Lowassa anaudhoofisha upinzani

Lowassa anaudhoofisha upinzani

Kwa taarifa iwapo cdm wangemsimamisha Slaa ambaye tayari alikuwa kwenye mitazamo ya wengi, huenda cdm isingeshinda lakini ingepata kura nyingi zaidi za urais, ingepata wabunge na madiwani wengi zaidi ya sasa. Kubwa zaidi ingeiacha cdm imara na sera yake kubwa ya kupinga ufisadi. Leo hii isingekuwa imeharibu haiba yake ya kuwa chama safi kwani nacho sasa kinaonekana kinakumbatia wachafu na hakina ubavu wa kukemea ufisadi kama chama.

Unasema Mbowe hana nia ya kugombea urais , sio hana nia bali hana sifa za kugombea urais kwani ili ugombee urais unatakiwa wangalau uwe na degree kwa sasa kitu ambacho Mbowe hana.

Hilo la kwamba Mbowe na Kikwete ni wenyeviti bora hakuna anayekupinga kwani ni maoni yako. Kwa mtazamo wangu Mbowe amefanya vizuri sana kabla ya kosa la kiufundi la kumpokea Lowassa na kumpa nafasi ya kugombea urais. Ila kwa sasa ni vyema akakaa pembeni aache taasisi imara ya cdm ikisonga mbele, yeye awe mshauri tu.
Nani alikwambia Mbowe hana degree?
 
Pole umepotea njia bila kujua mimi najua ukweli ulivyo kuliko wewe unayejua ukweli wa propaganda. Baadhi ya watu waliofanya mpango wa Lowassa kuja cdm, Slaa ndio alikuwa kinara. Ila hakutaka akija apewe nafasi ya kugombea urais kwani hiyo aliona ni haki yake na kweli alistahili. Tatizo lililojitokeza mpaka ikawa ilivyokuwa ni muungano wa Ukawa. Muungano huu ulitawaliwa na mitazamo ya nani haswa alipaswa kubeba jukumu la kugombea urais. Ushindani ukawa ni baina ya Lipumba na Slaa. Cuf waliona Lipumba anafaa na cdm waliona Slaa anafaa.

Kumbuka huu ulikuwa ni ushindani baina ya ccm dhaifu iliyokuwa inaogopa kupoteza dola lakini ikiwa na dola mkononi, na Ukawa yenye nguvu. Kwa mtazamo wao Cuf wakaona Slaa atapata shida kuungwa mkono na waisilamu kwani ilifahamika ccm wamejipanga kutumia siasa chafu kama kawaida yao ya kuongozwa na padri. Na cdm wakawa wanaona Lipumba hana ushawishi kama alivyokuwa huko nyuma. Hivyo bahati ikamuangukia Lowassa kwani naye alikuja na mzigo wake nyuma ya pazia, na pia kuuaminisha umoja huo kwamba yeye anaungwa mkono mpaka na wanaccm. Hivyo ili kuondoa mvutano wa Slaa na Lipumba, karata ikamuangukia Lowassa, huku Slaa na Lipumba wakiwa hawajaridhika na maamuzi hayo. CCM kwa kugundua tatizo hilo ndio wakawaribuni Slaa na Lipumba, na mengine kwa sasa ni historia. Kwa hiyo sio Slaa wala Lipumba waliondoka kwa ajili ya kuona eti Lowassa aliitwa fisadi, bali ushindani wao ndio uliosababisha Lowassa kuchukua nafasi waliyoitegemea wao. Na maadamu ccm hawakuwafuata mikono mitupu ulitegemea nini? Hivyo hilo la ufisadi ilikuwa ndio kete pekee ya kuaminisha watanzania. Matokea ya chochote kitu toka ccm ndio leo unamuona Lipumba anapata support ya wapi, na Slaa huko alipo hathubutu kuchangia dhidi ya ccm enzi zake.
Pole sana kwa kua uliendelea kua punda aliefungwa hatamu na ukaburuzwa na mahaba kipindi hicho haya yote hukuyaona wala kuyasema nini leo kimekuudhi kwa kipenzi chenu!
 
Ni hivi mimi ni mshabiki wa upinzani na hasa cdm, sikuwahi kuumuunga mkono Lowassa na nililalamika kwamba lile ni kosa kubwa haswa baada ya ule upuuzi aliokuwa akiufanya Shibuda. Nilitarajia upinzani na hasa cdm watakuwa walijifunza kuhusu kupokea makapi toka ccm na kuyapa nafasi, cha kushangaza ndio wakafanya kosa kubwa kuliko yote ya kumpokea Lowassa na kumpa nafasi namba moja katika chama ya kugombea urais.

Matokeo yake baada ya Lowassa kuingia cdm, cdm kimegeuka kuwa chama cha kikondoo, hakuna lolote jipya aliloleta Lowassa ndani ya cdm zaidi ya kuwinda nafasi ya kugombea urais tena kwa faida ya CCM. Mambo yaliyoipa cdm nguvu huko nyuma yote yamemezwa na ujio wa Lowassa, kiasi kwamba wanaposema Mbowe na uongozi wa juu walihongwa kutoa nafasi ya kugombea urais kwa Lowassa inakuwa ni ukweli. Leo hii Magufuli na ubovu wake katika uongozi anaonekana ni bora kwani analinganishwa na Lowassa. Lowassa hajawahi kuwa mwanasiasa wa aina ya siasa za cdm, ubora wake wote huwa unaimbwa na wapambe lakini sio yeye.

Nashangaa wapenzi washabiki na wanachama wa cdm kuwa kimya wakati chama kimeendelea kufubaa kwa sababu ya uwepo wa Lowassa. Hili tukubali la kuendelea kuwa na Lowassa ndani y ya cdm ni kuimaliza cdm, ni wakati wa wote wanaoitakia mema cdm kupinga Lowassa kukaa nafasi za mbelembele kwenye mambo ya chama kwani hana mapenzi na chama zaidi ya kuhakikisha cdm inampa nafasi ya kufikia matakwa yake. Huyo Mbowe sio wa kumuacha tena aamue lolote kwani amekiharibu chama kwa faida yake ya muda mfupi.
Ni wapinzani wachache sana wanaojua hilo. Wanachojua wao ni kutukana matusi.
 
mimi mengine siyajui ila ninalolijua kwa hakika ni kwamba tokea lowassa kahamia cdm makamanda wamekuwa waoga kichizi!!!!!
mbowe ndio kawa mwoga kabisa,halima got more balls than him..
after it's been said and done,slaa ndio hana uwezo kabisa wa kupata kura za kutosha.
 
Lowassa alijiunga upinzani baada ya kudhulumiwa Urais ccm. Vinginevyo hakuwa na khoja ya kuwa mpinzani. Hivyo, ni masilahi binafsi siyo sera zimempeleka upinzani.

La ajabu, upinzani uchwara tulionao unamwona ni JEMBE!

Lowassa siyo mpinzani hata chembe ila anatumiwa na ccm kudhoofisha upinzani.

Maswali ya kujiuliza

1) Mbona hasumbuliwi kwa kuwekwa ndani na kufikishwa Mahakamani kama wengine?

2) Mbona hakerwi na mfumo mzima wa chaguzi zetu? Lini ulimsikia akihimiza mageuzi ndani ya sheria za uchaguzi hususani NEC?

3) Mbona hajawahi kuomba msamaha kwa kuwapotosha wapigakura alipowaahidi suala la kulinda kura ni lake aachiwe na baada ya kushindwa akadai aliibiwa?

4) Mbona hadi leo hajatoa majumuisho ya kura alizozipata hususani fomu za vituo na za majimbo kutuhakikishia ya kuwa alishinda kwa 62% kama alivyodai?

5) Mbona hadi leo hajaenda Mahakama kuu kuiomba kibali cha kuhesabu kura zote ili tujue mbichi ni zipi ?

6) Mbona hajalalama marekebisho ya sheria za mgao wa ruzuku zinazolenga kuusambaratisha UKAWA?

7) Mbona hadi leo kaufyata kupigania haki ya kikatiba ya upinzani kuendesha shughuli zao bila vikwazo na vitisho?

NIONAVYO

Lowassa ni CCM mole yuko huko kuwadhoofisha kwa kuwatupia changa la macho kwa kuboresha ruzuku ili wasahau mambo ya kimsingi kama NEC kututendea haki wapigakura.

Lowassa has too much to lose and too much baggage to carry to represent a lynchpin of change we are looking for....
Lowasa hawezi kuiacha CHADEMA salama.
 
2015 Chadema ingemsimamisha mgombea yeyote yule tofauti na lowassa,JPM angeshinda kwa 90%.

Mwacheni mtu anayeitwa Mbowe,mwenyekiti pekee asiyependa kugombea urais kama wengine.

Wanasiasa bora Tanzania ni Kikwete na Mbowe tu.

2015 Jk alimzidi ujanja Mbowe sehemu ndogo sana,lakini karata ya Mbowe ilikua ni Bonge la dili.

Jamani mwacheni Mbowe,ni next level.Bila yeye chadema ingekua kama CUF ya leo hii.

Hahahahah basi wanasiasa wameisha kama huyu naye yumo
 
Lowassa Mimi namfananisha na kwenye Timu.Si mzuri kulazimisha kufunga kwahiyo Timu ikibanwa basi unaona kapwaya kama Lukaku Lakini Timu Pinzani ikiwa haipaki Basi Lowassa utafurahi atakavyotikisa Nyavu.Maana yangu sasa CDM wamebanwa na Mzee Lowassa si mtu wa kulazimisha kuongea.Mikutano ingeruhisiwa usingemuona amepwaya namna hii.Kila laheri
 
Pole sana kwa kua uliendelea kua punda aliefungwa hatamu na ukaburuzwa na mahaba kipindi hicho haya yote hukuyaona wala kuyasema nini leo kimekuudhi kwa kipenzi chenu!

Kipara kipya naona unadhani mimi ninaongea kishabiki kama ww. Narudia kukuambia ukiweza unaweza kupitia post zangu kama kuna mahali niliwahi kumshabikia Lowassa toka akiwa ccm au alipohamia cdm. Sikuwahi na wala sintowahi. Siko hapa kumzuia Lowassa kuwa mwana cdm au kuzuia asipewe cheo chochote, ninachosema ni mtazamo wangu kwamba hana faida kwa cdm kama chama. Mimi sio mwanachama wa cdm bali ni shabiki wa kutupwa wa cdm. Hivyo sina nafasi kwenye vikao vya maamuzi kwa hiyo nafasi yangu kukikosoa na kukishauri ni hapa jukwaani. Kama wengine wanaona anafaa siwezi kupinga mitazamo yao ila mimi kama mimi Lowassa hapana.
 
1) Mbona hasumbuliwi kwa kuwekwa ndani na kufikishwa Mahakamani kama wengine?
hajafanya chochote cha kumfanya afikishwe mahakamani

2) Mbona hakerwi na mfumo mzima wa chaguzi zetu? Lini ulimsikia akihimiza mageuzi ndani ya sheria za uchaguzi hususani NEC?
Amesema mara nyingi tu...Ingawa nakubaliana na wewe kuna udhaifu wa Ujumla wa Wapinzani katika kulivalia njuga suala hilo.

3) Mbona hajawahi kuomba msamaha kwa kuwapotosha wapigakura alipowaahidi suala la kulinda kura ni lake aachiwe na baada ya kushindwa akadai aliibiwa?
kwa hili kwa kweli aliniudhi sana...watu tumepiga kura kinoma..katudanganya atazilinda...aaaa..wapi?

4) Mbona hadi leo hajatoa majumuisho ya kura alizozipata hususani fomu za vituo na za majimbo kutuhakikishia ya kuwa alishinda kwa 62% kama alivyodai?
Alete kwa sasa ili iweje? alafu nini kifanyike? it will be wastage of time and resources....Pia hukumbuki vijana wa Chadema waliokuwa wanafanya hilo zoezi waliwekwa ndani takribani miezi 6

5) Mbona hadi leo hajaenda Mahakama kuu kuiomba kibali cha kuhesabu kura zote ili tujue mbichi ni zipi ?
Katiba Ya Tanzania hairuhusu kamwe matokeo ya Urais kuhojiwa POPOTE Pale MBUINGUNI AMA DUNIANI...Akishatamka mwenyekiti wa TUME YA UCHAGUZI Kuwa rais ni Fulani basi imetoka hiyo..Kwa Lugha Rais mwaka 2015 Kama LUBUVA angetangaza Mshindi ni HASHIM RUNGWE SPUNDA...Basi hakuna kima yoyote aliyepaswa kuhoji

) Mbona hadi leo kaufyata kupigania haki ya kikatiba ya upinzani kuendesha shughuli zao bila vikwazo na vitisho?
Unataka afanyeje ndugu yangu.....

Ingawa nakubaliana na wewe kuwa Aina ya Siasa za Lowasa zinashusha ari ya Upinzani nchini,lakini mchango wake pia ni mkubwa.Tunamheshimu sana

Kilichopaswa kufanywa na ndicho kinachofanywa ni Lowasa kuwekwa Pembeni na kubaki kama mshauri
 
ata Nyalandu ni tatizo pia. Lakini hata Tundu anaona wamelamba dume. Nchi hii hope is gone kwa upinzani makini
hapa sikubaliani na wewe,..Nyalandu ni JEMBE...Wanyaturu huwa ni watu smart sio wa kubebwabebwa tu
Nyalandu is the real deal
Time will tell
 
Kipara kipya naona unadhani mimi ninaongea kishabiki kama ww. Narudia kukuambia ukiweza unaweza kupitia post zangu kama kuna mahali niliwahi kumshabikia Lowassa toka akiwa ccm au alipohamia cdm. Sikuwahi na wala sintowahi. Siko hapa kumzuia Lowassa kuwa mwana cdm au kuzuia asipewe cheo chochote, ninachosema ni mtazamo wangu kwamba hana faida kwa cdm kama chama. Mimi sio mwanachama wa cdm bali ni shabiki wa kutupwa wa cdm. Hivyo sina nafasi kwenye vikao vya maamuzi kwa hiyo nafasi yangu kukikosoa na kukishauri ni hapa jukwaani. Kama wengine wanaona anafaa siwezi kupinga mitazamo yao ila mimi kama mimi Lowassa hapana.
Nimekuelewa dogo maamuzi yote anayo mbowe!
 
hapa sikubaliani na wewe,..Nyalandu ni JEMBE...Wanyaturu huwa ni watu smart sio wa kubebwabebwa tu
Nyalandu is the real deal
Time will tell
Samahani ungejaribu kutudadavulia. Nyalandu ni jembe kivipi? Au kwa sababu kahamia chadema
 
Kuwapa misifa majizi wa CCM wa miaka nenda miaka rudi pindi wanapoenda upinzani kunadhoofisha nguvu na ari za wapambanaji wa ukweli na waasisi wa upinzani halisi. Kwenye hili wapinzani halijakaa vizuri . Anayekuja aje ila kumwagia masifa yauwongo uwongo sio vizuri. CCM ni wezi hata waende wapi ni wezi na hata wabadilike ngozi bado ni wezi tu uangalifu unatakiwa maana hao wamezoea matendo ya kiCCM.
 
Nimekuelewa dogo maamuzi yote anayo mbowe!

Hilo la Mbowe kuwa na maamuzi yote halina ubishi, ila kitendo cha yeye kuwa na maamuzi yote hata mabovu ni udhaifu wa wanachama dhidi ya mwenyekiti wao.
 
Back
Top Bottom