Hakuna haja ya chuki, vijembe na siasa za maji taka ndani ya chama kimoja. Nadhani ikiwa hivi itafaa sana. Uwepo mkakati wa pamoja. Mafahari wawili wawekwe katika zizi moja kisha muafaka ndio njia rahisi ya kupata maridhiano. LOWASA akiwa rais, basi SITTA awe waziri mkuu.
SITTA akiwa rais, LOWASA nae awe waziri mkuu. Nadhani mambo yatakuwa bambam. Dalili zinaonyesha kuwa wazee hawa wameanza kuchukua jaramba taratibu kwa ajili ya kupokea kijiti. Kama ni kweli.
Basi nawatakia mbio njema.
Ama kweli ukustaajabu ya Mussa utaona ya Firauni. Kwani CCM mmeishiwa na watu wa maana hadi mkalambe matapishi? Kwani kilichomuondoa EL madarakani hamkumbuki? kwani alisingiziwa? Mnafikiri atabadilika nini? kwa nini mnapenda kujuta maisha yenu yote? Ama kweli mmetawaliwa na Freemason!Shetani arudi madarakani, mtauzwa na kuchinjwa hadi nyinyi wenyewe, waume na wake zenu na watoto. Mtajuta. Tabia haina dawa. Hebu kumbukeni wizara zote alizoshika alifanya nini cha kuwasaidia watanzania. Ama ni hilo la shule za kata? huo ni uharibifu namba moja! Tatizo ni akili ndogo kuongoza akili kubwa!!!! Lowasa hana akili ya kuwaongoza wasomi, hana 'capacity hiyo'. Anatumia mabavu kuliko akili.Kwanza hajaturejeshea fedha na mali alizotuibia watanzania kama alivyoaagizwa na T.B. Joshua.
Tatizo la Sitta ni unafiki na ukigeugeu. CCM tafuteni sura mpya yenye akili, kama mmeishiwa achieni ngazi. Tumechoka na sura za zamani ambazo hazitusaidii, tunataka sura mpya ambazo zitatusaidia na kuiweka Tanzania katika sura ya ulimwengu kwa mafanikio, sio kwa maovu, ujinga na mauaji kama ilivyo sasa hivi. Aliyeanzisha ujinga huu, kama ametumwa ASHINDWE KATIKA JINA LA YESU KRISTO ALIYE HAI.
just tell your paymaster that all he has to do is this, he should try harder to stay alive b4 2015