LIVE:Breaking news:CHARLES TAYLOR SENTENCING

Hatimaye aliyawahi kuwa raisi wa liberia ndugu charles taylor baada ya kutiwa hatiani na mahakama ya kimataifa ya haki za binadamu, leo hii amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka hamsini (50) gerezani.

Suala la kutafakari hapa ni, je adhabu aliyopewa inalingana na kosa alilolifanya kwa nchi na raia wa liberia kwa ujumla?

Je angekuwa ni kiongozi wa nchi za magharibi kama vile marekani angetiwa hatiani na kupewa adhabu hiyo?

Je mahakama hii ya kimataifa ni kwa ajili ya viongozi wa kiafrika tu?

Je kuna haja ya watu wanaotuhumiwa kwa makosa kama ya charles taylor kufunguliwa mashtaka katika mahakama za nchi husika?

Mapendekezo/maoni/ushauri/mitazamo yenu ni muhimu sana.

Siiiungi mkono hii mahakama hata kidogo. Ni mahakama ya kinafiki kweli kweli. Taylor alikamatwa na kufungwa Marekani lakini Marekani wakamwachia (ati alitoroka toka gereza la Marekani!!!!) kwa kazi maalumu. Huo ndio ukawa mwanzo wa vita. Taylor alikuwa akifanya kazi za wamarekani na baada ya kumtumia wakaamua kumtosa. Wao ndio walipanga mpango Taylor apewe hifadhi Nigeria na kisha wao hao hao wakamkamata na kumpeleka kwa Ocampo.

Naamini silaha zinazotumika Afrika zinatoka ulaya magharibi na mashariki. Wanasema Taylor alikuwa akiwapatia RUF ya Fadoy Sankoh silaha baada ya kubadilishana silaha na madini ya almasi; hizo silaha zilikuwa zikitoka wapi? Naamini zilitoka Ulaya. Je hao walaya (wazungu wa ulaya) hawana mikono yao kwenye hiyo vita? Huu ni usanii mtupu. Wantuuzia silaha tunauana kwa maelfu halafu wanamchukua mmoja wanaenda kumpumzisha the Heague.

Hivi Bush kwa viwango vyovyote si muuaji?
 
MAHAKAMA ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita ya mjini The Hague, imemhukumu kifungo cha miaka 50 jela aliyekuwa Rais wa Liberia Charles Taylor.

Baada ya kesi iliyodumu miaka sita, Taylor alipatikana na makosa kumi na moja ya kufadhili na kusaidia waasi nchini Sierra Leone, ili apate madini ya almasi.

Taylor ni kiongozi wa kwanza wa zamani kuhukumiwa na mahakama ya kimataifa tangu kumalizika kwa vita vya pili.

Source BBC
 
Sijaona kiongozi yeyote wa Ulaya au Amerika akifunguliwa mashitaka juu ya uhalifu.
Hii mahakama imekaa kwa ajili ya viongozi wa Afrika tu na si vinginevyo
 
Sijaona kiongozi yeyote wa Ulaya au Amerika akifunguliwa mashitaka juu ya uhalifu.
Hii mahakama imekaa kwa ajili ya viongozi wa Afrika tu na si vinginevyo

Hawana tabia mbovu na za ki-uaji kama hao
 
PM wa zamani wa UK, kesi yake imekaa vibaya, maana inasemekana alipata rushwa baada ya vita ya Iraq..... malipo yalipitia Investment Bank Moja ya USA.... subiri tuine!

Sijaona kiongozi yeyote wa Ulaya au Amerika akifunguliwa mashitaka juu ya uhalifu.
Hii mahakama imekaa kwa ajili ya viongozi wa Afrika tu na si vinginevyo
 
Harooooooooo,kwani huyu jamaa ana miaka mingapi? Miaka 50 ni umri wa mtu mzima si wangesema wanamfunga maisha tu? Sina hakika how old he is. Lakini I can guess he is more than 50 years old, sasa ukichanganya na hii 50 inakuwa 100+ maana yake huyu jamaa ni wa kufia gerezani. Saafi sana, hebu hili na liwe fundisho kwa madikteta wote na viongozi wa kiafrika wanaotawala watu kwa mabavu. Pambaf zao!
 
Sijaona kiongozi yeyote wa Ulaya au Amerika akifunguliwa mashitaka juu ya uhalifu.
Hii mahakama imekaa kwa ajili ya viongozi wa Afrika tu na si vinginevyo

ulitaka wa ulaya wapelekwe hata kama hawana makosa! hii mahakama inatufaa sana waafrika kwa kuwa mahakama za kwetu hazitoi haki kabisaaaa! acha yakamatwe na kufungwa mi hata siwaonei huruma kwa kuwa wao hawana huruma na walalahoi, majitu yanang'ang'ania madaraka as if ni their birth right!
 
Federal Offence that's only 25 years in Jail; they count Day and Night
 
Sijaona kiongozi yeyote wa Ulaya au Amerika akifunguliwa mashitaka juu ya uhalifu.
Hii mahakama imekaa kwa ajili ya viongozi wa Afrika tu na si vinginevyo

kwa kweli kama hujui basi ingia mitandao yao usome.
 
Rais wa Siera Leon Charles Taylor mwenye miaka 64 ahukumiwa miaka 50 jela na the Hague baada ya kupatikana na kosa nyanyasaji na mauaji ya watu
 
Back
Top Bottom