Lowassa amtisha Rais Kikwete

Kuna nchi ya waswahili ambapo waziri mkuu alijiuzuru tena kwa kashfa na arudi kuwa rais wao. Itakuwa history ya waswahili ambao wanafikiria kwa tumbo
 

ivi ni nini kitatokea endapo lowasa atapita kuwa raisi wa Tanzania?baadhi ya watu si watapata strock?watazificha wapi nyuso zao...jiandaeni pia kwa pande zote kukosa au kupata
 
Mzee wangu nae anamtaka EL mimi kwa upande wangu ni mpaka niwasikie wagombea kwenye kampeni...
 
Membe kahangaika weee hadi alienda Misitu ya Amazoni kusaka waganga ili cc wampitishe sasa ngoja tuone kama uchawi wa membe utafanya kazi.

Dah... Uchaguzi wa mwaka huu lazima utakuwa wa historia katika nchi yetu.
 
Hebu tufikirie Baraza la Mawaziri la ENL

  1. Waziri Mkuu Prof Juma Kapuya
  2. Makamu wa Rais Amani Abeid karume Jnr
  3. Waziri wa Sheria na Katiba Andrew Chenge
  4. Waziri wa Nishati na Madini William Ngereja
  5. Waziri wa maliasili na Utalii Mgana Msindai
  6. Waziri Mawasiliano na Uchukuzi Peter Serukamba
  7. Waziri wa Jinsia na watoto Beatrice Shelukindo
  8. Bunge Sera na Uratibu Hamis Mgeja
  9. ......................

Hebu Watanzania tuwe serious kwa safu hii mnatagemea kitu chochote kipya?!

Be The Juror yourself
 
Mufindi mnaogopa nini akiwa Rais huyu ndg? Wacha propaganda nyeusi hapa....ni nani zaidi ya Edward Lowassa ndani ya CCM yetu? hebu tuwe wakweli tuweke mipango binafsi kando
CCM yenu na nani hiyo ambayo mnampenda Lowassa?
 

Ni shiiida.
 
Ndo atapitishwa na itakula kwenu.
Sasa siasa imehama kutoka CCM vs Upinzani imekuwa CCM VS LOWASA VS UPINZANI
 
IQ ya Lowasa iko juu sana , atafanya kazi ktk muda wake atazuia na kuchukua hatua kali kwa ufisadi na wizi ambao utatokea ktk muda wake, kamwe hawezi kufanya kazi ktk vipindi vya watangulizi wake.
Eti itatokea fisi naye apewe Bucha kulinda?
 
Ndo atapitishwa na itakula kwenu.
Sasa siasa imehama kutoka CCM vs Upinzani imekuwa CCM VS LOWASA VS UPINZANI
Hakuna sababu ya kuhangaika na wapinzani kwa sasa wale ni weupe sana dawa yao ndogo, ni CCM kuja na mgombea anayeuzika siyo Lowassa ambaye upinzani wanaomba CCM wafanye makosa ili kwao iwe rahisi wakati wa kampeni
 
Rostam ambaye amehamishia sehemu kubwa za biashara zake nchini Kenya na Dubai.

Mtu kama huyu ndiye anae taka kuwaamlia watanzania hatima yao,kama hata wanyonga kabisa lakini kitakapo nuka atawaacha watanzania wanachinjana,mwenyewe huyooo kaishia zake
 
Mmeanza kujistukia wakati DJ anajiandaa kutuwekea mziki wa bakurutu baada ya kuona bongo fleva watu hawachezi. Viva Lowassa
 
Kama EL atashinda na kuwasweka ndani waliotumia madaraka yao vibaya itakuwa SAFIII sana.
Majizi yote mliyoiba katika utawala huu wa JK including wanafamilia yake mnajulikana, jiandeni kulala nyuma ya nondo.
 
Lowasa hatumpi.na wakimpa nahamia CHADEMA
 
Well said mkuu, mimi sijui kinacho watisha ni nini hasa? Maanake stori nzima imejaa woga tu na inaonekana wazi wazi imetungwa tu!!!!!

Wengi wanaompinga Lowasa wanajijua kwamba uadilifu wao ni wa kutiliwa mashaka na wanajua "Mwanaume" akiingia pale ni lazima waikimbie nchi.
 
Nashangaa watu wanajadili nini,hivi kwani ni Lowassa Peke yake Ndo Kaachiwa?mbona wengine hawasemwi?au hawakufungiwa na kuachiwa?Jamani tusitake kuweka habari tuu na kuiona CC Haina uwezo.Angeachiwa peke yake na wengine Kutoachiwa hapo naona ndo ingekuwa habari!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…