LIVE UPDATES: Mkutano wa CCM Morogoro

LIVE UPDATES: Mkutano wa CCM Morogoro

Mleta wataje na ye ameanza kuponda serikali ya sasa.
Kuna thread imeletwa hapa analalamika "Wanatumiwa tu " na hawanufaiki na
chochote.. ahadi waliahidiwa ni debe tupu ....

Aache kukufuru... Bila Serikali ya CCM yeye na Madansa wake wasingeijua USA ikoje; Lazima awachezee kokote wamempeleka sehemu asingezikanyaga yeye na Madansa wake... na kukaa hoteli swafi bila bughudha ya chakula; Malipo
 
kinana alitoa ushauri kwa chadema kuwa peoples power ni kwenye sanduku la kura, barabarani ni askari
 
Sasa nani masikini?
Anyway haina haja ya kubishana na msukule.
By the way... nakuja Arusha tukutane unikatie kitu kidogo basi au sio TAJIRI

unambiwa wale ndugu zako ni maskini sio wewe mlamba viatu vya ccm
 
"people's
power aka nguvu ya umma
inapatikana kwenye masanduku ya kura,
ninawaomba wananchi mjihadhari na Chadema
kwa kuwa viongozi wake ni wabinafsi, wenye
uchu wa madaraka na siku zote ndoto zao ni kuingia ikulu"


Katibu Mkuu wa CCM Bara, Ndugu Abdulrahman Kinana. Jumapili 21/04/2013 Morogoro.
 
Sio kweli, amezungumzia matatizo ya wakulima wa miwa kiwanda cha kilombero na mtibwa, migogoro ya wakulima na wafugaji, miundombinu ya barabara inayojengwa mkoani morogoro kuunganisha na mikoa mingine, katiba mpya na amani ya nchi...mwishoni kabisa ndio amezungmzia chadema..sala haiwezi kukamilika bila kumlaani shetani

Sema sala haiwezi kukamilika bila kumtaja muumba na anaetupa kuishi....Shetani ni kwa freemasons!
 
1._KINANA_AKIHUTUBIA_GAIRO_JIONI_HII_71472.jpg
 
Mimi huwa ninajiuliza, hivi CCM wanapoitisha mikutano kama hiyo wanawaambia nini wananchi? Maana tangu watuahidi maisha bora kwa kila mtanzania mwaka 2005, hali yetu ya maisha imekuwa mbaya kuliko ya awali, sasa wakija kwa wananchi wanasema nini?

Wanawapa sababu za maisha kuwa magumu zaidi, wanawaambia wavumilie hali inarekebishwa au wanawaambia CHADEMA wamekwamisha utekelezaji wa sera za CCM? Na wananchi tuna nini cha kutufanya tuwaamini hawa watu ambao ndiyo chanzo cha umaskini wetu?

Wakuu NENO CHADEMA lilitajwa mara 43!!! kwwenye hutuba za viongozi wa CCM jana Morogoro kwenye mkutano wao. CHADEMA ilifananishwa na Dr Savimbi. Vijana wengi waliokuwepo mkutanoni hawamjui tena Savimbi ni nani!!
 
Kwani chadema wanapowaita watu mkutanoni wanawaambia nn,hawajawahi kufanya lolote bota ya hao unaowapuuza sasa kaka acha kibeza kama shukrani huwezi kutoa kwa hayo basi hata kwenu ni vigumu kutoa kwa wazazi waliokizaa.
 
Nani asiyewahi kusoma historia labda wewe humjui savimbi kaka usitusemee!!
 
[h=3]KINANA AISHUKIA CHADEMA LEO MJINI MOROGORO[/h]*Asema viongozi wake wamekubuhu wa ubinafsi
*Wanajali maslahi binafsi ya Chama chao badala ya Watanzania
*Awataka Watanzania kuwapuuza


[TABLE="class: tr-caption-container, width: 605"]
[TR]
[TD="align: center"] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption, align: center"]Kinana akihutubia mjini Morogoro leo.Picha: Bashir Nkoromo[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
NA BASHIR NKOROMO, MOROGORO
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana ameisasambua Chadema na kusema ni chama ambacho daima kimekuwa kikiweka mbele maslahi yake binafsi kuliko ya Watanzania.

Amesema viongozi wa chama hicho wamekubuhu kwa udikteta kiasi cha kujiona wao ndio wanajua kila jambo kuliko watu wengine hata mwenzao wa chama cha upinzani ikitokea ana mawazo au msimamo wasioutaka au ameipongeza serikali kwao huonekana ni msaliti na kibaraka wa CCM.

Akihutubia leo mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika jana mjini hapa,Kinana, alisema kuwa Chadema ni balaa kwa nchi naa watu kwani viongozi wake wamekuwa ni watu wa kuhubiri machafuko badala ya mshikamano uliozoeleka Tanzania.

Alisema kutokana na umangimeza wao sasa Chadema kimeanza kuigawa nchi kwa kutumia sera ya ukanda licha ya kwamba sera hiyoi ni kinyume cha katiba ya nchi na watu wake.

"Ninapenda leo niwaelezeni ndugu Watanzania Chadema ilivyojawa na ubinafsi, wamekuwa wakiwakukusanya Watanzania na kuwagawa kwa sera yao ya majimbo. hili si mara ya kwanza maana katika kipindi cha siku za hivi karubuni walitangaza wazi kuigawa nchi kwa kutaka
kujitenga kanda ya Kaskazini eti ili iwe chini ya utawala wao", alisema Kinana.

Kinana alisema CCM kama chama kilichoingia mkataba na Watanzania haiwezi katu kukaa kimya na kuona hali hii ikitokea, kila mara tumekuwa tukihubiri amani na mshakamano lakini Chadema hili limewashinda jambo ambalo alisema ni dalili kwamba viongozi wa Chadema wameingia katika siasa kwa malengo yao binafsi.

"CCM itaendelea kusema ukweli kwa kila jambo na wala haitaficha hata likiwa siyo la kufurahisha wanachama wake ili mradi ni la kweli, tofauti na hawa Chadema, lazima Watanzania muwe makini nao kutokana na aina ya siasa na matendo yao wanayojinasibvu nayo" alisema Kinana.

Vurugu za Chadema
Kinana alisema kuwa Chadema wamekuwa ni watu wa maajabu na vurugu kubwa nchini, na katika hilo alitoa mfano ya mambo ambayo wanayafanya bungeni.


"Chadema kazi yao ni vurugu tu, utadhani wao ndio wamekuwa kambi ya upinzani wa kwanza bungeni katika nchi hii. Walikuwepo wapinzani kabla yao lakini kama CUF na Kina Mrema (Augustine Mrema) enzi za NCCR Mageuzi lakini hamkupara kushuhudia vituko kama

hawa Chadema ambao wanajiona wao ndio kila kitu. Wanatoa vitisho kila siku kwa Serikali hata kumtukana mkuu wa Nchi bila kujali kwamba ni kiongozi ambaye amefika pele kwa kuchaguliwa na idadi kubwa ya Watanzania", alisema.

"Wanabeza wapinzani wengine , wakiona mpinzani anapongeza kazi iliyofanywa na CCM wanaanza kumshambulia.Hakuna anayejua zadi ya Chadema .Wanamtukana Rais, wanaushambulia usalama wa Taifa, wanashambulia vyombo vya usalama,"alisema Kinana

"Hawa jamaa ni watu wa ajabu sana, kila kitu wanajua wao wengine hawajui.Wakigombana katika chama chao utasikia kuna mkono wa CCM. Sijui ni watu wa aina gani , wanafanya mambo ya ajabu sana kiasi cha kushangaza,"alisema.

Kinana alitoa ushauri kwa Chadema kuwa na uwezo wa kutafuta ufumbuzi wa matatizo yao kuliko kutumia muda wao mwingi kila jambo ambalo linakwenda kombo kunyoosha vidole kwa CCM.

"CCM tuna changamoto zetu nyingi, lakini tunatatua matatizo yetu wenyewe hatupotayari.Tuna makundi ndani ya chama lakini hayo ndio mambo ya siasa,"alisisitiza.

Mchakato wa Katiba mpya
Kinana alisema pamoja na kazi nzuri ambayo imefanywa katika mchakato wa Katiba mpya, kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni ametoa hotuba yake ambayo inaonesha wazi hakuna ambacho kimefanyika katika mchakato huo.

Alisema kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani Freeman Mbowe akiwa bunge ametumia muda wake mwingi kuzungumzia mchakato wa katiba mpya na kubwa katika hotuba yake kuwa haufai.

"Simsingizii kiongozi wa Kambi ya upinzani bungeni, ndani ya hotuba yake ameeleza wazi kuwa waliopewa dhamana ya kukusanya maoni ya Katiba mpya hawana ujuzi.Hii si kweli, waliopewa dhamana hiyo ni watu ambao wanaifanya kazi hiyo kwa uadilifu,"alisema.

Alisema Chadema ni watu binafsi ambao wao wametawaliwa na uroho mkubwa na wao kazi ni kuangalia maslahi zaidi na ni si maslahi ya nchi.

Ziara yake Morogoro
Kinana alisema kuwa ziara yake amejifunza mamb mengi lakini kubwa na msingi ambalo lipo kwa chama hicho kitahakikisha kinatafuta ufumbuzi wa matatizo ya wananchi na hasa migogoro ya ardhi, mipaka na huduma za jamii ambazo nazo ni changamoto kubwa kwa maeneo mbalimbali.

"Ziara yangu na viongozi wengine wa chama chetu ambayo tuimefanya katika wilaya zote za Morogoro tumeona changamoto nyingi.Tumetafuta ufumbuzi wa matatizo lakini mengine yanapatiwa ufumbuzi baada ya kukaa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa chama na kisha kutoa maagizo kwa Serikali kutekeleza,"alisema.

Agizo kwa wabunge CCM
Katibu Mkuu huyo wa CCM, alitumia nafasi hiyo kwa kuwataka wabunge wa CCM kutembea kifua mbele kwani chama chao kinafanya kazi kubwa lakini aliwataka wawe makini na Chadema na kuwataka kutowasikiliza kwani sasa imetosha.

Alisema Chadema wamekuwa wakisikiliza muda mrefu ndani ya Bunge na kuna wakati wabunge wa CCM walichukia baada ya Rais Jakaya Kikwete kukubali kukutana nao kujadili mchakato wa Katiba Mpya.
 
mkuu katika hili napingana na wewe kinana ni noma speech yake ni kali na ameumbua mambo mengi sana tuache uongo jamaa kaongea mambo ya msingi.
NI kwamba ulitegemea ataogea cha maana au uliskia vya maaana?Mi nilisikia vyote akiongea kimbea, na hakuna aliposhawishii ahta mwana CCM aliyekuwa nyuma yake hata aonyeshe kuridhia au hata kuchanganka kwa kumiskia kinana, sasa hata waliohudhuria wangevutiwa na nini? mzee alishaanza ulusinde alipoanza wapasha kuwa gwanada kitu gani, hata yeye alishavaa zamani na hata kama tunataka picture atazioyesha.Huu ni umbea tuu na mipasho hakuna kitu kwa mwanamumea, tena kiongezi wa lichama zee. Nahdani wewe ndio wale watu wa kusikiliza radio tanzania wakitangaza mechiya simba na yanga na kukuambi ni bonge la mechi, na ujinga miwngine.Wewe ndio unaamini usanii wa CCM.Kweli CCM wanamaliazana kw apropaanda zao za ujinga zaidi ya upinzani.Mbaya hata mibunge inayoona na kusikia huwa akili yao huwatuma kuamini uongo walioutunga wenyewe.
 
Back
Top Bottom