LIVE UPDATES: Mkutano wa CCM Morogoro

LIVE UPDATES: Mkutano wa CCM Morogoro

ccm wanahitaji rudi tafuta gamba ingine.kinana hana mvuto wala ushawishi zaidi ya kutia huruma.

Hotuba zake zaidi zaidi zinaonekana kuwa umbea zaidi ya kitu chenye maana.

Magamba wanahitaji rudi dodoma kutengeneza mkutano mwingine unaofafanana na shamba la aliyeti kwa rangi ya kijani na njano.

Sijui wamemaliza reserve.
 
Kinana naye anafikiri kuwa wanachi ni wajinga kiasi kwamba anaweza kuwadangaya kirahisi namna hiyo..
Hakuna chochote kilichofanywa kwa manufaa ya wananchi na ccm zaidi ya ufisadi unaothibitisha ubinafsi ndani ya chama hicho.. sasa anawaambia wananchi chadema ina ubinafsi pasipo kuangalia ubinafsi uliokithiri katika uvunaji wa rasilimali za nchi.
 
Nipo katika mitaa ya mji kasoro bahari kama kawaida naona jezi za ccm zimetapakaa maeneo mengi ya mji huku maroli na mabasi ya abiria yakisombawanachama toka pande zote za mkoa ili kuhudhuria mkutano wao.

Bodaboda zinaanza kuadimika mara baada ya ccm kuwakodisha kwenda katika maandamano


Kama kawaida yao Katibu wa Zanzibar aanza na mipasho kwa kukashifu CUF kuwa toka kinaanzishwa baba na mama na kitanda kilivyoanzishwa na mimba ilivyoingia anajua.

Ila kwa ufupi watu ni wachache mnoo sio kama ilivyotarajiwa na raia wengi wamekaa kwenye viti.

Updates.

Mbunge wa morogoro anaongea ila kama JK lazima asome.

Nape anaona watu wanaondoka anawambia Diamond anatudi stejini kuburudisha
inanikumbusha 2010 Mbeya JK alkuja na original comedy kitendo cha comedy kumaliza na JK Kusimama watu wakanza kusepa.
 
Sijui kuhusu CUF lakini chadema walishasema wamesusa na hawataki TBC itangaze habari zao.

CDM Sababu waliibainisha?
Na cuf je?
Pia kwa wakati huu tunaruhusu kuonesha mikutano ya vyama live kwenye TV ya taifa wakati si kipindi cha kampeni?
NITOENI PORINI WADAU.
 
Aliyetukana ni nani? au Tv yako king'amuzi kinakamata Billicana club? maaba huko ndo chuo cha matusi . ww vp?
huko ndiko walikojifunzia matusi lusinde,mwinguru,mkamia,na seru-kamba eh.
 
Chadema wanaangalia maslahi yao si ya watanzania,tujihadhari nao wanakotupeleka sipo
 
TBC nani anaangalia siku hizi? matangazo waliyo nayo ni kusafisha wauaji na wang'oa kucha meno na macho bila ganzi.
 
CDM Sababu waliibainisha?
Na cuf je?
Pia kwa wakati huu tunaruhusu kuonesha mikutano ya vyama live kwenye TV ya taifa wakati si kipindi cha kampeni?
NITOENI PORINI WADAU.

CDM kususa ni kawaida yao.

CUF sijui kama wameshawahi kuomba huduma ya TBC wakakataliwa.

TBC kurusha matangazo ya vyama ni sawa kwa sababu siasa ni sehemu ya shughuli za jamii, lakini hawapaswi kupendelea chama fulani. Kila chama kikiomba huduma kinatakiwa kipewe equal consideration.
 
CCM bado ina nguvu Morogoro msibeze, kuna kazi ya kufanya bandugu!

Mkuu uko sahihi ccm Moro bado ina watu ambao tongotongo bado halijawatoka, Kilosa bado mwamko uko chini kabisa. Mjini na kwenyewe kazi ya ziada inabidi ifanywe na lazima kieleweke.
 
baba yangu kinana analialia 2 hotuba nzima,hivi huo mkutano wao ni wa kuiongelea CDM au kuwaeleza watanzania utekelezaji wa ilani yenu?yani hakuna hoja ni kulia 2,na bado mtaendelea kulia hivyohivyo mpaka 2015
 
Back
Top Bottom