Live Coverage from Mzenga Old Stand Grounds Mlandizi

Live Coverage from Mzenga Old Stand Grounds Mlandizi

M4C itapita kila kona,unajua kuna mikutano mingapi ya CDM leo nchi nzima?
Mkurugenzi wa Mafunzo na Organaizesheni wa Chadema Taifa Singo Bensoni alisema Lengo la Mafunzo hayo ni kuhakikisha wanapata wakufunzi 30606 nchi nzima ambao watatawanyika katika kila kitongoji nchi nzima kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi na kuunda matawi ya Chama hicho ikiwa ni pamoja na kukifikishama hadi ngazi ya Chini
 
zitto naona alienda kwenye kampen ya kikwetukwetu iliyo kuwa inatangazwa na BLAAAUZI FM.
 
Diwani wa CDM Picha ya Ndege yuko jukwaani sasa,anasema kwamba kazi kuu tuliyonayo ni kuikomboa Kibaha,CCM wawe wapinzani maeneo haya,wamewapuuza wananchi kwa muda mrefu. sasa hawawezi tena,waondolewe
 
Wana JF,

Naomba mniruhusu kuwaletea kinachojiri au yatakayojiri katika viwanja hivi ambapo makamanda wa CDM wana mkutano wa hadhara wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kanda, Mabere Nyaucho Marando

granted kamanda tupiamo ma updates na mapicha mpaka wakae magamba!
 
M/Kiti Bavicha Mkoa wa Pwani anaongelea kuhusu joka la ccm,jinsi linavyoiba pesa za walalahoi halmashauri,ccm sasa wanapora ardhi na kuwapa watu wanaowafahamu wao kutoka dsm,wananchi wa Kibaha vijijini wamenyang'anywa ardhi Ruvu
 
Mzee amepanda jukwaani,anasema ni muda wa vijana kuleta mabadiliko ya nchi hii,muda ni sasa
 
Wasikilizeni hao watumishi wa Mungu, akina Musa wa Tanzania.
 
Anawasihi wananchi kuanza kuiadhibu CCM kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa
 

Attachments

  • IMG00005.jpg
    IMG00005.jpg
    16.5 KB · Views: 111
  • IMG00006.jpg
    IMG00006.jpg
    15.5 KB · Views: 95
M/kiti wa CDM Temeke yuko jukwaani sasa,anasema CDM ni chama pekee kilichopo kwa sasa ambacho ni tumaini la watanzania,wananchi wanaaswa hapa kufuatilia mabadiliko yanayotokea nchini juu ya wananchi kukataa kukandamizwa na kunyonywa,Mtwara inatolewa kama mfano
 
M/kiti CDM Ilala yuko jukwaani sasa,anasema kwamba muda wa mabadiliko ni sasa,mabadiliko ya kuelekea kwenye serikali makini na adilifu,wananchi waangalie sasa chama kinachosimamia maslahi ya wanyonge,CCM imeshindwa kuwaletea wananchi maendeleo,watupwe sasa
 
Muwakilishi kutoka K'ndoni anasema,mashina na matawi yanayoendelea kufunguliwa yawe imara,yajenge mbinu za hakika kuiondoa ccm madarakani kuanzia "level" ya familia
 
Muwakilishi kutoka K'ndoni anasema,mashina na matawi yanayoendelea kufunguliwa yawe imara,yajenge mbinu za hakika kuiondoa ccm madarakani kuanzia "level" ya familia
Mama, baba, mtoto, bibi na babu (MBBBM), Ndio
 
Back
Top Bottom