Live: Kutoka Mbamba bay mkutano wa Dk. Slaa

Live: Kutoka Mbamba bay mkutano wa Dk. Slaa

Chishango

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2008
Posts
875
Reaction score
363
Wakuu kama nilivyowaeleza jana kuwa kutakuwa na mkutano mkubwa hapa Mbamba Bay watu wanaendelea kumiminika uwanja wa Polisi hapa Mbamba Bay wakimsubiri Dk. Slaa.

Mch. msigwa ameshawasili hapa pamoja na viongozi wengine, katibu wa chama wilaya anamkaribisha mch. Msigwa naye anawasalimia wananchi na moja kwa moja anawaambia kuwa Rais wetu ni mtalii nchi ina rasilimali nyingi lakini inafilisiwa na wezi yaani CCM.

Bado dk. Slaa hajawasili.

UPDATE:
Dk slaa kawasili kwa helikopta analakiwa kwa vifijo na nderemo na vigelegele akina mama wanalala chini hali inayomzuia kuendelea kuelekea jukwaani ...hatimaye anapanda jukwaani anakaribishwa mara moja ili kwenda na wakati....anaanza kwa salaamu ya chama then anaomba radhi kwa kuchelewa anawaambia wanyasa kuhusu maendeleo chini ya serikali hii ya CCM wasahau kwani hawana jipya wamechoka hawana visheni....anagusia kuhusu safari za rais anawaambia wanyasa safari ya juzi ya JK ni ya 358 tangu aingie madarakani hana muda na watanzania na watz waliomchagua .......anaendelea.... CCM wana mpango a kuhujumu mchakato wa katiba mpya hawataki kuona katiba ya watanzania wote inapatikana....anawaambia wananchi kuwa zaidi ya 72% ya mapendekezo ya rasimu ya katiba mpya ni ya Chadema....anawaambia vijana wajitokeze kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la kudumu anamaliza na kuondoka kuendelea na ratiba maeneo mengine.

Leo Dr. Slaa akizungumza na wa Mbamba bay amesema safari ya mwisho ya JK ilikuwa ni ya 358.

Kama safari za JK zimefikia 358, yaani jumla yake ni karibu sawa na siku za mwaka mmoja; na kama tukisema kuwa katika kila safari alitumia siku 2 tu huko nje, basi ni sawa na kusema kuwa ha.tu.ku.wa na raisi kwa miaka miwili katika miaka minane ya JK ikulu. Kwa lugha nyingine:
based on my assumption that JK spent only 2 days in each trip, basi ni sawa na kusema kuwa, asilimia 25% ya muda aliokaa JK ikulu ameutumia angani (nje ya nchi).



1616320_563207830437574_72167640_n.jpg 1616320_563207830437574_72167640_n.jpg 1616758_563207597104264_1594604505_n.jpg 1579805_563208650437492_1008271359_n.jpg 1606908_624879004226083_707136898_n.jpg
 

Attachments

  • 1085227_563193920438965_1701766001_n.jpg
    1085227_563193920438965_1701766001_n.jpg
    28.2 KB · Views: 1,863
  • 1558790_563194133772277_494047750_n.jpg
    1558790_563194133772277_494047750_n.jpg
    27 KB · Views: 1,832
  • 1608747_563208360437521_1809778408_n.jpg
    1608747_563208360437521_1809778408_n.jpg
    44.9 KB · Views: 1,578
Na bado wale woote wakaanga sumu watazinywa wenyewe tutawakimbiza mpaka 2015.
 
Hii hatari kabisa, yaani msururu wote huo na Dr. bado kufika?
 
Teh teh teh ccm chali,Nape wapi iyoooo hahahaaaa Kinana kimya baada ya Jk kutangaza baraza la Mawaziri...
 
Hongera Chadema Chama cha Walinzi wa Rasilimali za Taifa.

Hilo jina la Mbamba Bay linafanana kama Congo vile,
 
Hongera Chadema Chama cha Walinzi wa Rasilimali za Taifa.

Hilo jina la Mbamba Bay linafanana kama Congo vile,

Unaonekana kilaza wa kutupwa..CDM wamelinda rasilimali gani za taifa?

Na umesoma Jografia gani ya kuifananisha Mbamba bay na Congo?..dIV5 Loading.............
 
MIMI namtaka nape na KINANA na kamati kuu ya CCM waliafikiana vipi na JK kuendelea na mawaziri mizigo?hapo ndipo tunawataka waje kutueleza mawaziri mizigo ina maana JK yeye awaoni big up CHADEMA toeni elimu ya uraia
 
kamanda tunakushukuru sana kwa uaminifu wako , jana ulituahidi kutuletea live updates na leo umetimiza , ubarikiwe sana .
 
Watu weweeeeeeee!!!!!!!!!!chadema wamechachamaa cha! tupe mavitu kijana
wapi mwanamuziki komba nyoka kaingiga chumban lazima utoke
 
hiki chama kinanifurahisha huwa hakiishiwi mipango hata, Hakiishiwi rasilimali watu pia, wasaliti wameondoka sasa hivi kimekuwa chepesi kweli.
 
mleta mada nakupa hongera ila picha zako hazina kiwango na hazichukui eneo kubwa la mkutano
 
Hiki chama kinanipa raha hatari.....lets keep on moving
 
hiki chama kinanifurahisha huwa hakiishiwi mipango hata, Hakiishiwi rasilimali watu pia, wasaliti wameondoka sasa hivi kimekuwa chepesi kweli.

hiyo ndiyo cdm mkuu , waliodhani tunatania wataisoma namba !
 
Makamanda tukotayari kukabidhiwa nchi na mah.uni, ya ccyem yanayopagawa yakisikia jina chadema.
 
Back
Top Bottom