Lowassa akimbia Mdahalo wa Wagombea Urais

Lowassa akimbia Mdahalo wa Wagombea Urais

Kwanza nianze kwa kusema kusema Lowassa sio kweli kwamba hawezi kuzuia mafuriko yake kwa mkono,ukitizama watu waliomsindikiza kuchukua fomu utagundua lowassa anao uwezo wa kuyatengeneza na pia kuyazuia mafuriko yake kwa mkono kama alivyoyazuia leo akichukua fomu.

Tuyaache hayo ya lowassa na mafuriko yake ya kutengeneza.

Naomba kuwauliza wapambe wa lowassa,mnazijua sababu za lowassa kuukacha mdahalo kuhusu uchumi uliondaliwa kwa watangaza nia wote? Nasikia sitta,membe,January na hata sumae wamethibitisha kushiriki mdahalo huo ulioandaliwa na kina Ali mfuruki.Lowassa anaogopa nini kutuambia mipango yake ya uchumi na kutupa nafasi ya kumpima kwa maswali mazuri yatakayompa nafasi ya kujifaragua kinagaubaga kwenye eneo Hilo la kiuchumi.Tunahitaji ufafanuzi zaidi kutoka kambi ya lowassa naona mmekua kimya kwenye hili la mdahalo
 
Mzimu wa Richmond huo bado unamsakama.
Maana wapo ambao watauliza juu ya ilo
 
Hana uwezo wa kujibu wa maswali kama ya Richmond.
 
1. Muda wa mdahalo bado, wananchi hawawezi kuchagua mgombea wa CCM, kwa sasa ni wana CCM wenyewe ndio wanaotakiwa kufanya mdahalo sio watu baki kama Mufuruki. Mdahalo wa public unatakiwa uwe baada ya vyama vyote kupitisha wagombea wao. Mdahalo wa Mufuruki sio lazima, Lowassa ana haki ya kutokukubali kwenda bila kujieleza chochote kile.
2. Wagombea wengine kama wassira, ngeleja, makongoro...mbona hawajaalikwa na wala haisemwi majibu yao yalikuwa ni nini ila Mufuruki anatweet majibu ya Lowassa tu kuwa amekataa? Kunani hapo? Mufuruki bado ana super-dealership ya Airtel? Lowassa bado ana super-dealership ya voda?
 
mkuu kama ni kweli ni kosa kubwa sana. by the way mdahalo huo unafanyika lini na wapi?
 
You're such a dumb dude I never heard before! Mdahalo ni njia mojawapo ya kufikia wapiga kura wengi bure bila kulipia muda ktk television, kwa kunadi sera na kujitofautisha na wagombea wengine. Wewe kwa akili yako finyu unaona sio level yake? What level is Lowasa? Make watanzania hatuchaguI KINGS bali Raisi. We need someone like us not above us! Nakushauri kufikiria kwanza kabla ya kuweka utumbo hapa!
 
Watu wanamlaumu Lowassa bure. Lowassa hajakimbia mjadala, kilichotokea ni akina Ali Mfuruki kumikimbiza Lowassa katika mjadala. Waandaji wanaposema watazungumzia uchumi bila kumhusisha mtu tayari watakuwa wanamzungumzia mtu.

Hivi utaongeleaje uchumi bila kugusa maeneo muhimu kama nishati? Ukigusa nishati utakuwa umemgusa umeme kama nishati ya awali tuliyo nayo. Hapo utakuwa unazungumzia Tanesco na kisha kumkaribisha 'mchepuko' Richmond

Ukitaja Richmond, majina ya kwanza kutokea ni Lowassa. Kwa mwendo, mfuruki atatuambiaje hawajamkimbiza mzee!
 
Kifikra yuko sawa kabisa ila tukiwa wepesi wa kuvutwa na hisia basi utaona amekosea.

Uchumi unakuwa kwenye ilani ya CCM sasa yeye CEOrt/Ali Mufuruki wanaijua sera ya uchumi wa CCM ya mwaka 2015/20?

Huyo mzee kakurupuka tu.

Mdahalo ungekuwa mzuri kwa taasisi kama yao wangesubiri kwanza vyama vyote vitoe ilani zao za uchaguzi.

Waangalie ilani ipi ina sera zenye maslahi yanawiana na mitazamo yao halafu ndiyi wawaite wagombea wa vyama husika waweke huo mdahalo.

Kukurupuka unafikiri ndiko unakowaza. The concept aimed at revealing what was behind the political curtain
 
Sioni umuhimu wa kuandaa mdahalo wakati ndio kwanza watu wanaanza kuchukua form. Wangesubiri hadi idadi kamili imejulikana ndo wafane hiyo kitu wote wawekwe kwenye podium kwa pamoja. Tukifuata hiyo system aliyoisema Ali Mufuruki kuwa wiki ijayo waanze watano alafu wiki nyingine waongezeke kuna watakaopiga chabo.
Tumia akili! Mdahalo sio interview maswali yakaya yaleyale
 
EL anaonyesha ujanja ujanja tu. Sijawahi kumuona akiongea kitu cha msingi na maendeleo katika taifa hili zaidi ya kumfukuza mtendaji wa kata. Tunataka tuwaone.
 
Akutanishwe na viongozi wa kimila wa kabila la Masai labda ataweza kudibet
 
yale yale ya 2005 na 2010, tukumbushane hapo kwanza, JK alishiriki mdahalo wowote miaka tajwa?
 
huyu mgombea urais nae.kweli mwaka huu ukawa njia nyeupe
 
Back
Top Bottom