Wakati huu mchakato wa wanachama wa CCM waliochukua fomu kuwania kuteuliwa kukiwakilisha chama katika kinyang'anyiro cha urais kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu 2015 wakizunguka mikoa mbali mbali kutafuta wadhamini, waziri mkuu aliyejiuzulu ambaye naye anawania kuteuliwa anaonekana kupewa upendeleo wa wazi kwenye vyombo vya habari kama televisheni, redio na magazeti.
Mimi binafsi sijaelewa kama upendeleo huu ni kutokana na mhusika mwenyewe kuwagharimia waandishi wa habari au ni vyombo vyenyewe ndio vinaonesha upendeleo huo au kuna asali imepitishwa ili jamaa apewe promo kubwa. Ukweli ukifuatilia taarifa za mizunguko ya watia nia wakitafuta wadhamini, Lowassa anapambwa sana na vyombo vya habari hasa TV kuliko wenzake.
Yaani wengine hata hawasikiki utadhani wamechukua fomu na kwenda nazo nyumbani. Mimi nashauri vyombo vya habari kutupa habari kwa haki na usawa kwa watia nia wote hasa kama taarifa zao zinagharimiwa na vyombo husika.
Lakini Kama ni watia nia wenyewe ndio wanaogharimia waandishi hapo sina neno kwani jamaa yule mpunga kwake sio tatizo na kila mwandishi angependa kuambatana naye maana wahenga walisema "Fuata asali ule nyuki"
Jamani hebu ifike mahali tuangalie ukweli na uhalisia uliopo mbona vyombo vya habari vinavyomkebehi lowassa kuutwa kila siku mbona hamsemi kwamba vinampendelea?
Kwa maajabu yanayotendeka katika mikusanyiko ya anapokua lowassa jamani hata kama Mimi mwandishi lazma ningechukua habari na kupiga picha maana inapendeza jinsi watanzania walivyokua na muamko wa mabadiliko jinsi watanzania sasa wameamua kumpa support mtu wanaeamini kua ndie atawapa Tanzania waliokua wanaitamani.
Haijawahi kutokea katika historia ya tanzania mafuriko ya watu katika wagombea wa ccm na wengine kwanini vyombo vya habari visikusanye habari hizo na kuweka historia?
Hyo dhana ya kwamba mtanzania hafanyi jambo jema bila pesa mmeitoa wapi mbona mnawadhalilisha watanzania mwenzenu kwa shutuma ambazo hata hazina ukweli
Mnawadhalilisha waandishi wa habari kua wana njaa wakati ni kazi yao kutoa habari pale inapobidi.
Kwani wagombea wengine habari zao hazitoki? U nadhani hawataki? Ni kwamba wamezidiwa na mafuriko wanaona aibu kwa majigambo yao sasa magazetini wakaonekana watu hata mia hawafiki kwao ni fedheha sio kwamba vyombo vya habari vinapendelea.
Lowassa watu wanamhitaji jamani acheni utani, acheni chuki tena bila kumung'unya maneno