LONDON: Kibelloh & Disturbing News!

Ina maana kwa kuwa, tuseme, mathalani, hakuiba alipokuwa Utalii au Foreign Affairs, ndiyo kusema kwamba HAIWEZEKANI akaiba sasa??
 
Hawezi kuacha mapesa yote ya utalii, akaja kuiba picha tena at the time ambayo anajua kuwa kila mtu anamuangalia baada ya misuko suko yote aliyoipata mwaka huu, na jana hawezi akatuhubutu kuiba picha, wala hela za geti, sio kweli!
 
taarifa za karibu ni kwamba huyu mzee ni kiburi sana na hasa ukiongezea backing ya VDG.Hajui hata kuishi na watu wa chini yake . Alimfukuza ndug Ally lakini unamtetea kivipi na wewe hukai wala kufanya kazi kwenye ubalozi wa UK? Unategemea kupewa habari ama na Kibelloh ama wapenzi wa Kibelloh pekee na huwezi kusikia from the other side . Jiulize kuna mabalozi wangapi huko Nje why Kibelloh all the time nawe unamsimamia?

Sikilizeni sasa . Once kabla ta Makamu wa rais wa sasa hajaulamba ukuu alikuwa anasoma UK na alikaa nyubani kwa Mzee ally .Mzee hakuwa mwajiriwa wa Ubalozi bali ni mtaalam wa mahesabu kwamba kila Ubalozi walipo vurunda walimwita awape msaada .Imekuwa hivyo na alikuwa ni part timer Old man .Sasa neno kufukuzwa labda ni kubwa mno bali alikataliwa baada ya Makaku wa rais kuwa UK akamuona na kumchangamkia . Kibelloh ni mpuuzi fulani hivi mwenye wivu na umimi pia . Ndiy product za CCM hizo alidhani anajulikana yeye tu.

Sasa nadhani watetezi wa Kibelloh mtatia akili how huyu mzee alikataliwa kazi ya part time pale Ubalozini na Kibelloh .Sasa Makamu wa rais kwa hali ulitaka afanyeje ? Mtu ni kibarua na anaomba na wao baada ya kuvuruga na alimkataa kwa kuwa tu sasa alijua siri zake za wizi zingalikuwa nje mapema . Kibelloh ni mwizi na mapicha anayo si ya ofisni bali ya nyumbani .
 
Wooow! Kibelloh ana matatizo mangi juu ya ku-deal na wananchi on personal level, na hasa wananchi mlioko nje na kwa sababu mbali mbali ambazo ni nusu ni makosa ya wananchi na nusu yake ni makosa yake, hilo simtetei isipokuwa hayaingilkiani na kazi yake tuliyomtuma yaani taifa,

maana hata kabla hajaondoka London, ndio kwanza amewashawizshi wazungu huko London kuupatia mkoa mmoja bongo vifaa vya shule vyenye thamnani ya karibu paundi 40,000, kwa nini asiviibe vifaa hivyo? Nani bongo angejua kuwa alipewa?

Je afukuzwe kazi kwa sababu ana wivu fulani? kuhusu huyo Ally, mimi simfahamu lakini kwa maneno yako mwenyewe ninayaona majibu, kwanza ubalozi wetu nje hauruhusiwi kuajiri mtanzania aliyoko nje kuwa accountant, maa-accountant hutoka bongo kama maofisa, kwa hiyo kumuajiri part time ilikuwa pia ni makosa, hata kama ni ndgu ya makamu wa rais,

picha tumesikia mara za ofisini na sasa tena ni za nyumbani, hebu nyie watu wa London please make up your mind ameiba picha za ofisini au nyumbani?
 
hutafanikiwa kuupinda ukweli kisa unamoenda Kibelloh na sasa naamini kila mmoja amesha jua kwamba unatetea maslahi yako na si Tanzania . Nasema kwa sauti kubwa Ally was a part timer na ni kawaida .Kama mmleta ma Accountant vilaza kwa nini Kibelloh asitafute msaada.Watu wapo na Kibelloh kamuulize anavyo mjua Ally na utaalam wake acha kubabaisha watu kwa maneno .

Kibelloh kaiba picha za ndani .Yaani wall paintings toka nyumbani kwa Balozi na si picha za ofisini .Kwa hiyo wizi wa matumizi ya gate , picha za ndani.
 
Mzee TT,

Ninakuomba kukubali kutokubaliana, maana kuuliza maswali ni kutafuta masilahi toka kwa Kibelloh?, Kibelloh ana masilahi gani ya kunipatia mimi huku kunyumba?

isipokuwa huko London punguzeni majungu!
 
Nadhani kuna hypothesis 2 hapa:

Aidha Kibelloh anachukiwa bila sababu (kwa sababu ALMOST kila kona analaumiwa) au malalamiko dhidi yake ni sahihi.Kuhusu majungu,nadhani si London pekee bali huo ni kama utamaduni wetu watanzania,na majungu hutokana na moja kati ya haya:

A.Mtu asiestahili kupata au kuwa na alichonacho kuendelea kupata/kuwa nacho
B.Kuonewa kijicho kwa hicho anachopata japo ni haki yake.

Putting that in perspective,

AIDHA
---Kibelloh anapigwa majungu kwa vile watu wanamwonea wivu
---Kibelloh anapigwa majungu kwa sababu hafai.

Naamini mjadala huu utafikia tamati tu pale wenye tuhuma hizo watapozithibitisha beyond any reasonable doubt
 
Mbona hujasema kama labda kuna ukweli kama huu wa Msabaha na Richmond lakini kwa kuwa ni mshikaji wa Rais anahamishwa wizara ?

Umesha sikia Kibelloh damu damu na JK na wengineo sasa leo kama pana ukweli na ukafumbiwa macho na watu wakaendelea kupiga kelele juu ya ukweli huo utasemaje?

Unataka ushahidi ama vipi? Yaani uletewe ushahidi hapa wakati watu wamesema kila kitu na kutaja hata majina ya wahusika kwa nini RO na JK na kundim lake wasifuatilie ndiyo wenye mamlaka ya kumpekua na kuujua zaidi? Unataka documents ana invoices ziletwe hapa ndiyo uamini? Tutaanza kukuomba na wewe ushahidi sasa katika kila post yako.
 
Hawa wenzetu walioko London, akina TT, wanaonekana wana habari za karibu kiwakati na kigeographia kuhusu Kibelloh nami kwa asilimia kubwa ninatend kuwaamini bali kuna mambo machache katika misemo yao bado inahitaji ufafanuzi.

Wanasema Kibelloh ni swahib wa JK kwa upande mmoja, na papo hapo RO na Radhia nao ni maswahib wa JK kwa upande mwengine. Papo hapo wanabodi waliokuwa wanamtetea Kibelloh walituambia kuwa Radhia na RO ni maadui wakubwa wa Kibelloh. Mkorogo huu haumake sense.

Pili hatuelezwi ni wakati gani ambapo mhasibu Ally (swahib wa VP) alitiliwa ngumu kibarua cha muda ubalozini - ni baada ya kufanya kibarua hicho chini ya Kibelloh na kuachishwa baada ya Kibelloh kujuwa usawhib wake na VP au aliwekewa ngumu mara tu Kibelloh alipofika?
 
Ninasema moja la wizi na kusimamishwa kwa Mzee Ally. Baada ya VP kufanya Ziara UK na wakati anakutana na watu ama staff wa Ubalozi Ally alikuwepo ndipo akawa singled out kwamba alah Ally na wewe upo hapa? Habari za siku nyingi na mbele ya Kibelloh ndiyo ikaanzia hapo.

Huu ni ukweli na Kibelloh kum ditch Juma Ally was not hard at all maana alikuwa part time kuwasaidia vitabu. Fanya uchinguzi utaona anaombwa tena baada ya balozi mpya maana Mzee anayajua mambo kuliko waajirwa wa Serikali yetu. Naishia hapa na msimamo wa wizi wa Kibelloh na Ally kufutwa kibarua.
 
Back
Top Bottom