Kwa taarifa iwapo cdm wangemsimamisha Slaa ambaye tayari alikuwa kwenye mitazamo ya wengi, huenda cdm isingeshinda lakini ingepata kura nyingi zaidi za urais, ingepata wabunge na madiwani wengi zaidi ya sasa. Kubwa zaidi ingeiacha cdm imara na sera yake kubwa ya kupinga ufisadi. Leo hii isingekuwa imeharibu haiba yake ya kuwa chama safi kwani nacho sasa kinaonekana kinakumbatia wachafu na hakina ubavu wa kukemea ufisadi kama chama.
Unasema Mbowe hana nia ya kugombea urais , sio hana nia bali hana sifa za kugombea urais kwani ili ugombee urais unatakiwa wangalau uwe na degree kwa sasa kitu ambacho Mbowe hana.
Hilo la kwamba Mbowe na Kikwete ni wenyeviti bora hakuna anayekupinga kwani ni maoni yako. Kwa mtazamo wangu Mbowe amefanya vizuri sana kabla ya kosa la kiufundi la kumpokea Lowassa na kumpa nafasi ya kugombea urais. Ila kwa sasa ni vyema akakaa pembeni aache taasisi imara ya cdm ikisonga mbele, yeye awe mshauri tu.