Lowassa anaudhoofisha upinzani

Lowassa anaudhoofisha upinzani

Lowassa alijiunga upinzani baada ya kudhulumiwa Urais ccm. Vinginevyo hakuwa na khoja ya kuwa mpinzani. Hivyo, ni masilahi binafsi siyo sera zimempeleka upinzani.

La ajabu, upinzani uchwara tulionao unamwona ni JEMBE!

Lowassa siyo mpinzani hata chembe ila anatumiwa na ccm kudhoofisha upinzani.

Maswali ya kujiuliza

1) Mbona hasumbuliwi kwa kuwekwa ndani na kufikishwa Mahakamani kama wengine?

2) Mbona hakerwi na mfumo mzima wa chaguzi zetu? Lini ulimsikia akihimiza mageuzi ndani ya sheria za uchaguzi hususani NEC?

3) Mbona hajawahi kuomba msamaha kwa kuwapotosha wapigakura alipowaahidi suala la kulinda kura ni lake aachiwe na baada ya kushindwa akadai aliibiwa?

4) Mbona hadi leo hajatoa majumuisho ya kura alizozipata hususani fomu za vituo na za majimbo kutuhakikishia ya kuwa alishinda kwa 62% kama alivyodai?

5) Mbona hadi leo hajaenda Mahakama kuu kuiomba kibali cha kuhesabu kura zote ili tujue mbichi ni zipi ?

6) Mbona hajalalama marekebisho ya sheria za mgao wa ruzuku zinazolenga kuusambaratisha UKAWA?

7) Mbona hadi leo kaufyata kupigania haki ya kikatiba ya upinzani kuendesha shughuli zao bila vikwazo na vitisho?

NIONAVYO

Lowassa ni CCM mole yuko huko kuwadhoofisha kwa kuwatupia changa la macho kwa kuboresha ruzuku ili wasahau mambo ya kimsingi kama NEC kututendea haki wapigakura.

Lowassa has too much to lose and too much baggage to carry to represent a lynchpin of change we are looking for....
Sasa kama ni CCM nini kinakuuma? Ujinga tu mnaandika
 
Naheshimu mtazamo wako. Ila sina hakika ya moja kwa moja wapiga kura wengi kujali CV sana zaidi ya uwezo wa kuwashawishi jukwaani. Sipingi mtazamo wako.
Nakuelewa mkuu ila labda unipe mtazamo wako je slaa angeweza kugawa kura za CCM iliyoungana na bila makundi??
 
Nu kkweli wapinzani wanaudhoofisha uongozi, lakini mjue chdema inatumika kijanjaa kuiimarisha ccm, mhgesimama kwa hoja mngeshindaaa sana tuu,
 
Mkuu tufanye rejea ya jina lako kwanza. Nadhani hoja zako ni nyepesi sana na kimsingi sijaona mantiki zake, labda tuangalie kwa jicho lingine kwa walio shikamoo ushukani.

Mfano juu ya mgogoro mkubwa wa nyuma na Western countries. Tuseme sasa wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa hadi tunaona ni jambo la kawaida?
 
Ila lowasa nae katulia sana daaa,ata mi naanza mshtukia,yeye anasubl tu uchaguz agombee urais bla kufanya harakat,hapana chadema tunapaswa kujtazama
 
Nakuelewa mkuu ila labda unipe mtazamo wako je slaa angeweza kugawa kura za CCM iliyoungana na bila makundi??

Mkuu kwa dhati ya moyo wangu bado Slaa angekuwa best candidate kwa cdm tena hata bila ya muungano wa Ukawa. Na kikubwa zaidi hata kama angeshindwa bado chama kingekuwa na nguvu kubwa ya kuibana ccm sasa hivi bila chama kuonekana kimbilio la watu wenye makandokando toka ccm. Kwanza Slaa alikuwa ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja jukwaani kuliko Lowassa. Alikuwa anazifahamu vyema siasa za upinzani na udhaifu wa ccm kuliko Lowassa.

Slaa aliandaa mazingira mazuri ya ushindani wa hoja na sera za kuuza kwa wananchi tena kwa mdomo wake kuliko Lowassa aliyesema ilani iko kwenye mtandao!! Slaa ndiye haswa aliyechangia ccm kumchagua Magufuli kwani ndiye waliyeona wangalau ana rekodi nzuri ya utendaji wa kuweza kushindana na Slaa, japo wanamjua ni mtu wa maamuzi ya kukurupuka na jazba bila kujali matokeo yake kama inavyodhihirika sasa. Tukubali tu kwa kumpokea Lowassa tulitema big G kwa karanga za kuonjeshwa. Matokeo yake ndio leo hatuna ile kete yetu na Lowassa hana ubavu wa kushindana na siasa za aina ya Magufuli kwani si msafi japo Magufuli sio msafi sana lakini ndio mwenye dola. Iwapo ccm wangejua Slaa sio atakayegombea nakuhakikishia Magufuli urais angeusikia kwenye bomba.
 
Sipingi hoja zako moja kwa moja hasa msimamo wa Dr. Slaa linapokuja suala la misamamo yake toka kuacha upadre na hasa hasa huyo Lowassa. Kwa kiasi kikubwa sikuridhika na maamuzi ya Slaa kukiacha chama japo niliheshimu sana maamuzi yake. Ila nilichogundua Slaa ni mtu mwenye misimamo mikali ambayo wakati mwingine inaweza isimpate kila anachokitaka. Leo hii tunawaona wanaccm wakatuhumu na kukashifu wapinzani wanaposusia mijadala kwa kusema njia nzuri sio kukimbia bali kubaki na kujadili mpaka mwisho. Iweje leo wanaccm muonyeshe kuunga kitendo cha Slaa kukimbia chama chake badala ya kubaki na kupambana akiwa chamani mpaka kieleweke? Simply huu unaoleta ni unafiki wa kiccm.

Ni kweli kuwapokea wanachama wenye makando kando sio jambo zuri sana, lakini nikuulize, kama kweli ccm huwa inashinda kihalali kwanini hawa hawa wenye makando kando wanashinda wakiwa ccm? Huoni kwamba wapiga kura wanachagua bila kujali makando kando ya wagombea? Kama wapiga kura huwa wanachagua kihalali basi wakulaumiwa ni wao kwani wanaccm wengi wanasifa mbaya za wazi na za kificho lakini bado wanashinda uchaguzi. Kwa hiyo cdm wanaweza wasilaumiwe sana kwani wao huwa wanachagua bila kujali sifa za mgombea. Vinginevyo uniambie kwamba ushindi wa hao wagombea wenye sifa mbaya sio kikwazo cha wapiga kura. Mfano Lowassa alikuwa nia hiyo sifa mbaya kuliko Magufuli. lakini alipata kura milioni 6+ akawashinda akina Mama Mghirwa, Dovutwa, Hashimu Rungwe nk ambao hawakuwa na sifa mbaya za kifisadi.

Wangalau hili la kutowapa uongozi ninakuunga mkono. Hata mimi nimeshapendekeza sana humu jukwaani kwamba cdm iepuke sana kuwapa nafasi za kugombea wanachama toka vyama vingine haswa ccm tena wale wenye makando kando. Sikuishia hapo nikapendekeza pia mtu ili aweze kupata nafasi ya kugombea hasa aliyetoka chama kingine wangalau atumikie chama miaka sio chini ya miwili, kisha ndio apatiwe nafasi ya kugombea kama anataka. Sio lazima chama wafanyie kazi mapendekezo yangu ila wakifanyia kazi mapendekezo haya yanaweza kusadia baadhi ya mambo tofauti na ilivyo sasa.
Nimekuelewa sana pia nathamini sana mawazo yako. Lakini elewa uanachama unaweza uita ni utamaduni. Kuna watu wana imani kwamba upinzani wakishinda watavunja amani tuliyonayo. Hao ni wengi huko vjjn na ndiyo wanaowapa kura kina Lowasa na wa aina yake. Kwa uthibitisho huo iangalie Monduli ilivyo.

Lakini elewa mm ni mtz nisiye na itikadi ya chama chochote. Mm naamini katika mtu na siyo katika chama. Kwa ujumla sina chama. Kidogo cdm ilinishawishi kuipenda lkn kwa hii ya akina Lowasa sumaye Nyalandu kwa kweli aina sbb tena ya kuiunga mkono
 
Sijawahi kuona MTU ambaye si asset, kisha mkapoteza muda wenu kumwongelea humu. Mbona hamuwaongelei akina Mrema au Cheyo?? Mnafurahishana tu wenyewe na unafiki wenu.
 
Lowassa alijiunga upinzani baada ya kudhulumiwa Urais ccm. Vinginevyo hakuwa na khoja ya kuwa mpinzani. Hivyo, ni masilahi binafsi siyo sera zimempeleka upinzani.

La ajabu, upinzani uchwara tulionao unamwona ni JEMBE!

Lowassa siyo mpinzani hata chembe ila anatumiwa na ccm kudhoofisha upinzani.

Maswali ya kujiuliza

1) Mbona hasumbuliwi kwa kuwekwa ndani na kufikishwa Mahakamani kama wengine?

2) Mbona hakerwi na mfumo mzima wa chaguzi zetu? Lini ulimsikia akihimiza mageuzi ndani ya sheria za uchaguzi hususani NEC?

3) Mbona hajawahi kuomba msamaha kwa kuwapotosha wapigakura alipowaahidi suala la kulinda kura ni lake aachiwe na baada ya kushindwa akadai aliibiwa?

4) Mbona hadi leo hajatoa majumuisho ya kura alizozipata hususani fomu za vituo na za majimbo kutuhakikishia ya kuwa alishinda kwa 62% kama alivyodai?

5) Mbona hadi leo hajaenda Mahakama kuu kuiomba kibali cha kuhesabu kura zote ili tujue mbichi ni zipi ?

6) Mbona hajalalama marekebisho ya sheria za mgao wa ruzuku zinazolenga kuusambaratisha UKAWA?

7) Mbona hadi leo kaufyata kupigania haki ya kikatiba ya upinzani kuendesha shughuli zao bila vikwazo na vitisho?

NIONAVYO

Lowassa ni CCM mole yuko huko kuwadhoofisha kwa kuwatupia changa la macho kwa kuboresha ruzuku ili wasahau mambo ya kimsingi kama NEC kututendea haki wapigakura.

Lowassa has too much to lose and too much baggage to carry to represent a lynchpin of change we are looking for....
JF itabaki kuwa juu
 
Back
Top Bottom