Lowassa anaudhoofisha upinzani

Lowassa anaudhoofisha upinzani

I concur! Lowassa alikuwa asset kipindi cha uchaguzi, kwa sasa anaanza kuwa liability!
Sijasema hivyo. 90% hasara ila 10% faida kwa kukuza ruzuku ya cdm na wabunge wa kike ambao bungeni kazi ni moja tu....kuuza sura.
 
Thats your fair opinion,
Lowassa hajaua upinzani, siasa za sasa si siasa za kianaharakati au siasa za hoja kwa hoja...(Lissu ni classical example wa hili)
Pili indicator ya kujua kama upinzani umekufa au umedorora hadi sasa ni kura pekee...
Tukutane 2019 kwenye serikali za mitaa.

Hata hivyo nikubaliene na wewe kias kuwa upinzani wamegwaya kidogo.. na ukweli ni kwamba hii mikwara si ya kitoto...

Niongeze kusema pia kuwa Chadema inahitaji mabadiliko ya ngazi ya juu ya uongozi... tunataka watu wenye pumzi ndefu na wasioogopa kupoteza kitu...
1.Lissu
2.Lema
3.Msigwa
4. Masha
5.Wenje

Suala la dini hapo ni wao watakavoamua kubalancisha mambo

Hadi sasa huwezi acha mashine kama za kina Nyalandu, Mahanga, Sumaye et all wakabaki hivi hivi bila kazi maalumu...
Lazima washiriki kwenye kanda kadhaa katika kujenga chama kitakachoheshimiwa na top class citizen and business class.

Lowassa alicholeta chadema ni heshima kwa kundi na marika mbali mbali na madaraja ya juu ya wananchi.. hasa wafanyabiashara na viongozi wastaafu, si mtu wa kubeza hata kidogo kwa mpenda mabadiliko yeyote yule...
Hata Nyalandu ni tatizo pia. Lakini hata Tundu anaona wamelamba dume. Nchi hii hope is gone kwa upinzani makini
 
Lowassa alijiunga upinzani baada ya kudhulumiwa Urais ccm. Vinginevyo hakuwa na khoja ya kuwa mpinzani. Hivyo, ni masilahi binafsi siyo sera zimempeleka upinzani.

La ajabu, upinzani uchwara tulionao unamwona ni JEMBE!

Lowassa siyo mpinzani hata chembe ila anatumiwa na ccm kudhoofisha upinzani.

Maswali ya kujiuliza

1) Mbona hasumbuliwi kwa kuwekwa ndani na kufikishwa Mahakamani kama wengine?

2) Mbona hakerwi na mfumo mzima wa chaguzi zetu? Lini ulimsikia akihimiza mageuzi ndani ya sheria za uchaguzi hususani NEC?

3) Mbona hajawahi kuomba msamaha kwa kuwapotosha wapigakura alipowaahidi suala la kulinda kura ni lake aachiwe na baada ya kushindwa akadai aliibiwa?

4) Mbona hadi leo hajatoa majumuisho ya kura alizozipata hususani fomu za vituo na za majimbo kutuhakikishia ya kuwa alishinda kwa 62% kama alivyodai?

5) Mbona hadi leo hajaenda Mahakama kuu kuiomba kibali cha kuhesabu kura zote ili tujue mbichi ni zipi ?

6) Mbona hajalalama marekebisho ya sheria za mgao wa ruzuku zinazolenga kuusambaratisha UKAWA?

7) Mbona hadi leo kaufyata kupigania haki ya kikatiba ya upinzani kuendesha shughuli zao bila vikwazo na vitisho?

NIONAVYO

Lowassa ni CCM mole yuko huko kuwadhoofisha kwa kuwatupia changa la macho kwa kuboresha ruzuku ili wasahau mambo ya kimsingi kama NEC kututendea haki wapigakura.

Lowassa has too much to lose and too much baggage to carry to represent a lynchpin of change we are looking for....
Mzee wa mabadiriko
 
Hana mission yoyote, yeye kaja cdm baada ya kukosa nafasi ya kugombea urais huko ccm. Ila yeye sio aina ya mtu anayefaa kwa siasa za cdm, kwanza ni mzee na muda wake umeshapita, na toka alivyokuja hana jipya aliloleta chamani, labda wanaojua faida yake ni viongozi nyuma ya pazia. Mimi kama mimi siwezi kumuunga mkono Lowassa japo nitaendelea kuipenda cdm na nitaendelea kumpinga waziwazi bila kupepesa macho.
La ajabu, anajichua tena kwa 2020 badala ya kuandaa damu changa
 
Sheria za Tanzania ni tofauti sana na zile za Kenya. Matokeo ya urais hayahojiwi kwa namna yoyote ile mahakamani.
Sijazungumzia kuhoji matokeo bali kurudia kuzihesabu kura. Kura hutunzwa kwa miaka 3 kwaajili hiyo. Kuhesabu hakitengui matokeo bali ni kuhakiki kujihakikishia zoezi halina walakini kama upo kutafuta chanzo ili kuboresha chaguzi zijazo.
 
Hivi kwa mfano uchaguzi ujao jina lake lisipopitishwa na peoples kugombea uraisi na badala yake akajitokeza mwanachama mwenye nguvu na mvuto wa kisiasa zaidi yake ataendelea kubaki hapo peoples?
Atabaki sioni wapi atakwenda
 
Mbona ni wagumu wa fadhila mafuriko yote yale na amesaidia ruzuku ya chama kuongezeka!
Ruzuku na idadi ya wabunge ni mchango mkubwa hakuna ubishi lakini chama cha siasa ni kushika dola siyo kupapasa
 
Makamanda akili zimeanza kurudi ....tunaitaka CDM ile .....ile isiyoogopa chochote ....ile iliyokesha viwanja vya NMC ....ile iliyopigwa bomu .....ile iliyofanya Mwangosi akauawa ...ile si hii ....
Kwa uongozi upi?
 
Tz n ya aman ameona akkomaa dunia yote itameangalia yy
Mwenye nacho tangia lini akahatarisha mali zake jiulize. Suala kama ni amani yetu kwa nini hakubaki ccm kama Malecela n.k?
 
Kama sio nguvu za yule mtaalamu wa tehama saa hizi EL angekuwa yupo zake magogoni . Mwanatehama alifanya yake JPM akamalizia na usemi huu" Mimi John Pombe Magufuli ndiyo Rais basii!!"
 
Kama sio nguvu za yule mtaalamu wa tehama saa hizi EL angekuwa yupo zake magogoni . Mwanatehama alifanya yake JPM akamalizia na usemi huu" Mimi John Pombe Magufuli ndiyo Rais basii!!"
Angeliomba vote recount inaruhusiwa na sheria za uchaguzi kifungu cha 35(2)....

Screenshot_2017-11-10-00-07-47.png
 
2015 Chadema ingemsimamisha mgombea yeyote yule tofauti na lowassa,JPM angeshinda kwa 90%.

Mwacheni mtu anayeitwa Mbowe,mwenyekiti pekee asiyependa kugombea urais kama wengine.

Wanasiasa bora Tanzania ni Kikwete na Mbowe tu.

2015 Jk alimzidi ujanja Mbowe sehemu ndogo sana,lakini karata ya Mbowe ilikua ni Bonge la dili.

Jamani mwacheni Mbowe,ni next level.Bila yeye chadema ingekua kama CUF ya leo hii.
 
2015 Chadema ingemsimamisha mgombea yeyote yule tofauti na lowassa,JPM angeshinda kwa 90%.

Mwacheni mtu anayeitwa Mbowe,mwenyekiti pekee asiyependa kugombea urais kama wengine.

Wanasiasa bora Tanzania ni Kikwete na Mbowe tu.

2015 Jk alimzidi ujanja Mbowe sehemu ndogo sana,lakini karata ya Mbowe ilikua ni Bonge la dili.

Jamani mwacheni Mbowe,ni next level.Bila yeye chadema ingekua kama CUF ya leo hii.

Kwa taarifa iwapo cdm wangemsimamisha Slaa ambaye tayari alikuwa kwenye mitazamo ya wengi, huenda cdm isingeshinda lakini ingepata kura nyingi zaidi za urais, ingepata wabunge na madiwani wengi zaidi ya sasa. Kubwa zaidi ingeiacha cdm imara na sera yake kubwa ya kupinga ufisadi. Leo hii isingekuwa imeharibu haiba yake ya kuwa chama safi kwani nacho sasa kinaonekana kinakumbatia wachafu na hakina ubavu wa kukemea ufisadi kama chama.

Unasema Mbowe hana nia ya kugombea urais , sio hana nia bali hana sifa za kugombea urais kwani ili ugombee urais unatakiwa wangalau uwe na degree kwa sasa kitu ambacho Mbowe hana.

Hilo la kwamba Mbowe na Kikwete ni wenyeviti bora hakuna anayekupinga kwani ni maoni yako. Kwa mtazamo wangu Mbowe amefanya vizuri sana kabla ya kosa la kiufundi la kumpokea Lowassa na kumpa nafasi ya kugombea urais. Ila kwa sasa ni vyema akakaa pembeni aache taasisi imara ya cdm ikisonga mbele, yeye awe mshauri tu.
 
Ni hivi mimi ni mshabiki wa upinzani na hasa cdm, sikuwahi kuumuunga mkono Lowassa na nililalamika kwamba lile ni kosa kubwa haswa baada ya ule upuuzi aliokuwa akiufanya Shibuda. Nilitarajia upinzani na hasa cdm watakuwa walijifunza kuhusu kupokea makapi toka ccm na kuyapa nafasi, cha kushangaza ndio wakafanya kosa kubwa kuliko yote ya kumpokea Lowassa na kumpa nafasi namba moja katika chama ya kugombea urais.

Matokeo yake baada ya Lowassa kuingia cdm, cdm kimegeuka kuwa chama cha kikondoo, hakuna lolote jipya aliloleta Lowassa ndani ya cdm zaidi ya kuwinda nafasi ya kugombea urais tena kwa faida ya CCM. Mambo yaliyoipa cdm nguvu huko nyuma yote yamemezwa na ujio wa Lowassa, kiasi kwamba wanaposema Mbowe na uongozi wa juu walihongwa kutoa nafasi ya kugombea urais kwa Lowassa inakuwa ni ukweli. Leo hii Magufuli na ubovu wake katika uongozi anaonekana ni bora kwani analinganishwa na Lowassa. Lowassa hajawahi kuwa mwanasiasa wa aina ya siasa za cdm, ubora wake wote huwa unaimbwa na wapambe lakini sio yeye.

Nashangaa wapenzi washabiki na wanachama wa cdm kuwa kimya wakati chama kimeendelea kufubaa kwa sababu ya uwepo wa Lowassa. Hili tukubali la kuendelea kuwa na Lowassa ndani y ya cdm ni kuimaliza cdm, ni wakati wa wote wanaoitakia mema cdm kupinga Lowassa kukaa nafasi za mbelembele kwenye mambo ya chama kwani hana mapenzi na chama zaidi ya kuhakikisha cdm inampa nafasi ya kufikia matakwa yake. Huyo Mbowe sio wa kumuacha tena aamue lolote kwani amekiharibu chama kwa faida yake ya muda mfupi.
Sijui kwanini kiwango cha kufikiri kinashuka sana. Hivi Lowasa ukiacha nafasi ya kugombea urais, sasa hivi ni nani ndani ya chama? Hivi mlitegemea siasa za Chadema zisibadilike awamu hii? Kutumia Lowasa kama kiini cha mabadiliko ya siasa za Chadema katika mtazamo wa kwamba chama kimepoteza mwelekeo wake ni makosa makubwa. Inavyoonekana kuna wengi wetu hamuelewi nchi iko katika hali gani.
 
Back
Top Bottom