Leo Kinana kadhihirisha kuwa CDM ni koboko ya ccm, kuhutubia wananchi kwa kuisema mwanzo mwisho ni dhahiri kuwa kinamnyima usingizi, kama sivyo alipaswa kuja jukwaani na hoja mbadala za wapinza mfano;-
- Mikataba ni bora ya uchimbaji dhahabu hakuna shida kwasababu kadha wa kadha.
- Mikataba ya ujenzi wa bandari bagamoyo ni kwa maslahi ya nchi kwasababu kadha wa kadha.
- Mikataba ya uchimbaji mafuta na gesi ni kwa maslahi ya taifa kwasababu kadha wa kadha.
- Kuhusika kwa serikali katika utekaji si kweli kwasababu kadha wa kadha, nk.
Akifanya hivyo atakuwa ametuziba mdomo wale wote tuliowaka nyongo kwaajili ya uvunaji hovyo wa rasilimali na usimamizi mbovu wa serikali.