Lowassa asababisha timua timua ITV

Lowassa asababisha timua timua ITV

Hata kama ingetokea alazwe hospitali, bado tutamchagua Lowasa!
 
Afya ya mtu si jambo la kulitumia kisiasa.
Mpaka sasa tumewapoteza wanasiasa Mohamed Mtoi na Deo Filikunjombe(Mungu awalaze pema peponi) ingali ni vijana wenye siha njema!
Usimnyanyapae mtu ilihali wewe hujui ni nini kinachotokea kwenye seli (chembehai) moja ya mwili wako.
 
Ni kudhoofu tu na kukohoa kwa saana lakini sijasikia kama ameshapata kudondoka jukwaani. Nadhani hakuna tatizo saana kama matatizo yake ni hayo tu, kuliko angedondoka jukwaani.
 
Acha watimuliwe tu maana kama watakuwa walifanya hivyo, ni kinyume cha maadili. Pia ukimdharilisha mteja wako ni kuharibu biashara yako. ITV inajiendesha kibiashara na Lowasa ni mteja wao, walitakiwa kulinda heshima na siri zake
 
Wacheni kumkufuru Mungu kwa kumwita Lowassa mgonjwa kama nyiye ndiyo mliomuumba.

Jiulize swali moja tu la msingi ni kwa nini wagombea wengi wanaoonekana kuwa wako fit sana ndiyo wanapukutika na kumwacha Lowassa ambaye anadaiwa kuwa mgonjwa?

Hiyo inatuonyesha namna Mungu anavyotuonyesha utukufu wake mkuu.

Mkuu ahsante Kwa mchango wako.

Ila, sijaelewa huyo Mungu wako, katika hili unavounganisha na uhusiano wa Lowasa.

Kama ni swala la kufa aliye Mzima na kuanchwa aliye mgonjwa, bila shaka anaonyesha Mipango yako ilivyo..

Ila kama, anaua wazima ili kuonyesha Dunia na walimwengu kwamba emeshamteua EL kuwa Rais basi mwambie huyo Mungu wako "this is too low for him". Kwa uwezo wake alikuwa na njia nyingi za kuliwezesha hili.
 
Siku akili zake zikimtuma kufyatua mizinga dhidi ya majirani usije ukaanza kulia maana atakuwa ameamua kigonjwa gonjwa

Atatoa agizo sawa mbinu na mikakati ya kivita ni jukumu la mwamunyange.huyu atatoa ushauri muafaka kama anaridhika kupigana na majirani au la.Uraisi ni taasisi hivyo kuna check na countercheck.
 
The Don Edo hachafukiki hasa kwa muda huu. Kura kwa Edward N. Lowasa. Kura zitalindwa mita 200
 
Mie nimeziona hizo clip kwani uongo?wasiwaonee kuwafukuza kazi jwa kusema ukeeli,kwani uongo
 
Ama kweli mbinu zimewaishia xx swala la ugonjwa wa mtu na sera vina uhusiano gani?? Mwenzenu nae katumia fursa hiyo kujinadi kwa kupiga push up.....Hatima ya maisha ya mtu anaijua mwenyezi Mungu peke yake...Hata huyo mnaemuona ni mzma kwa akili zenu fupi Mungu anaweza akamchukua muda wowote.....
 
Ma-ccm kama endeleeni kumchafua lowasa ila mimi nawahakikishieni kua watu wengi sana wanampenda. Unajua kwa nini? Kwasababu watu hawapendi kuambiwa mtu ni mbaya wanataka kujionea wenyewe na sasa wameona lowasa si mbaya. Kwasababu.... Hamjibu mtu vibaya, na ni mtendaji pia.
 
Huyu mzee simpendi,lakini huwa sioni kama ni jambo la busara kumsimanga afya yake,suala la kuwa mgonjwa halijalish wewe ni tajiri au maskini.tumponde kwa mengine lakini mambo ya afya yake tumuachie yeye na mungu wake.
Brother najua kabisa wewe ni Team Magu lakini umenena
 
Mimi nitampa kura ugonjwa co ishu mana ajuwae bwana Mungu mtu mzima kuwa mfu mgonjwa kuwa salama
 
kulindana huku n shda utakuta mwanzlsh wa maada h n mtu mkubwa kwenye uongoz wa chama tawala kias kwamba hata watu wa mawasiliano wanashndwa hata kumkamata na mm najiulza kwann walioeleza propaganda kuwa meng kajitoa kumdhamn el na taarfa nyngnezo hawajakamatwa licha ya mhusika kukanusha na kuwaomba wanaohusika kuhakksha wahuska wanakamatwa? kwann ukianzsha maada znazoenda knyume na chama tawala m2 anakamatwa? si vzr mm nafkr wa2 wa mawasiliano n watu makn na hawayumbshw na upande wowote na wahuska watatiwa mbaron
 
No wonder nchi yetu ni masikini na inaendelea kudidimia kwa umasikini, hii yote ni kwasababu watu hatujifunzi. Mpiga pushapu mwigulu juzi kaenda chini akashindwa kurudi juu huko tarime...Magufuli naye kaona mnamgeuza katuni mnampigisha pushapu lakini message haiwi delivered na inakuwa kinyume chake kwa kuondoka wazima.
Kuna kipindi kilkuwa kinarushwa na Redio Tanzania Dar es salaam kilikua kinaanza na kufungwa kwa wimbo huu ' Ajuaye Bwana Mungu kwa mzima kuwa mfu mgonjwa kuwa salamaaa leo tunawapeni polee....'
 
Back
Top Bottom