Ngoja nikusaidie kidogo, mengine utaongezea.
Taasisi imara zinajengwa na Katiba ya wananchi. Katiba ya wananchi ni ile yenye kuwapa wananchi mamlaka kamili. Yaani kwa Katiba ya aina hiyo, viongozi wanakuwa kweli viongozi na siyo watawala. Katiba hiyo itawapa wananchi mamlaka ya kumwondoa kiongozi yeyote wakati wowote ule kwa utaratibu wa referendum, ambapo mwananchi au kikundi cha wananchi a/kinaweza kuanzisha mchakato huo wa kumwondoa kiongozi husika kwa kukusanya sahihi kadhaa za wananchi walio eligible kuchagua kiongozi.
Pili, hili litafanikiwa zaidi kwa uwepo wa local governments zenye mamlaka kamili ya kiutawala na kifedha, haswa kwenye kutunga sheria za kodi na kukusanya kodi. Nchi yetu ni kubwa mno. Huu mfumo wa sasa ulio centralised ni wa kizamani. Mfumo huo unatengeneza sana mianya ya rushwa, uzembe, inefficiencies n.k. Katika jambo kubwa ambalo nawaunga mono CHADEMA ni ili la serikali za majimbo. Kwa uwep wa centralised state, Magufuli hata afanye nini uzembe, rushwa na kutowajibika kwa viongozi hukuwezi kuisha. Sana sana atakavyozidi kubana, watakaothirika ni wananchi walioko kwenye local governments.
Kwa kuwapa wananchi mamlaka kamili kupitia mfumo wa serikali huru na kamili za majimbo, wananchi wataweza kuwawajibisha viongozi na serikali zao za majimbo.
Kuna nchi nyingi tu duniani zinatumia mfumo wa kitaasisi niliousema hapo juu. Je, Magufuli yupo tayari kwa hili? Sidhani. Kwa kuwa kwa ilivyo sasa, Magufuli hana legitimacy ya kupambana na rushwa na upigaji, ilhali naye ni mla rushwa na mpigaji. Bila ya mfumo nilioulezea, watu wa serikalini wataendelea kumchora tu, huku wakuendelea na upigaji kama kawaida, kwani wananchi hawawezi kuwafanya lolote.