Slaa alisema nini? alichokifanya Slaa ni kuzira baada ya nafasi ya kugombea urais kupewa Lowassa. Hiyo tabia ya kuzira ya Slaa inaeleweka muda mrefu na hata wanaccm huwa mnamsifia kwa kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa kwani sasa hivi haikosoi serekali ya ccm. Sipingi mchango wa Slaa kwa cdm nauheshimu sana, lakini kilichomtoa cdm sio kufukuzwa bali ni nafasi ya urais kupewa Lowassa.
Ujio wa Nyalandu kwangu sioni jipya kwani kwangu yeye ni mwanaccm kama walivyo wanaccm wengi. Sio Nyalandu tu, hata akija Nape huku cdm bado siwezi kushangilia kwani najua kabisa ataondoka ccm kuja cdm sio kwa kuipenda bali sehemu ya kupoozea machungu yake lakini sio kupenda sera zake. Wangalau Nyalandu, ukiacha sifa mbaya ya ufujaji wa mali ya umma aliyonayo mbele ya jamii kama alivyo Magu, yeye anamejitoa muhanga kwa kuhama ccm huku akiacha wadhifa wake bila kufukuzwa na kutokuogopa vitisho vya mwenyekiti asiyetaka kupingwa wala kukosolewa. Yeye namsifu kwa kuchukua maamuzi magumu kwa wakati huu na mazingira yalivyo, huu nauona ni ushujaa na si msifu kwa kutaka kujiunga cdm.
Mpendwa siyo kweli kwamba Dr slaa alizira eti kwa sababu alikosa nafasi ya kugombea uraisi, bali alikataa kula matapishi yake. Au kwa msemo wa Mwl Nyerere alikataa kugeuka nyuma kwani angekuwa jiwe.
Kumbuka kwa miaka miingi Dr Slaa amekuwa akimtaja Lowasa kuwa ni fisadi papa, je kwa mtu mwenye kusimamia msimamo wake, ingekuwa sahihi kubadili kauli hiyo na kumnadi Lowasa kama clean man!!!
Si hivyo tu bali pia Kumbuka umaarufu wa cdm umetokana na kuwashambulia mafisadi mojawapo akiwa ni Lowasa, je Dr Slaa angekuwa na kauli ipi kuhusu swala zima la ufisadi katika mikutano ya kumnadi Lowasa?
Kubali kataa cdm ingepata umaarufu sana na ingeendelea kupata umaarufu kama ingewakataa kuwapokea watu wowote wanye makandokando kama Liwasa na Nyalandu.
Kumbuka cdm walivyokuwa wakimsema Nyalandu kuhusiana na ubadhilifu wa mali za umma ikiwa ni pamoja na kusafirisha Twiga hai. Leo hii cdm wanadiliki kusema ya kuwa kumpata Nyalandu wamelamba dume!! Je kwa wenye akili waitafasili vipi kauli hiyo!!
Huoni kama kwa sasa cdm ni kama inaunda kundi maarumu la mafisadi? Kuna kila sababu kwa cdm kujitafakali upya kuhusu watu wanaowapokea. Si ajabu kesho tukasikia wakimpokea kwa shangwe pro Maghembe, nyoka wa makengeza, Zitto mliyemwita msaliti nk
Hata Sumayi hakuwa mtu sahihi kupokelewa cdm. Na kama mngempa uanachama basi mngeepuka kumpa uongozi. Kumbukeni huyu mlimwita mr zero je hiyo akili ameipata wapi baada ya kuja cdm?
Cdm mnaonyeshe wazi kuwa hamsimamii mnachokiamini kuwa si sahihi. Bali mko tayari kuchukua hata mizoga ili mradi tu mwingie ikilu. Kumbukeni kila binadamu ana ubongo hivyo kila binadamu ana kumbukumbu.