Mimi huwa ninajiuliza, hivi CCM wanapoitisha mikutano kama hiyo wanawaambia nini wananchi? Maana tangu watuahidi maisha bora kwa kila mtanzania mwaka 2005, hali yetu ya maisha imekuwa mbaya kuliko ya awali, sasa wakija kwa wananchi wanasema nini?
Wanawapa sababu za maisha kuwa magumu zaidi, wanawaambia wavumilie hali inarekebishwa au wanawaambia CHADEMA wamekwamisha utekelezaji wa sera za CCM? Na wananchi tuna nini cha kutufanya tuwaamini hawa watu ambao ndiyo chanzo cha umaskini wetu?
Hivi huu mkutano ni kuhusu Chadema? Aaargh nani kanambia niangalie leo TBCCM
kwa maana hizi pg 12 kwenye uzi huu mnasifiwa sana eeh! kweli akili ndogo...................................Kama unataka habari za mkutano wa chadema nenda kwenye thread yake. Ipo kule ina comments nane tu tangu mchana.
Nafikiri kususa hakukutokana na mikutano ya live, bali kulitokana na kutangaza matukio kinyumenyume. Na issue ilikuwa ni kuuawa kwa Mwangosi ambapo TBC walishadadia kifo kile huku wakikielezea CHADEMA kama chama cha vurugu ilihali ushahidi ulikuwa wazi. Ndiyo tangu pale CHADEMA wakatangaza mgogoro na TBC. Lakini nakubaliana na wewe pia kwamba badala ya CHADEMA kutangaza mgogoro na kuwasusia ambako wamewapa advantage, wangechukua hatua dhidi ya chombo hiki cha umma. Kwa kuwasusia ni kwamba wamekubali kodi zao ziliwe na TBC kwa kazi ya kukibeba CCM.Lakini badala ya kususa na kutangaza live kuwa hawataki huduma yake wangeacha jamii ione kama wanaonewa na ihukumu yenyewe. Waliposusa wameharibu kwa sababu sehemu kubwa ya jamii ilikuwa haijaona kama chadema inaonewa.
Swali la kitoto na kama siyo la kitoto basi bado unaishi katika dunia ya zama za mawe.Mi si mshabiki sana wa siasa, ila mkuu UNATISHA:
Umejiunga JF APRI 8 (SIKU 13 ZILIZOPITA) hadi leo una post 732( WASTANI WA POST 56 KILA SIKU) zaid hata ya watu waliojiunga mwaka mmoja uliopita. Mkuu nijibu mawali yangu mawili tu
1. HUNA KAZI YA KUFANYA HAPA MJINI ZAIDI YA KUSHINDA JF NA KUPOST SIKU NZIMA?
2. UNALIPWA KWA KILA POST UNATUPIA JAMVINI?
3.JF MODS WAMEKOSEA IDADI YA POST ZAKO?
KWA KWELI NIMESHANGAZWA SANA WANA JF
Itakuwa ngumu sana kwao kuongelea ya CCM kwa kuwa hawana lililo positive. Mengi ya mambo waliyonayo yana mwonekano hasi mbele ya jamii, kwahiyo wanaamua kujikita kwenye kuwasakama wapinzani wao ili watu waone CCM ina unafuu kuliko wapinzani.Yani inaleta ukakasi,mkutano mkubwa kama huu..badala ya kuongelea utekelezaji wa sera za chama,matatizo na suluhu zake,yani wao kila sentensi ni chadema,chadema,chadema...
Viongozi wao wamekaa muda mrefu madarakani lakini watu wakitaka kuwaondoa kwa demokrasia wao wanasema ni ccm