bei juu 78%;matibabu hamna;watoto wote wana feli;maji saafi hamna lkn hapa tunakesha kujadili Zitto na Lowassa na hawala wa Mbowe na sometimes uhusiano wa Dr Slaa




umelogwa peke yakoo kama ile mitambo ni ya kishenzi mbona OBAMA AMEENDA PALEEE
 
Jan 8th 2014

Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Brother Edward Lowassa, ametembelea miradi ya maji katika kata ya Selela iliyopo Jimbo lake la Mondul na kuongea na wapiga kura wake na kuwapiga vijembe viongozi wa chama chake waliomwambia watamchukulia hatua kali kwa sababu ya kutangaza nia ya kugombea kiti cha urais mwanzoni mwa mwezi hata kwa chama JIWE atakuwa rais 2015.

Brother Lowasa aliwakumbusha akina Nape na Mangula kwamba yeye Uwezo a
nao, nia anayo, wananchi wananipenda wakanitangazia siyo mimi nimetangaza na kuhusu harambee nimechangia kama wenzangu wanavyochangia, au nikiitwa kwenye harambee nisishiriki mpaka uchaguzi wa rais 2015 upite? Hiyo ni adhabu. Tuwe wangalifu na kuchambua maneno, Tusiwe wepesi kulaumu na kuhukumu na pia kuwa kiongozi siyo kutisha na kuogopesha wanachama, wote tuna haki sawa katika chama chetu.

Ni hivi majuzi viongozi wa juu wa CCM walimuonya Lowasa na wananchama wengine wa chama hicho kuacha kujitangazia kuwania urais kupitia CCM kwa vile muda wake rasimi bado na pia kutoa michango ya harambee mbali mbali, na kwa kufanya hivyo ni kuvunja kanuni, sheria za mwongozo wa chama na adhabu yake ni ku-jiqualify automatically wenyewe kwenye kuwania urais. Hata kinana mmoja ndugu sebastiani Kiondo wa Sanawari Arusha alisema vyama siasa nchini vyote lao moja kupigania maslahi yao badala ya wananchi,...ebu niambe ndugu mwandishi Brother Lowasa anakosa gani kama siyo fitina za viongozi wakuu wa CCM?, ukiona hivyo wana mgomea wao tayari na tayari ameshajaza fomu ya kugombea kinachosubiliwa ni siku ya kumtangaza, alimaliza ndugu kiondo kwa masikitiko. —

in Magu Kahangara.








Hii imetulia!
 
Huyu mzee ananifurahisha sana..ana urguments za msingi sana...watu wanapolalamika richmond mara dowans...mi nakuwa sielewi kwa kuwa ndo mitambo hiyo hiyo kaja obama kuizindua..au wao USA hawajui!!!watz amkeni tunaonekana mapimbi sana kwa ajili ya mambo haya

We ushauzwa huna habari tanzania shamba la bibi umebaki wewe kwenda kulima kwenye mashamba ya viazi na mahindi usa dada zako siku hizi wanapelekwa uarabuni ukoloni mambo leo unakuja taratibu.
 
Nani wa kumtema? yeye ndo mwenye uwezo wa kuwatema kama alivyofanya majaribio kwenye kura za marohani baada ya kupata mafanikio sana alitoa suluhisho la kusitisha uasi na ukafanikiwa !
tatizo ni kuwa si mjumbe wa kamati kuu
 
haya embu tuwekee ushaidi wako hapa,na ukishindwa kuweka ushaidi hapa tutaamin ni wivu kama alio nao mama yako mzazi
 
CCM wajikaze tuu..Lowasa kasema sasa nakwenda timiza ndoto zake..TAYARI MACCM WANAANZA PIGANA NAYE....Lowasa si mhaini, si msaliti wa CCM, na katumia haki yake kusema kuwa muda ukifika atakwenda gombea....CCM wanakuja juu.
Maswali ni haya:

-Je CCM wanamchosaupport Zitto tena mhasi na haini mkubwa,kwanini hawawezi hata robo yake kwa Lowasa asiye na kosa kwa vipimo vya CCM?
-Je CCM wameanza mtafuna Lowasa kwa itikadi zao za kutotaka mtu wa kaskazini?
-Au CCM hawmataki lowasa kwa vile ni mkristu?

time would tell.
 
Wakijaribu kumgusa Lowassa ccm itafutika kwenye historia ya vyama vya siasa

Lowasa ni bonge la juha, na ni jitu la kutoswa tu.

1. Alitoswa na Nyerere mpaka mchozi ulimtoka akitaka kugombea uraisi. CCM haikuvunjika.

2. Katoswa na Kikwete uwaziri mkuu kakimbilia Munduli- CCM HAIKUVUNJIKA.'

3. Safair hii atatoswa na kamati kuu na wananchi- CCM HAITAKUFA.

Eleweni kuwa LOwasa hana nguvu hivyo ambavyo Tanzania Daima, Arusha na Kilimanjaro inayompaka.

Atakufa pabaya huyu mzee tena kwa presure.
 
Wanabadili majina tu ya wamiliki lkn mitambo ni ile ile ya Ubungo!

Sisi watz nahisi tumelaaniwa na Mungu;umeme bei juu 78%;matibabu hamna;watoto wote wana feli;maji saafi hamna lkn hapa tunakesha kujadili Zitto na Lowassa na hawala wa Mbowe na sometimes uhusiano wa Dr Slaa
Hizo si agenda na hazipewi nafasi kwenye heading ya vyombo vyetu vya habari hasa magazeti, kiukweli nguvu kubwa tumeiweka kujadili mambo ya utawala na tunasahau mambo ya msingi ya kiuchumi kwani utawala unakwenda sambamba na uchumi
 
Lowasa ni bonge la juha, na ni jitu la kutoswa tu.

1. Alitoswa na Nyerere mpaka mchozi ulimtoka akitaka kugombea uraisi. CCM haikuvunjika.

2. Katoswa na Kikwete uwaziri mkuu kakimbilia Munduli- CCM HAIKUVUNJIKA.'

3. Safair hii atatoswa na kamati kuu na wananchi- CCM HAITAKUFA.

Eleweni kuwa LOwasa hana nguvu hivyo ambavyo Tanzania Daima, Arusha na Kilimanjaro inayompaka.

Atakufa pabaya huyu mzee tena kwa presure.
Ni kwa DIni yake, au ukanda wake...ndio maana CCM mnamzunguka?Hizo Sifa CCM wamekuwa msatri wa mbele sana kuzipiga vita.Kuanzia ktk vyama hadi ktk maish aya kawaida.
 
Lowasa ni bonge la juha, na ni jitu la kutoswa tu.

1. Alitoswa na Nyerere mpaka mchozi ulimtoka akitaka kugombea uraisi. CCM haikuvunjika.

2. Katoswa na Kikwete uwaziri mkuu kakimbilia Munduli- CCM HAIKUVUNJIKA.'

3. Safair hii atatoswa na kamati kuu na wananchi- CCM HAITAKUFA.

Eleweni kuwa LOwasa hana nguvu hivyo ambavyo Tanzania Daima, Arusha na Kilimanjaro inayompaka.

Atakufa pabaya huyu mzee tena kwa presure.

ila cha ajabu hakutoswa na yule mzazi wako wa kike
 
Basi unataka kutuaminisha kuwa CCm na serikali yake wote ni wezi. Haiwezekani lowasa mnamuita fisadi mkubwa na hajawahi kukamatwa na kuhojiwa na polisi wala mahakama. Hii maana yake ni kuwa CCM wote wako hivyo na wakilinganisha wanaona huyu lowasa kuwa angalau kidogo.

Au mnamtaka kapuya awe mgombea ili akabake watoto wetu wa shule za kata?
Kinachoendelea kwa EL ni ushahidi tu kwamba watanzania tuna bongo kama za samaki.eti leo lowassa naye anajadriwa kwenye masuala ya uraisi,tena kibaya zaidi anao wapambe wanaozidi kuongezeka siku hadi siku.imefika mahala eti wapambe wa lowasa wanauliza kwani lowasa alifanya kosa gani?lile halikuwa kosa lake.hivi wamesahau au ni upofu utokanao na pesa anazogawa mithiri ya njugu?hivi ukiacha kashifa ya Richmond huyu bwana ana historia safi kweli?kama huyu jamaa ni msafi nikwanini mwaka 1995 alikwepa mwaliko wa kawawa pale msasani,appointment ambayo ilitakiwa kumkutanisha na nyerere,ili nyerere akamsafishe kama lowasa alivyokuwa ameomba kabla?kwanini maswali ya mwalimu juu ya huyu bwana alivyopata kumiliki mali nyingi kiasi kikubwa cha utajiri alionao,utajiri ambao mwalimu alidai unazidi wakwake yeye aliyekuwa rais wa nchi kwa miaka 23,hayakuwahi kujibiwa mpaka anaingia kaburini?kwanini matakwa ya mwl.nyerere ya ccm kuhitisha cc kwa gharama zake mwenyewe(mwalimu) ili akapate kumsafisha lowasa huko hayakutekelezwa?
 
Basi unataka kutuaminisha kuwa CCm na serikali yake wote ni wezi. Haiwezekani lowasa mnamuita fisadi mkubwa na hajawahi kukamatwa na kuhojiwa na polisi wala mahakama. Hii maana yake ni kuwa CCM wote wako hivyo na wakilinganisha wanaona huyu lowasa kuwa angalau kidogo.

Au mnamtaka kapuya awe mgombea ili akabake watoto wetu wa shule za kata?
beyalala kwani hakuna maisha nje ya ccm?
 
Hukusoma kabisa report ya Mwakyembe iliyomtaka Lowasa na Msabaha kujiuzulu. Unataka kutudanganya mchana kweusi kumbe jua linawaka. Lowasa alikuwa implicated kwenye Richmond kwa vimemo alivyokua anaviadika kushinikiza Richmond ipewe tenda hali akijuwa ni kampuni fake, ya Mwanae.

Sasa unasema ati angemwaibisha rais, kivipi? Kwamba Richmond ilikuwa kampuni ya rais? Kwahiyo Lowasa aliamua kwa kupenda kujiuzulu? Mbona alisubiri report ya Mwakyembe imtimue? Hivi ukiwajibika kwa shinikizo utaitwa shujaa au mharifu? Ni Tz tu na CCM ndio inakumbatia watu wa aina ya Lowasa, Chenge, Rostam, na list ya majangili. Hawa walitakiwa wawe jela na sio kuwa huru kiasi cha wengine kutaka kuwa viongozi wa nchi. Papa Msofe na Masawe sijui wanasubiri nini kutangaza nia ya kugombea ubunge.

usilolijua ni usiku wa giza hakuna kitu ccm kuanzia rais mpk watendaj wake wote hakuna ambaye alikuwa anasalimika kwny richmond kwa chama cha CDM mtu km huyu wangemfuta uanachama sababu hafai saiz ndo anaharibu chama sasa ndo yaleyale ya zitto
 
Endelea kupaka rangi kwenye upepo...EL ni maarufu anakubalika zaidi ya CCM na WanaCCM kwa umoja wao x 1000... I'm afraid so far CCM haina option nyingine zaidi ya EL... Kubali kata ujinyonge ...

issue hapa si umaarufu,issue ni integrity yake as far as presidency is concerned.
 
Huyu mzee ananifurahisha sana..ana urguments za msingi sana...watu wanapolalamika richmond mara dowans...mi nakuwa sielewi kwa kuwa ndo mitambo hiyo hiyo kaja obama kuizindua..au wao USA hawajui!!!watz amkeni tunaonekana mapimbi sana kwa ajili ya mambo haya

Mkuu tatizo haikuwa mitambo, tatizo lilikuwa ni kukiukwa kwa taratibu za manunuzi kwa kujitenegenezeakampuni yake mwenyewe(Richmond) kuipa tenda hiyo na matokeo yake kukawa na ucheleweshaji wa kufika kwa mitambo hiyo ambayo ilifika wakati tatizo la umeme kwa mwaka huo lilikuwa limeisha baada ya dams kujaa tena. Kimsingi huyu jamaa anajua makosa yake ndiyo maana akawa mkimya maana angejaribu kubishana angeweza hata kufa kwa kihoro! Ngoja tusubiri tuone lakini kwa njaa ya wtz tunaweza kumkabidhi nyani kutulindia mahindi yetu mabichi shambani 2015!
 
Back
Top Bottom