Kinachoendelea kwa EL ni ushahidi tu kwamba watanzania tuna bongo kama za samaki.eti leo lowassa naye anajadriwa kwenye masuala ya uraisi,tena kibaya zaidi anao wapambe wanaozidi kuongezeka siku hadi siku.imefika mahala eti wapambe wa lowasa wanauliza kwani lowasa alifanya kosa gani?lile halikuwa kosa lake.hivi wamesahau au ni upofu utokanao na pesa anazogawa mithiri ya njugu?hivi ukiacha kashifa ya Richmond huyu bwana ana historia safi kweli?kama huyu jamaa ni msafi nikwanini mwaka 1995 alikwepa mwaliko wa kawawa pale msasani,appointment ambayo ilitakiwa kumkutanisha na nyerere,ili nyerere akamsafishe kama lowasa alivyokuwa ameomba kabla?kwanini maswali ya mwalimu juu ya huyu bwana alivyopata kumiliki mali nyingi kiasi kikubwa cha utajiri alionao,utajiri ambao mwalimu alidai unazidi wakwake yeye aliyekuwa rais wa nchi kwa miaka 23,hayakuwahi kujibiwa mpaka anaingia kaburini?kwanini matakwa ya mwl.nyerere ya ccm kuhitisha cc kwa gharama zake mwenyewe(mwalimu) ili akapate kumsafisha lowasa huko hayakutekelezwa?