List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania

Ili nchi tusonge mbele, hawa watu inatakiwa wanyongwe.

1. ANDREW J. CHENGE

Mheshimiwa Andrew Chenge ni Mbunge wa Bariadi Magharibi na Waziri wa Miundombinu katika Serikali ya sasa ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Kabla ya hapo, Mheshimiwa Chenge alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa miaka yote kumi ya utawala wa Rais Benjamin W. Mkapa. Kwa wadhifa huo, Mheshimiwa Chenge ndiye alikuwa "mshauri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano juu ya mambo ya sheria na &[HASHTAG]#8230[/HASHTAG]; aliwajibika kutoa ushauri kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano kuhusu mambo yote ya kisheria, na kutekeleza shughuli nyinginezo zozote zenye asili ya au kuhusiana na sheria&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];." Katika kipindi hicho cha miaka kumi na mbili, Mheshimiwa Chenge amehujumu taifa la Tanzania kama ifuatavyo:

(i) Kama Mkurugenzi katika kampuni ya kigeni ya Tangold Limited alishiriki na/au kufaidika na malipo haramu ya dola za Marekani 13,736,628.73 ambazo zimeelezewa kwa kirefu katika sehemu inayomhusu Gavana Balali;
(ii) Kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mheshimiwa Chenge ameshiriki kuishauri vibaya na/au kutokuishauri vizuri Benki Kuu ya Tanzania na kusababisha ufujaji wa mabilioni ya fedha za umma ambayo yameelezewa katika sehemu inayomhusu Gavana Balali;
(iii) Kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mheshimiwa Chenge ameshiriki moja kwa moja katika kutoa ushauri kwa Serikali na/au Wizara ya Nishati na Madini kuingia mikataba mibovu na makampuni mbali mbali ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa limepoteza mabilioni ya fedha za kigeni. Kwa mfano, katika hotuba yake Bungeni tarehe 6 Novemba 2006, aliyekuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mheshimiwa Bernard Membe alitoa taarifa kwamba katika kipindi cha miaka mitatu hadi kufikia 2006, makampuni ya uchimbaji dhahabu yaliyoko Tanzania yaliuza dhahabu yenye thamani ya shilingi bilioni 2,340 wakati ambapo makampuni hayo yalilipa mrahaba na kodi nyinginezo kwa Serikali za shilingi bilioni 72. Katika kikao cha Bunge la Bajeti la mwaka huu, Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mheshimiwa William Ngeleja aliliambia Bunge kwamba katika kipindi cha kuanzia mwaka 1998 Mgodi wa kwanza wa dhahabu wa Lusu Nzega ulipofunguliwa hadi mwaka huu, makampuni ya uchimbaji dhahabu yaliuza nje dhahabu yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 2.614 wakati Serikali ikiambulia mrahaba wa dola milioni 78 tu! Endapo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Chenge angeishauri vema Serikali ya Jamhuri ya Muungano kama alivyotakiwa na Katiba ya nchi yetu, taifa lisingekuwa linapoteza utajiri wake wa madini kwa kiasi kikubwa namna hii.

2. BASIL P. MRAMBA

Mheshimiwa Basil Mramba ni Mbunge wa muda mrefu wa Jimbo la Rombo na Waziri wa Viwanda na Biashara na kwa miaka kumi ya utawala wa Rais Mkapa alikuwa ndiye Waziri wa Fedha. Katika kipindi hicho cha miaka kumi, Mheshimiwa Mramba amehujumu taifa la Tanzania kama ifuatavyo:

(i) Kwa kutumia wadhifa wake kama Waziri wa Fedha, alishinikiza kampuni ya Alex Stewart (Assayers) Government Business Corporation ya Washington DC, Marekani kupewa kazi ya kukagua mahesabu ya makampuni ya uchimbaji dhahabu. Chini ya mkataba wake na Serikali ya Tanzania, Kampuni hiyo inalipwa asilimia 1.9 katika ya asilimia 3 za mrahaba inaolipwa Serikali ya Tanzania na makampuni ya madini ya dhahabu. Kufuatana na barua ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu, katika mwaka wa fedha 2005/06, Alex Stewart (Assayers) walilipwa shilingi 14,175,753,189.46 kama malipo ya ukaguzi wa mahesabu ya makampuni ya dhahabu, ijapokuwa "hakuna ripoti za ukaguzi zilizowasilishwa na wakaguzi hawa kuhusu ukaguzi uliofanywa katika mwaka 2005/06"! Vile vile Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu alisema katika barua yake kwamba "hakuna ushahidi wowote wa kuthibitisha kwamba wakaguzi hawa wa dhahabu walipatikana kwa kufuata utaratibu wa zabuni ya ushindani."

(ii) Vile vile kuna taarifa za kuwepo kwa rushwa na/au ufisadi mkubwa kuhusiana na mkataba kati ya Serikali na Alex Stewart Assayers. Barua pepe iliyoandikwa na Erwin Flores ambaye ni Makamu wa Rais Mtendaji wa kampuni hiyo ya Novemba 14, 2006 inamtaja mtu mmoja mwenye jina la Bwana Basil ambaye ana wadhifa wa Waziri katika serikali ya Jamhuri ya Muungano na kuwa yeye pamoja na wenzake ambao hawakutajwa wana asilimia 12.5 za hisa kwenye kampuni hiyo na kuwa analipwa na kampuni hiyo. Kwa mujibu wa Flores, hakuwezi kukawa na ushahidi wowote kuthibitisha kwamba &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];Bwana Basil' anapokea malipo kutoka kwa Alex Stewart kwa vile malipo yote kwake yamekuwa yakifanyika nje ya nchi. Kwa kadri tunavyofahamu, mtu pekee aliyekuwa waziri katika serikali ya Awamu ya Tatu na ambaye pia ni waziri katika Serikali ya Awamu ya Nne na ambaye ana jina la &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];Basil' ni Mheshimiwa Basil Pesambili Mramba. Tumemtaka Waziri wa Fedha kutupatia nakala ya Mkataba kati ya Benki Kuu na Alex Stewart, na kuwataka Mheshimiwa Basil Mramba na Erwin Flores walete maelezo yao kwetu kwa mujibu wa Sheria ya Mamlaka, Haki na Kinga za Bunge ya mwaka 1988 kwa barua yetu ya tarehe 18 Julai 2007 ili waweze kujibu tuhuma hizi. Bado tunasubiri majibu hayo.

(iii) Mheshimiwa Mramba amehusishwa pia na ufujaji na/au matumizi mabaya ya fedha za umma na uuzaji holela wa rasilmali za taifa letu. Kashfa hizo ni pamoja ni ununuzi wa rada ya kijeshi, ununuzi wa ndege ya Rais, na ubinafsishaji wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) na National Microfinance Bank (NMB).

3. GRAY S. MGONJA

Bwana Gray Mgonja ni Katibu Mkuu wa siku nyingi wa Wizara ya Fedha. Vile vile ni Mkurugenzi wa Benki Kuu ya Tanzania na anashikilia nafasi ya ukurugenzi katika kampuni ya kigeni ya Tangold Limited ambayo maelezo yake tumeyatoa kuhusiana na ufisadi unaomhusu Gavana Balali na Andrew Chenge. Kwa kuzingatia nafasi yake kama Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Mkurugenzi katika Benki Kuu na vile vile Mkurugenzi katika Tangold Ltd. iliyolipwa mabilioni ya fedha za umma katika mazingira yenye utata mkubwa, ni wazi kwamba kumekuwepo mgongano mkubwa wa kimaslahi unaomhusu Bwana Mgonja.

4. PATRICK W.R. RUTABANZIBWA

Kwa miaka mingi Patrick Rutabanzibwa alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini wakati mikataba mibovu ya madini inasainiwa na kashfa kubwa ya IPTL inatokea. Kwa sasa Bwana Rutabanzibwa ni Katibu Mkuu Wizara ya Maji na vile vile Mkurugenzi wa kampuni ya kigeni ya Tangold Limited. Ufisadi unaomhusu umeelezewa kwa kina katika maelezo yanayomhusu Gavana Balali na Andrew Chenge. Hapa pia kuna mgongano mkubwa kati maslahi yake binafsi kama Mkurugenzi wa kampuni binafsi iliyopokea mabilioni ya fedha za umma na maslahi ya umma aliyotakiwa kuyalinda akiwa kama kiongozi wa umma.

5. NIMROD ELIREHEMA MKONO

Mheshimiwa Nimrod E. Mkono ni Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijiji na Mshiriki Mkuu wa kampuni ya mawakili ya Mkono & Company Advocates ya Dar es Salaam. Barua ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali inaainisha kuwa Benki Kuu imekuwa ikilipa malipo makubwa kwa Mkono & Co. Advocates hasa yale yanayohusu kesi ya Valambhia ambapo Benki Kuu inadaiwa jumla ya shilingi bilioni 60. Kwa mujibu wa barua ya wakaguzi tayari Mkono & Co. Advocates wamekwishalipwa shilingi 8,128,375,237 kwa fedha taslimu kwa kesi hiyo ambayo bado iko mahakamani. Malipo haya ni sawa na asilimia 13.5 ya deni lote inalodaiwa Benki Kuu. Hoja ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu ni kuwa kesi hii haina muda maalumu wa kumalizika na hivyo inawezekana kabisa malipo ya wanasheria yakazidi kiasi cha fedha inachodaiwa Benki Kuu.

Lakini hoja nyingine ya kimsingi ni kama malipo haya kwa mawakili yanaruhusiwa chini ya Kanuni za Malipo ya Mawakili na Uamuzi ya Gharama za Kesi za mwaka 1991, Tangazo la Serikali Na. 515 la mwaka 1991 (Advocates' Remuneration and Taxation of Costs Rules, 1991). Kanuni hizi zimeweka kiwango cha malipo ya mawakili katika kesi ambazo fedha inayodaiwa ni zaidi ya Shilingi milioni 10 kuwa ni asilimia tatu. Kwa kufuata masharti ya sheria hii ya malipo ya mawakili, kampuni ya Mkono & Co. Advocates ilipaswa kulipwa Shilingi bilioni 1.8.

Kampuni ya mawakili ya Mkono & Co. Advocates imekuwa ikitajwa kuhusiana na kashfa kubwa za ufujaji na/au ubadhirifu wa fedha za umma kwa muda mrefu. Kwa mfano, &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];Taarifa ya Uchunguzi Kuhusu Tuhuma Dhidi ya Makampuni ya Tanfarms Ltd., Makinyumbi Estates Ltd., Centrepoint Investments Ltd., na Arusha Farms Ltd. Yanayomilikiwa na V.G. Chavda Kuhusiana na Matumizi Mabaya ya Fedha za Debt Conversion Programme' iliyotolewa Bungeni na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Mheshimiwa Edward Oyombe Ayila mwezi Novemba 1994 ilisema yafuatayo kuhusu Mheshimiwa Nimrod Mkono: "Mhe. Spika si nia yangu kulichosha Bunge lako tukufu na hotuba ndefu lakini ni vizuri nikaelezea juu ya uhusiano unaotia mashaka kati ya V.G. Chavda na Mashamba yake na Subash Patel mwenye makampuni ya DECO ART, MM Motors, MM Garage, Hotel Sea Cliff, City Bureau De Change na Nimrod Mkono, Wakili wa kujitegemea ambaye pia ni Mkurugenzi katika makampuni ya AZANIA AGRICULTURAL ENTERPRISES, LIBERTY LEATHER SHOE LTD., AZANIA EXIMCO, n.k. (AIMS GROUP OF COMPANIES)

Baada ya kuelezea uhusiano huo ulivyokuwa Mheshimiwa Ayila alimalizia kwa kusema yafuatayo: "Mheshimiwa Spika, ni vigumu kabisa katika hali ya kawaida kwa mtu yeyote kuamini kwamba makubaliano haya na uhusiano uliojitokeza hapa haukuwa wa hila. Chavda kwa kupitia wakili wake Nimrod Mkono, aliomba Mahakama Kuu kuzuia kabisa shughuli za Kamati (permanent injunction). Aidha ni wakili huyo huyo ambaye ameshuhudia uuzaji wa deni la Deco Art (reassignment) kwa Chavda. Mheshimiwa Spika, hali hii ukiitazama kwa undani utaona kwamba pengine kuna kitu kinafichwa. Nimrod Mkono alikuwa Mkurugenzi Mkazi wa Kampuni ya Oxford Services Ltd. na pia anamiliki Kampuni ya Marcus Ltd., makampuni ambayo kwa pamoja yamefaidika kwa kuupata jumla ya Shs. 4,477,870,279.61 chini ya utaratibu wa DCP."

6. BENJAMIN WILLIAM MKAPA

Benjamin William Mkapa alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia mwaka 1995 hadi 2005 alipomaliza kipindi chake cha pili. Ufisadi wote ulioelezewa katika waraka huu ulitokea wakati wa utawala wa Rais Mkapa na anawajibika nao moja kwa moja ama kwa kuubariki au kwa kuunyamazia. Zaidi ya hayo, kuna ushahidi unaoonyesha kwamba wakati akiwa madarakani Rais Mkapa alishiriki moja kwa moja au kwa kutumia ndugu na/au washirika wa karibu wa familia yake katika ufisadi mkubwa na uliolipotezea taifa fedha nyingi. Kwa mfano, wakati akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mkapa alitumia wadhifa huo kuhakikisha kwamba kampuni iitwayo Tanpower Resources Limited inamilikishwa asilimia 85 ya hisa za kampuni ya Kiwira Coal Mines Ltd. inayochimba mkaa wa mawe huko Kiwira Mkoani Mbeya. Hisa zilizobaki asilimia 15 zinamilikiwa na Serikali. Tanpower Resources Ltd. ni kampuni iliyoanzishwa kwa ajili ya kuinuifaisha familia ya Rais Mkapa na washirika wake wa karibu. Taarifa za BRELA zinazonyesha kwamba wakurugenzi wa Tanpower Resources Ltd. ni Anna Mkapa, mkewe Rais Mkapa, Nicholas Mkapa, mtoto wa Rais, Bwana Joseph Mbuna, wakili wa kujitegemea na baba mkwe wa Nicholas Mkapa, Daniel Yona, Waziri wa Nishati na Madini wakati wa utawala wa Rais na bwana Joesph Mapundi. Baada ya Tanpower Resources Ltd. kutwaa umiliki wa Kiwira Coal Mines Ltd. kwa nguvu za Ikulu ya Rais Mkapa, iliingia mkataba na Shirika la Ugavi wa Umeme nchini TANESCO wa kujenga mtambo wa kuzalisha umeme kwa kutumia mkaa wa mawe na kuiuzia umeme TANESCO. Mkataba huo utainufaisha kampuni ya Kiwira Coal Mines Ltd., na kwa hiyo Rais Mkapa, familia na washirika wake wa karibu kwa kiasi cha dola za Marekani milioni 271 kwa wakati wote wa mkataba.

7. RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE

Rais Jakaya Kikwete amekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia Desemba 2005. Kabla ya kuwa Rais, Mheshimiwa Kikwete alikuwa Waziri wa Mambo Nje na Uhusiano wa Kimataifa kuanzia 1995 hadi 2005, Waziri wa Fedha 1994 hadi 1995 na Waziri wa Maji, Nishati na Madini kuanzia mwaka 1990 hadi 1994. Kama Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mheshimiwa Kikwete alishiriki moja kwa moja katika kusaini mikataba mibovu ya madini na makampuni ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa limeendelea kupoteza utajiri mkubwa na kuinyima Serikali uwezo wa kifedha wa kuhudumia wananchi. Kwa mfano, mnamo tarehe 10 Aprili 1990, Major Jakaya Mrisho Kikwete aliingia mkataba wa madini ya kampuni ya SAMAX Limited ambapo kampuni hiyo ilipewa leseni ya kuchimba dhahabu katika eneo la Lusu, Wilayani Nzega Mkoa wa Tabora. Matokeo ya mkataba huo, maelfu wa wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu waliokuwa eneo hilo waliondolewa kwa nguvu na vikosi vya FFU na bila ya kulipwa fidia yoyote. Hadi leo wananchi hao hawajalipwa fidia yoyote licha ya miaka zaidi ya kumi ya kufuatilia haki zao. Baada ya kutwaa utajiri wa dhahabu wa eneo hilo, SAMAX Limited iliuza eneo hilo kwa kampuni ya Ashanti Goldfields ya Ghana kwa dola za Marekani milioni 253. Ashanti Goldfields nao wakauza eneo kwa kampuni ya Resolute Limited ya Australia kwa kiasi kisichojulikana cha fedha za kigeni. Resolute Limited ndio waliojenga na wanamiliki Mgodi wa Dhahabu wa Golden Pride ulioko eneo la Lusu, Nzega hadi sasa na ambao ulifunguliwa mwezi Novemba 1998.

Mnamo tarehe 5 Agosti 1994 Luteni Kanali Jakaya Mrisho Kikwete aliingia tena mkataba na kampuni ya madini Kahama Mining Corporation Ltd., kampuni tanzu ya kampuni ya Sutton Resources ya Canada. Ijapokuwa mkataba huu unaonyesha wazi kwamba ulikuwa unahusu eneo la Butobela Wilaya ya Geita Mkoani Mwanza, mwezi Agosti mwaka 1996 Kahama Mining Corporation wakisaidiwa na vikosi vya FFU walivamia eneo la Bulyanhulu, Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga na kuwaondosha kwa nguvu watu takriban laki nne waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo hilo. Baada ya kutwaa eneo hilo kwa nguvu za kijeshi, Sutton Resources iliiuza Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu kwa Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto, Canada kwa dola za Marekani milioni 280. Leo hii Bulyanhulu ni moja ya migodi tajiri kwa dhahabu katika Bara la Afrika.
 
Watakua wamefanya jambo la maana if really we need reforms lazima tuanzie huko mafisadi wote warudishe hela ya serikali na wale ambao kwa macho ya kawaida hawaonekani wakatwe mikono
Dah kumbe saanane mpambanaji wa miaka mingi.... Hii post imenitoa chozi..... Afu viongozi wa upinzani wamelala tu mtu haonekani mwaka sasa
 
Hii mada hakuna mwandishi anayeweza kuibua mjadala huu huko kwenye magazeti ...HAYUPO ....mambo yaliyojadiliwa humu yalipaswa kuendelea kujadiliwa hadi tupate mwafaka ....Chadema vinara wa issue hii wameshaifuta kwenye tovuti yao ....UNAFIKI wa kutisha ....shame on you ...
Chama chako CCM ilichukua hatua gani???
 
Haya maneno yako ni ya ovyo kweli kweli lakini ni haki yako kidemokrasia kuyatoa.

Tanzania ninayo ijua mimi ni ya kubishana kwa hoja na si kwa mitutu ya bunduki.HARAKATI za kudai demokrasia hazijawahi kuwa nyepesi.
Demokrasia gani tena unayoitaka mkuu?
Nafikiri labda una matatizo ya kufahamu nini hasa maana ya demokrasia? Naomba nenda North korea hapo nafikiri ndiyo utaweza tofautisha kati ya udikteta na demokrasia.

Mbona wewe mkuu unatumia huu mtandao kuji eleza mwenyewe unachotaka? Una weza safiri nchi yeyote ile unayo taka na bila ruhusa ya serikali?
Una uwezo wa kuwasiliana na mtu yeyote yule alipo ulimwenguni kwa whatsapp, tweeter, Facebook, instagram na mingineyo mingi, wa north korea hawana fursa hiyo. Barua zako kutoka nje hazifunguliwi pia.

Una ruhusiwa kufanya biashara na nchi yeyote ile, wa north korea hawana ruhusa hiyo.

Akina Msigwa & co. wanaweza sema lolote wanalo litaka kuhusu Magufuli na serikali yake, wa north korea hawana fursa hiyo.

Tuna vyama vingi wa north korea hawana vyama vingi.

Katia bunge letu kuna block la wapinzani wa north korea hawana kitu kama hicho. Mpaka hapa nafikiri sijaelewa unachokitaka bado.

Najua huta kubaliana na mimi kwa sababu Tundu Lissu amesha kuingia akilini, lakini tactic ya Tundu Lissu lazima uikubali, hiyo haikuwa siasa. Yule jamaa anahitaji kwenda psychatric. That is an obsession na sio siasa. Msitudanganye hapa na kutufanya sisi watu tusio jua nini maana ya demokrasia.

Badala ya nyie kumwonya Tundu Lissu wenu eti mnamwonya Magufuli. Yule jamaa kafika sehemu na kumtangazia Rais wetu personal war. Nyie mna shangilia tu. Alitakiwa ajue kuwa yeye ni Rais na kama Rais ana stahili heshima yake. Kuna njia za kum attack president lakini sio hivyo. Ukumbi anao mkubwa bungeni wa kuikosoa serikali na sio kila kitu serikali inachofanya kumwattack Magufuli. Huyo ni mwenda wazimu.

Yeye ni nani kwanza mpaka kumwita Rais wetu dikteta uchwara, mjinga, mpumbavu na kadhalika. Ana wadhifa gani kwanza? Au kwa sababu yeye ni mbuge na mwana sheria mkuu wa wapinzani?

Asijivunie Masters yake ya sheria. Kuna watu wana PHDs za sheria na wamesoma kuliko yeye lakini wako kimya. Sio wajinga hawa na wanauelewa mkubwa sana wa sheria na siasa kuliko yeye. Yeye ana nini? Amesha enda kupambana na wanasheria wengine kwenye court za ulimwengu? Ana experiance gani zaidi ya kuwatambia na kuwapumbaza watanzania na Masters yake? Masters yake ina saidia nini kama hana hekima na respect kwa viongozi wetu?

Mwana sheria aliyesoma kweli na anajua principles za sheria za nchi kwa kufuata misingi ya kidemokrasia, hawezi behave mwenyewe kama yeye anavyo fanya kwa Rais wetu na mbele yetu. It is ridiculous! Lakini kwa vile sisi watanzania ni watu wa kushabikia na kushangilia kila jambo, tunaona sawa tu. Hiyo sio sawa. Lazima naye aheshimu peoples choyce! Sisi ndiyo tulio mchagua Magufuli na kumwona yeye anafaa kutuongoza na hatukumchagua yeye au Lowassa. Wajipange upya na wagombee tena 2020 katiba yetu ina sema hivyo na haija mzuia mtu. Kwanza yeye bado ni kijana na anaweza akagombea urais mpaka 2035 kulingana na umri wake kama sijakosea. Haraka ya nini?

Msidanganyike watanzania kama kuna nchi duniani ina ruhusa maandamano ya uchochezi, hiyo sahau. Hata Amerika kwenye hakuna kitu kama hicho. Wapinzani wameshindwa watulie na watafute njia nyingine. Sio kila kitu anachofanya Rais kwake sio. Yeye ana akili gani za kuwashinda watanzania milion 50 wote? Wo is he? Ni Yesu yeye?

Nawashangaa sana watanzanua wanao shabikia upuuzi wa Lissu. Huyo ni sadist.
 
Chadema wamebaki wapinzani wakuu wa maendeleo ya wananchi; wameacha misingi Yao ya awali.
 
Nina maanisha ivi ilituamini kuwa kunamaendeleo angeachia bunge live angalau wakati bajeti tuone kama wapo vizuri na mikutano ya siasa angalau kwa miezi 6 iwe wiki moja ndani yahiyo miezi 6 au kwa mwaka 1 iwe kunamwezi mmoja wa mwisho katika mwaka tungejuwa kunamafanikio au laa lakini hivi kusika mtu mmoja au chama kimoja sidhani kama inafaa kusema mafanikio sijui viva wakati kunatetesi za 1.5 hazijulikani zilipo unafikiri nipesa za mchezo hizo wewe unaita mafanikio viva
Nasikitika kukuambia ukweli kuwa hujui unacho kitaka na kama unajua basi aidha mmoja wetu hamwelewi mwenzie.

Sikiliza ndugu yangu, siasa haziwezi kupigwa kila siku. Kuna mda serikali iliyo pewa dhamana ya kutekeleza malengo na maadhimio ya chama cha siasa ambayo kimeyaweka kuiendeleza nchi, haina budi kikapewa nafasi hiyo ya kufanikisha malengo hayo. Sasa kama kila siku wana siasa wanapiga domo lini unadhani maadhimio na malengo hayo ya chama yatatekelezwa?

Wajibu wa vyama vya upinzani ni kukikosoa chama ambacho kimepewa dhamana ya kuunda serikali ambayo inatekeleza maazimio yake, pale inapo ona serikali hiyo inashindwa utekelezaji wa sera ya chama hicho kwa ufanisi mzuri kulingana na matarajio yaliyo wekwa majimboni mwao kwenye kampeni ya kupiga kura au uchaguzi. Sehenu nyingine ni Bungeni.

Mbowe na Zitto Kabwe ni viongozi wa vyama vyao vya kisiasa, CHADEMA na NCC Wazalendo. Wana wajibu wa kui-attack CCM kwa kuunda serikali ambayo haitekelezi wajibu wake kiufanisi majimboni na sio kuishambulia serikali kuu au watumishi wake hadharani kwa matusi na kejeli. Tuna enda wapi? Hawana mamlaka hayo kabisa kikatiba. Kama nimekosea basi wajuao zaidi wanijuze!

Wanaweza kuishambulia na kuilaumu serikali kwa utendaji wake mbovu wa kuleta maendeleo kwa wananchi Bungeni kwa vile wao ni wanachama wa Bunge. Huko ndiyo wapambane na serikali kupitia watendaji wake mawaziri na waziri mkuu na wabunge wengine wa viti maalumu.

Angalia Amerika toka Donald Trump ameapishwa kuwa kiongozi mkuu wa serikali umemsikia Hilari Clinton akimshambulia Rais Trump hadharani na kumwita yeye dikteta uchwara au mwenda wazimu kama akina Mbowe, Zitto Kabwe au Tundu Lissu wanavyo fanya kwa Magufuli? Rais kama Amiri Jeshi mkuu wa nchi ana mamlaka ya kutunga sheria per Decree bila kutumia katiba. Angeweza kumswaaga Tundu Lissu jela bila hata mahakama kwa kumdhalilisha Rais hadharani.

Yaani ni huruma tu ya Rais Magufuli, hawa watu kwa kufanya hivyo wana mdhalilisha kiongozi na Amri jeshi mkuu wa nchi! Walitakiwa wawekwe jela au kama kuna adhabu ya kifo basi wahukumiwe kwa kunyongwa.

Nchini yeyote ile Rais akisha apishwa tu basi sio mtu wa kuchezewa tena. Ni chama chake tu ndiyo chenye mamlaka ya kumwondoa madarakani kama ita thibitisha kuwa usalama wa nchi una hatarishwa. Lakini sio akina Mbowe au Tundu Lissu. Wao ni akina nani kwa rahisi wa nchi? They are nothing. Mbowe ni mbunge wa High Mimi mtu wa Nachingwea nahusika naye na nini? Sija mchagua na wala hatetei maslahi yetu Nachingwea. Kwa hiyo utaona kuwa kama mnachingwea "he is nobody" kwangu. Sembuse kwa Rais wa nchi? Tuache masihara pembeni!

Wao ni wawakilishi tu wa majimbo yao. Kazi yao kubwa ni kuiandama serikali Bungeni ili watu wao wapate kile ambacho kime wafanya wao wawachague. Lakini sio kumdhalilisha na kumtukana Rais wa nchi hadharani.
Mtu kama Tundu Lissu ashukuru Mungu sana. Kama mwana siasa wa chama na mbunge hathubutu kumdhihaki Rais wa nchi kwa kumwita yeye ni Dikteta uchwara hadharani. Alistahili kifo. Anajua lakini maana ya mtu kuitwa Rais?

Kwa hiyo ndugu yangu usipende kuchanganya mambo. Nakushauri kama vitu huvielewi vizuri ni bora unyamaze. Lakini sio kuleta uzushi wa mambo usiyo yajua.

Nenda kajipange upya kabla huja amua kumtetea au kumlaumu mtu au kiongozi kwa kiushabiki wa vyama.

Sisi wananchi tuna mamlaka ya kumpindua au kumwondoa Rais madarakani kwa kupitia kura zetu tu pale tunapo chagua chama kingine ambacho kita mteua mwakilishi wake wa kumnadi katika cheo cha urais kwa mujibu wa katiba. Soma katiba vizuri uielewe. Usipende kuimbaimba tu madude yasiyo eleweka. Cheo cha urais ni cheo kikubwa sana katika nchi na sio Tanzania tu bali duniani kwote.
 
Nasikitika kukuambia ukweli kuwa hujui unacho kitaka na kama unajua basi aidha mmoja wetu hamwelewi mwenzie.

Sikiliza ndugu yangu, siasa haziwezi kupigwa kila siku. Kuna mda serikali iliyo pewa dhamana ya kutekeleza malengo na maadhimio ya chama cha siasa ambayo kimeyaweka kuiendeleza nchi, haina budi kikapewa nafasi hiyo ya kufanikisha malengo hayo. Sasa kama kila siku wana siasa wanapiga domo lini unadhani maadhimio na malengo hayo ya chama yatatekelezwa?

Wajibu wa vyama vya upinzani ni kukikosoa chama ambacho kimepewa dhamana ya kuunda serikali ambayo inatekeleza maazimio yake, pale inapo ona serikali hiyo inashindwa utekelezaji wa sera ya chama hicho kwa ufanisi mzuri kulingana na matarajio yaliyo wekwa majimboni mwao kwenye kampeni ya kupiga kura au uchaguzi. Sehenu nyingine ni Bungeni.

Mbowe na Zitto Kabwe ni viongozi wa vyama vyao vya kisiasa, CHADEMA na NCC Wazalendo. Wana wajibu wa kui-attack CCM kwa kuunda serikali ambayo haitekelezi wajibu wake kiufanisi majimboni na sio kuishambulia serikali kuu au watumishi wake hadharani kwa matusi na kejeli. Tuna enda wapi? Hawana mamlaka hayo kabisa kikatiba. Kama nimekosea basi wajuao zaidi wanijuze!

Wanaweza kuishambulia na kuilaumu serikali kwa utendaji wake mbovu wa kuleta maendeleo kwa wananchi Bungeni kwa vile wao ni wanachama wa Bunge. Huko ndiyo wapambane na serikali kupitia watendaji wake mawaziri na waziri mkuu na wabunge wengine wa viti maalumu.

Angalia Amerika toka Donald Trump ameapishwa kuwa kiongozi mkuu wa serikali umemsikia Hilari Clinton akimshambulia Rais Trump hadharani na kumwita yeye dikteta uchwara au mwenda wazimu kama akina Mbowe, Zitto Kabwe au Tundu Lissu wanavyo fanya kwa Magufuli? Rais kama Amiri Jeshi mkuu wa nchi ana mamlaka ya kutunga sheria per Decree bila kutumia katiba. Angeweza kumswaaga Tundu Lissu jela bila hata mahakama kwa kumdhalilisha Rais hadharani.

Yaani ni huruma tu ya Rais Magufuli, hawa watu kwa kufanya hivyo wana mdhalilisha kiongozi na Amri jeshi mkuu wa nchi! Walitakiwa wawekwe jela au kama kuna adhabu ya kifo basi wahukumiwe kwa kunyongwa.

Nchini yeyote ile Rais akisha apishwa tu basi sio mtu wa kuchezewa tena. Ni chama chake tu ndiyo chenye mamlaka ya kumwondoa madarakani kama ita thibitisha kuwa usalama wa nchi una hatarishwa. Lakini sio akina Mbowe au Tundu Lissu. Wao ni akina nani kwa rahisi wa nchi? They are nothing. Mbowe ni mbunge wa High Mimi mtu wa Nachingwea nahusika naye na nini? Sija mchagua na wala hatetei maslahi yetu Nachingwea. Kwa hiyo utaona kuwa kama mnachingwea "he is nobody" kwangu. Sembuse kwa Rais wa nchi? Tuache masihara pembeni!

Wao ni wawakilishi tu wa majimbo yao. Kazi yao kubwa ni kuiandama serikali uBungeni ili watu wao wapate kile ambacho kime wafanya wao wawachague. Lakini sio kumdhalilisha na kumtukana Rais wa nchi hadharani.
Mtu kama Tundu Lissu ashukuru Mungu sana. Kama mwana siasa wa chama na mbunge hathubutu kumdhihaki Rais wa nchi kwa kumwita yeye ni Dikteta uchwara hadharani. Alistahili kifo. Anajua lakini maana ya mtu kuitwa Rais?

Kwa hiyo ndugu yangu usipende kuchanganya mambo. Nakushauri kama vitu huvielewi vizuri ni bora unyamaze. Lakini sio kuleta uzushi wa mambo usiyo yajua.

Nenda kajipange upya kabla huja amua kumtetea au kumlaumu mtu au kiongozi kwa kiushabiki wa vyama.

Sisi wananchi tuna mamlaka ya kumpindua au kumwondoa Rais madarakani kwa kupitia kura zetu tu pale tunapo chagua chama kingine ambacho kita mteua mwakilishi wake wa kumnadi katika cheo cha urais kwa mujibu wa katiba. Soma katiba vizuri uielewe. Usipende kuimbaimba tu madude yasiyo eleweka. Cheo cha urais ni cheo kikubwa sana katika nchi na sio Tanzania tu bali duniani kwote.
Huyu sijuwi umekula maharagi ya wapi au unasaka teuzi na atakae kuteuwa wewe sijui ninani hata huyo uliomtolea utetezi kakudharau 1 eti mboewe ni mbunge wahai hujui kitu mbowe nimbunge wa bunge la jamuhuri ya muungano wa tz nahuko nachingwea anahusika 2 sio chama husika au mwnanchi wanaoweza kumuajibisha rais Bali hata bunge linauwezo wakupiga kura yakutokuwa naimani nae sasa sijui unafahamu zito mbowe lisu niwabunge?3 yeye rais kasema siasa basi hadiwakati mungine hatamimi nilikubali hivyo lakini nilitegemea hata yeye ataacha siasa mpaka hapo baadae lakini yeye anatumia shughuli za serekali kufanya siasa au kunadi chama mfano sikosa yeye kutembelea mikoa wilaya na nk lakini kila anapo tekeleza wajibu wake utaona watu waliovalia sare za chama chao nawengine wanakwenda mbali zaidi wakisha vaa sare hizo ndio wanatoa matatizo yao akisikiliza matatizo nayeye utamsikia chama chake oyee sasa huu mkutano wachama au waserekali kumbuka pale anatumia pesa ya serekali kwani hata hivyo vyama vingine nao kunakodi yao imetumika kumsafirisha hapo pia kuna majimbo mengine walishinda upinzani na mbunge analazimika kuwepo katika ziara hiyo alafu unasikia lichama lake oyee 3 jifunze kuandika kitu kama kilivyo sio ncc wazalendo ni act wazalendo umeropoka sana nakuona hujui kitu
4 rais ninafasi kubwa sana kama ulivyo sema ukijiheshimu nawewe utaheshimiwa namaana hii Mimi nilitegemea mh rais kwakua amekataa siasa angepita nchini kama serekali tu lakini naona anatumia kodi ambayo ccm chadema act nccr tlp chauma cuf adc na nk pamoja wananchi wasio navyama wamelipa kufanyia kazi 2 yaani yaserekali na yachama chake oyee hii sio sawa hata kidogo nawaomba wanaomshauri watusaidie najuwa mh rais anaouwezo wakutumia ziara zake kiserekali bila kuingiza chama chake ndani shughuli hizo iwapo moyo wa uzalendo utamtuma kufanya hivyo.hata hivyo sijasikia ukielezea kuhusu 1.5 trn kama wewe umeridhishwa naupotevu huu nakuita maandeleo nakuomba basi zisemee hata kidoga tafadhali kuna kodi yako yangu na yawangine tujionee huruma sisi wenyewe tuungane tuombe ufafanuzi nihaki yetu
 

Mwanasiasa maarufu duniani Tundu Lissu leo atakuwa akihojiwa na mwanahabari nguli Africa Mzee Shaka Ssali kuhusu demokrasia ya Afrika.

Ssali anayeheshimika kuendesha vipindi makini vya Straight Talk Afrika anampa heshima Tundu Lissu kutokana na kukunwa na maono yake

Kipindi hiki kinaweza kurushwa saa 3:30 kupitia Star TV au Kiss Fm

======
VIDEO:



Nani anasema kuwa Lissu ni mwana siasa maarufu duniani? Ana maarufu gani? Labda wa kusema mambo ya uongo kuhusu Rais Magufuli na watanzania. Acha kelele mkuu.

Naomba utambue kuwa katika mazungumzo yake yote aliyo yafanya mpaka sasa imebainika kuwa Lissu hajui taaluma yake na wala hajui maana ya haki za binadam ni nini. Nikupe ufafanuzi kidogo wa haki za binadam na Freedom of speech.

Kitu kikubwa katika haki za binadam kwanza ni upendo kwa binadam wenzako. Huu mwenendo Lissu wako hana. Lissu anachuki kubwa na binadam wenzake hasa na Rais wetu Magufuli. Lissu hawapendi binadama wenzake na wala hawaoni kama binadam wenzake wana thamani kwake. Kama yeye angekuwa kweli anathamini haki za binadam kama anavyo dai asinge zurura duniani kwote kuwaomba mabeberu na vibaraka wake eti wasitupe sisi misaada wala mikopo, anacho taka yeye ni kuona watanzania wanateseka kishenzi na kufa kwa kukosa misaada na mikopo maadam yeye anamwona Magufuli anaingia mtelu na kuondoka Madarakani. Kwa hali hii ya kutaka watanzania wakiwemo kaka zake, shangazi zake na ndugu zake wengine wateketee kwa shida, peke yake amesha vunja miiko ya haki za binadam. Utaliliaje haki za binadam wakati yeye mwenyewe hawezi kinda hizo haki? Wewe utawezaje waombea binadam wenzako aasulubiwe na wafe? Na atathibitisha vipi kuwa yeye anafuata maadili ya haki za binadam wakati hana upendo na binadam? Kwa hayo namwomba asije hapa na kauli kama hizo. He has no credit for that at all.

Kuhusu Freedom of speech nayo ni hivyo hivyo uozo mtupu. Freedom of speech haimaanishi mtu kufanya defamit. Kila akitoa kauli ni matusi tu na defamation kwa Rais wetu ambaye amechaguliwa na wengi na ambaye wengi wanampenda na kumwamini. Katika Freedom of speech yeye anataka nini? Mbona kila mmoja anasema anavyo taka? Na kuna magazeti na mitandao ya kila aina?

Ukiangalia maswala ya demokrasia pia nayo yanamsuta. Aanze kwanza kupigania demokrasia katika chama chake kabla hajaja na madai ya udemokradia wa nchi. Tanzania imefanya uchaguzi 2015 na wengi wamemchagua Magufuli kuwa Rais wetu, sasa yeye anampinga kwa kesi gani? Yaani kuwaambia wapinzani wasiandamane hovyo hovyo na kuweka vikao hadharani ndiyo kosa la kutaka Magufuli aondolewe madarakani? Yeye ni nani kwanza na wako wangapi wakati wengi wetu tunampenda? Sisi wengi wetu hatuoni shida kuzuia maandamano. Kweli maandamano Sana saidia nani? Na kwa msingi ipi? Hakuna serikali duniani ambayo itakubali maandamano yasiyo na tija kwa wananchi. Waspain walitumia polisi wao kuwa vuruga wakatalonia ambao walitaka kujitenga. Wafaransa hivi juzi juzi tu polisi wao wamewapiga vibaya waandamanaji na wengine wako rumande. Mambo kama haya mbona hayako Tanzania? Hivi huyu anataka nini?

Mtu atakaye mchukia Magufuli ni mtu ambaye ni mwenda wazimu na mchumia tumbo lake. Tundu Lissu ni mmoja wapo wa watu wanaotaka kuchumia matumbo yao. Huwezi ukadai Rais aondolewe kwa kuzuia maandamano ya kisiasa kila wakati. Freedom of speech Tanzania iko na serikali yetu inajali haki za binadam pia. Na Rais anaye jali haki za binadam wenzake ni yule anaye pigana usiku na mchana kutafuta njia za kutatua matatizo yanayo wakabili wanachi na nchi yake kwa ujumla.

Mtu aliyetakiwa kulalamika mitaani kama Rais angekuwa mbaya kweli, kama yeye anavyo dai, ni sisi wananchi ambao hatuna uwezo wa kulisemea hilo Bungeni. Lakini yeye kama mbunge angepeleka mswada Bungeni wa kutaka Rais aondolewe madarakani kwa vitendo vyake viovu kama vingebainika vipo. Na kama majority ya wabunge wangekataa hiyo ndiyo demokrasia. Sasa yeye anaitaka demokrasia gani? Na haki gani za binadam?

Anatoa mambo ya uongo ambayo hayako. Hivyo yeye anafikiri nini? Mwana sheria gani anakuwa na ukaidi kama mtoto mdogo? Mwana sheria wa miembeni labda. Yaani kama Masters ya Law ndiyo inamfanya awe na kichwa ngumu na kutoa waheshimu hata watu walio pigania uhuru wetu?

Kwa matendo yake Tundu Lissu naona hana sifa hata moja kuwa kiongozi wa nchi. Hata familia yake hawezi kuiongoza. Sioni kama anamifano mizuri kwa familia yake. Anatoa mifano gani kwa watoto wake wakati wanasikia na kushuhudia baba yao kila wakati na kila tamko analolitoa ni la kumtukana na kumkejeli mkuu wa nchi. Anategemea kweli watoto wake watakuwa na heshima kwa viongozi wao wa baadae?

Natamani Mwalim Nyerere angekuwa bado Rais angemwonyesha. Rais Magufuli ni mwema sana na anapenda sana watu. Kama asingekuwa mpole sijui ingekuwaje kwa kwa Lissu?
 
Back
Top Bottom