oooh, my God!
dunia hii??
watu wamekuwa wanyama mwitu, sijuui tukimbilie wapi??
kwa kweli bila Yesu, dunia ni ubatili mtupu!!
===================
1.
Yesu nakupenda, u mali yangu,
anasa za dunia, kwangu sitaki,
Yesu nakupenda, u mali yangu,
anasa za dunia, kwangu sitaki
njoo njoo Yesu, maishani mwangu,
njoo njoo ukae, rohoni mwangu,
shetania anivizia, simtaki kwangu,
njoo njoo Yesu, uniokoe,
tukimaliza kazi, tutavikwa taji,
tutaimba wimbo mpya wa Mwana Kondoo,
watakaoshinda vita vya dunia hii,
waimba pamoja na na Malaika,
wataoshindwa vita vya dunia hii,
walia pia na kusaga meno!!
2.
maisha ya dunia, yamejaa taabu,
nimejitahidi sana, sikufanikiwa,
maisha ya dunia, yamejaa taabu,
nimejitahidi sana, sikufanikiwa,
dunia ni ubatili, ubatili mtupu,
maisha ni maua, yanyauka upesi,
duniani si kwetu, kwetu ni mbinguni,
tutamani ya Mbinguni, ruache ya dunua!!
tukimaliza kazi, tutavikwa taji,
tutaimba wimbo mpya wa Mwana Kondoo,
watakaoshindwa vita vya dunia hii,
waimba pamoja na na Malaika,
wataoshindwa vita vya dunia hii,
walia pia na kusaga meno!!
SHUKRANI: ST. JAMES TUMAINI CHOIR-KALOLENI
ARUSHA
WIMBO: YESU NAKUPENDA
ALBUM: SILAHA YA USHINDI
mbarikiwe sana wapendwa,
Glory to God!