Lissu is too shallow compared to Prof Kabudi

Lissu is too shallow compared to Prof Kabudi

britanicca,nimefanya kazi na Prof Kabudi kwa vipindi viwili tofauti na sehemu mbili tofauti.
Yeye ni sawa na Prof. P. Limumba, "tongue twister".
Mh. T. Lissu sijapata bajati ya kufanya naye kazi au kuwa karibu naye zaidi ya kumfahamu kupitia kaka yangu waliyesoma naye na harakati zake tangu enzi hizo za 1990's.
Naomba uniambie wewe na wengine wote hapa jukwaani,ni nani aliyekuwa anatetea rasilimali za Taifa kabla ya mwingine!?
Naomba niambie,ni nani kati ya Mh. T. Lissu na Kabudi ameweka rehani uhai wake na wa kizazi chake kwa kutetea ukweli katika tasnia yao ya sheria?
Naomba utoe ushahidi wa "kimatokeo" wa jambo ambalo kila mmoja alilisimamia kisheria hadharani na akafanikiwa ama bado anaendelea nalo na msimamo wake ule ule wa awali kuhusu kambo hilo.
Ukiweza kunijibu hayo,utaniaminisha kuwa wewe si tu ni "msemakweli", bali pia ni "iwee originali" .
Tafadhali.
Hawezi kukujibu hapo. Subiri sana labda mwingine !!
 
Ahaaa haaa haaa
lisu ni mtupu SANA. wengi kwa sababu ya upeo wao mdogo, HAWAKAZII FIKIRA ZAO ANACHOSEMA BALI WANAANGALIA JINSI ANAVYOSEMA.

yeye tundu lisu hata ukimuuliza wewe ni NANI, atakavyojibu kwa gesture hiyo mpaka utashangaa. hata salamu ni vivyo hivyo.
 
Ahaaa haaa haaa
lisu ni mtupu SANA. wengi kwa sababu ya upeo wao mdogo, HAWAKAZII FIKIRA ZAO ANACHOSEMA BALI WANAANGALIA JINSI ANAVYOSEMA.

yeye tundu lisu hata ukimuuliza wewe ni NANI, atakavyojibu kwa gesture hiyo mpaka utashangaa. hata salamu ni vivyo hivyo.
Aisee wewe ni NDEZI!!


Usimwambie MTU.
 
Kabuti hajawahi hata kupigwa manati anajuwa nini. Noah kwa kila Mtz naskia imebadilika kuwa Balimi 7
 
Ni kweli kabisa Lissu thinking yake ni too shallow!!

1. Sijui Tundu Lissu alitaka Raisi mamlaka yake hayo ya kutunga sheria ayapate wapi kama si kwa kupitia Katiba?

2. Mamlaka ya mihimili yote yanapatikana kupitia Katiba. Hata hayo mamlaka ya muhimili wa bunge ya kupitisha misuada ya sheria yanatokana na Katiba.

3. Yaani Tundu Lissu anataka kuwadanganya wananchi kwamba bunge peke yake linaweza kutunga sheria. Kazi ya muhimili wa bunge ni kupitisha misuada ya sheria iliyoandaliwa (usually) na muhimili wa serikali (executive under the president). Misuada hiyo ikishapitishwa na bunge (kwa kusomwa mara ya tatu) inabaki kuwa misuada na hurudishwa kwa Rais. Rais akiridhia na kuweka saini yake ndipo misuada hiyo hugeuka kuwa sheria. Rais asiporidhia misuada hiyo haiwezi kuwa sheria, na hutupwa kapuni. Sasa kwa mwenye akili timamu anaweza kweli kusema kwamba Rais hana mamlaka katika kutunga sheria?

4. On top of all that, Katiba pia imempa Rais mamlaka ya kutoa tamko (decree) ambalo likichapishwa kwenye gazeti la serikali linakuwa sheria moja kwa moja, yaani bila kupitia utaratibu wa kupeleka musuada kwenye bunge. Halafu mtu kama Tundu Lissu, huku akichechemea hospitalini, anasema eti Rais hana mamlaka yo yote kwenye kutunga sheria! Indeed it is very flabagasting.
 
wote walewale tu japo prof. Kabudi ananafuu kidogo, anachokera ni kuleta u'lejendali kwenye mambo ya msingi, kuwapoteza watu mpaka wanasahau topic.
 
Lisu ni Nabii wa Afrika nzima!
Ninapomuona Lisu najivunia kuwa kumbe bado Afrika ina watu wanaoweza kupigania Uhuru wao bila kujali nguvu kubwa za Wakoloni weusi.

Namuheshimu mtu anayesimama katikati ya Magereza ,Mahabusu za Polisi ,figisu za Uhamiaji, mabomu na vifaru ,Ukatili na amri za magavana wa Mikoa na wilaya wa Leo. Figisu na kufukuzwa Bungeni, Kuandama na vitisho kila kukicha ,nguvu ya chama dola, ubinafsi na uroho na ulevi wa madaraka wa wakoloni weusi na kutetea msimamo wake kwa nguvu zote.

Wakati mwingine walioshiba na kuninginiza tai zao wanaona watu kama akina Lisu kama watu wapiga kelele tu wasio na maana kwa sababu wao wamezungukwa na nguvu kubwa ya dola.

Kuitetea Serikali na kuipigania ni rahisi sana sana.Ni sawa na Mchunga kondoo anapomwona Fisi ameingia zizini na kisha kutimua mbio kwa woga huku kondoo wakiwa hawana mtetezi kwa sababu ya kumwogopa Fisi.

Mchungaji anayejua kazi yake ni yule jasiri anayeweza kuwatetea kondoo wake bila kujali ukali wa Fisi.
Lakini mwoga anakimbia na kumwacha Fisi ararue kondoo wake.

Serikali yeyote yenye watawala badala ya viongozi wa watu haina tofauti na Serikali nyingine yoyote ya Kikoloni tofauti ni rangi tu za watawala.
Kusimama na Serikali ni rahisi sana kwa kuwa Hazina ya fedha ,benki kuu na kila cheo chenye heshima na maslahi kiko mikononi mwa Serikali. Tumeona wakuu wa Wilaya wakivunja sheria na katiba wazi kabisa lakini huyo Mtu anayesifiwa kuwa ni mtaalam wa sheria hajawahi kusema anaona ni sawa tu. Haoni kuwa wanaotendewa dhulma na uonevu ni binadamu kama yeye. Hajui kuwa Mungu anapenda haki itamalaki kwenye ardhi. Mungu alimuumba binadamu kwa heshima kubwa sana. Kwa hiyo kitu cha kwanza duniani ni heshima ya binadamu na utu wake sio daraja wala vyombo vya usafiri. Hivyo vyote ni kazi ya mikono ya binadamu.
Ukiona mtu anatetea haki,utu ,heshima na Uhuru wa Binadamu huyo ndiye mchamungu na hakika thawabu yake ni kubwa.

Huyo mtu wetu kumlinganisha na Lisu ni makosa makubwa sana mana ni watu wawili tofauti kabisa kifikra na kimtizamo . Mmoja anaongea kile anachokiamini (Lisu) hata kama watawala watapinga na hawataki kusikia mawazo yake. Na huyo mwingine anaongea kile kinachoaminiwa na watawala. Kile anachokiamini yupo tayari kukikana saa yoyote ili aweze kuboresha maisha yake kwa kupata vye kirahisi . Wasomi wengi wa Afrika hasa wenye madigrii mengi wamekaa darasani kwa lengo moja tu kupata mishahara inayokidhi maisha yao. Sio zaidi ya hapo. Mtu akihangaika kupiga shule na maresearch mengi usifikiri kuna changamoto anataka kuitatua au kuna ugunduzi wowote anataka kuufanya LA hasha ,anataka mshahara wake upande. Ndio maana wanasiasa wakimpa mshahara mkubwa basi ataweka pembeni Fikra zake na utaalam wake na kuanza kutumia fikra za watu wengine.

Kuwa na uwezo wa kusema na kusimamia kile mtu anachoamin kama Lisu inahitaji uwezo wa Mungu na kujitoa sana.
Bahati mbaya kwa ubinafsi na chuki za waafrika tunashindwa kumtumia tunatumia wasaka tonge ambao wanatuangusha siku zote.
Lisu anathawabu kubwa sana hata mbele za Mungu.
Lisu ni kati ya watu ambao baadae watakapoondoka duniani itabidi atangazwe kuwa mwenye heri.
 
Kama unaongelea sheria mwanasheria mzuri unampima mahakamani sio katika majukwaa ya siasa,upo ushaidi wa kutosha wa kazi za Lissu akiwa mahakamani,unafahamu kwa nini mara zote hata wanaomkamata hawapendi kumpeleka huko sababu wanaijua shida yake,yeye anapapenda sana huko na ni mwanasheria bora sana akiwa huko.Tuwekee kazi za Kabudi tufanya ulinganisho sahihi zaidi ya hapo ni porojo na uelewa finyu
 
Propesa Kabugi hajui sheria, hajawahi kusimama mahakama kuu kuargue mijadala ya sheria na kushinda shauri

Kabugi anajua tu Historia ya mambo machache machache ikiwemo Historia ya Sheria.

Kabugi alitwambia wakati wa mchakato wa katiba kuwa Raisi wa JMT hana mamlaka hata ya Kuyoa Ushauri kwa Serikali ya SMZ, Lakini baada ya kupewa ulaji kabadiri mtizamo na kudai raisi wa JMT ana power hata za kuwaagiza mawaziri wa SMZ. Angekuwa anajua sheria angesema lililonyooka kisheria

Propesa Kabugi anadai hakuna haja ya likitabu liitwalo katiba, bali katiba halisi ni mila na desturi za watu katika nchi, na akadai Waingereza walituandikia katiba kwa sababu waliamini sisi wenyewe kwa wenyewe hatujiwezi kujisimamia mambo yetu bila rejea ya kwenye kitabu!. Lakini hakusema nchi kama Marekani, Uchina, Japan zina katiba ya maandishi je vipi hao hawawezi kujisimamia?. Je aliposhiriki kwenye tume ya katiba mbona waliiweka rasimu katika maandishi?

Kabugi akadai Barick wamekubali kutupa Share 50% plus kuendelea kulipa kodi mbalimbali, kitu ambacho hakimake sense hata kwa watoto wa form one

Kwa kweli sijawahi kuona Propesa anayebugi kama propesa Kabugi

Mleta mada, next time tofautisha kati ya uwezo wa kukremu darasani ukapata ma GPA makubwa na uwezo halisi wa kuanalyse kuchambua na kuona mambo kwa kina!. Naamini humo kwenye familia yenu kuna watu hawajakanyaga shule lakini uwezo wao wa kiakili unaukubali kuwa hawa watu ni Magenius!

Sasa Lissu ni genius, laiti angeamua kuwa bundi kusomasoma, angekuwa Profesa tangu akiwa na miaka 30 hivo!
 
Ni kweli kabisa Lissu thinking yake ni too shallow!!

1. Sijui Tundu Lissu alitaka Raisi mamlaka yake hayo ya kutunga sheria ayapate wapi kama si kwa kupitia Katiba?

2. Mamlaka ya mihimili yote yanapatikana kupitia Katiba. Hata hayo mamlaka ya muhimili wa bunge ya kupitisha misuada ya sheria yanatokana na Katiba.

3. Yaani Tundu Lissu anataka kuwadanganya wananchi kwamba bunge peke yake linaweza kutunga sheria. Kazi ya muhimili wa bunge ni kupitisha misuada ya sheria iliyoandaliwa (usually) na muhimili wa serikali (executive under the president). Misuada hiyo ikishapitishwa na bunge (kwa kusomwa mara ya tatu) inabaki kuwa misuada na hurudishwa kwa Rais. Rais akiridhia na kuweka saini yake ndipo misuada hiyo hugeuka kuwa sheria. Rais asiporidhia misuada hiyo haiwezi kuwa sheria, na hutupwa kapuni. Sasa kwa mwenye akili timamu anaweza kweli kusema kwamba Rais hana mamlaka katika kutunga sheria?

4. On top of all that, Katiba pia imempa Rais mamlaka ya kutoa tamko (decree) ambalo likichapishwa kwenye gazeti la serikali linakuwa sheria moja kwa moja, yaani bila kupitia utaratibu wa kupeleka musuada kwenye bunge. Halafu mtu kama Tundu Lissu, huku akichechemea hospitalini, anasema eti Rais hana mamlaka yo yote kwenye kutunga sheria! Indeed it is very flabagasting.
Usiwe unakimbilia kuchangia kama hujaelewa vizuri.
Tundu Lissu amechambua vizuri ni kipindi gani rahisi anaweza kutumia nafasi yake kuweka sheria. Sio wakati wowote eti raisi anaweza kutumia hiyo nguvu yake kuna mazingira na wakati maarumu ndio raisi anaweza kufanya hivyo. Ni rahisi tu kuelewa yaani ni kama kusoma a, e, i, o, u.
 
Back
Top Bottom