Lawkeys
JF-Expert Member
- Nov 16, 2009
- 1,118
- 287
Kuna wachungaji wa mshahara wanapotosha watu kuhusu mitishamba!!
Mtaani kwetu
Leo asubuhi nimemsikia mchungaji mmoja wa kanisa flani akikashifu dawa ya Loliondo, alikuwa akitoa muongozo wa maandiko kwa mpangaji wake, amesema;
"Miti yote ina pepo, na watu wote wana mapepo ambayo yanawaongoza kutumia miti na matunda kama dawa badala ya kutumia kama chakula."
Akaendelea kusema,
"Mapepo yalio ndani ya watu ndio yalio waongoza watu 6000 kwenda kunywa dawa Loliondo."
Mpangaji akanywea. Inawezekana wanazuoni hamtapata nafasi ya kupitia aya, hivyo ili kurahisisha mambo nitatupa mbili.
1. Ezekiel 47:12- Na karibu na mto, juu ya ukingo wake, upande huu na upande huu, utamea kila mti wa chakula, ambao majani yake hayatanyauka, wala matunda yake hayatatindika kamwe; ...matunda yake yatakuw ni chakula na majani yake yatakuwa ni dawa.
2. Ufunuo 22:2- katika njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao, matunda aina kumi na mbili,wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni kuwaponya mataifa.
Wazungu watu wabaya sana, wametufanya tuamini kwamba kila kitu chetu ni uupuzi. Jamani hata dawa kutika katika majani? Bila hata uthibitisho unasema DECI wakina kakobe muogopeni Mungu.
Ili mradi hakuna ibada ya mizimu, kupiga ramli, na uchawi, mitishamba inakubalika katika maandiko.
Mtaani kwetu
Leo asubuhi nimemsikia mchungaji mmoja wa kanisa flani akikashifu dawa ya Loliondo, alikuwa akitoa muongozo wa maandiko kwa mpangaji wake, amesema;
"Miti yote ina pepo, na watu wote wana mapepo ambayo yanawaongoza kutumia miti na matunda kama dawa badala ya kutumia kama chakula."
Akaendelea kusema,
"Mapepo yalio ndani ya watu ndio yalio waongoza watu 6000 kwenda kunywa dawa Loliondo."
Mpangaji akanywea. Inawezekana wanazuoni hamtapata nafasi ya kupitia aya, hivyo ili kurahisisha mambo nitatupa mbili.
1. Ezekiel 47:12- Na karibu na mto, juu ya ukingo wake, upande huu na upande huu, utamea kila mti wa chakula, ambao majani yake hayatanyauka, wala matunda yake hayatatindika kamwe; ...matunda yake yatakuw ni chakula na majani yake yatakuwa ni dawa.
2. Ufunuo 22:2- katika njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao, matunda aina kumi na mbili,wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni kuwaponya mataifa.
Wazungu watu wabaya sana, wametufanya tuamini kwamba kila kitu chetu ni uupuzi. Jamani hata dawa kutika katika majani? Bila hata uthibitisho unasema DECI wakina kakobe muogopeni Mungu.
Ili mradi hakuna ibada ya mizimu, kupiga ramli, na uchawi, mitishamba inakubalika katika maandiko.