Lissu is too shallow compared to Prof Kabudi

Lissu is too shallow compared to Prof Kabudi

Wasioelewa watakushukia kwa maneno ya kipumbavu lakini ukweli ndo huo. Lissu hana anachojua zaidi ya kubwabwaja. Ni kati ya wanasheria wa hivyo kuwahi kutokea. Hata bwana mdogo Albert Msando anamtoa kwente reli. Ajitathmini aone kuwa nje ya ulingo wa siasa anacho kitu anaweza kufanya ? He is a bare headed mind in the darkest of ghost.
haa haa hii inaitwa mahaba niue mkuu. mambo ya sheria waachie wenyewe.
 
Kizazi cha wadogo zetu ni kizazi ambacho hakijui substance ya maana ni ipi. Mtanzania kuiteka akili yake ni jambo dogo sana.

Unashangaa kusikia eti wachekeshaji na wao wanafungua makanisa na bado wanapata vichwa vingi tu.

Kabudi yupo juu sana, nimeiangalia hii clip ya bunge la sasa, jamaa anamwaga shule, kama vile mwalimu anaongea na wanafunzi.

Lissu ana tatizo la kushindwa kuitawala arrogance yake, hachelewi kuanza kupayuka, na hawezi kudhibiti hisia zake.
Sasa mbona alidanganya na kutuhaminisha matrilioni bila kuchambua jinsi kina Ossoro walivyodanganya. Yaani wewe utoto unakisumbua kuangukia tambo za Kabudi. Kabudi kila anapopata nafasi anatamba na kudhani kina Msukuma na Lakairo watamuelewa. Wanaomuelewa wengi wako mle kupiga makofi
 
Lissu ni mropokaji na mpiga kelele tu hajui lolote kinacho mbeba ni kwamba wananchi wanahamu kubwa ya mabadiliko ya kiuchumi na kiutawala.
Yaan jina linaanza na Prof utalinganisha na huyo anayeanza na blank??? Yaan wachagadema wapuuzi
 
Mkuu britanicca , with due respect, hukuwa na haja ya kuanzisha mada hii hapa JF hata kama ni muanzishaji mzuri na mkongwe wa mada-hata zile zinazokinzana. Hakuna mahali popote ambapo kuna mabishano kuwa ni nani kati ya Prof. Kabudi na Lissu yuko 'vizuri' kuliko mwenzake. Hao ni wanasiasa na wanajibizana kisiasa. Hakika, huna hoja wala hukuwa na haja ya kuanzisha mada hii ambayo inaweza kuishia kumtweza mmoja wa hao. Kama huna hoja, si lazima uanzishe mada. Muda mwingine soma za wenzako!
Tukubali hapa ni jukwaaa la siasa. Kwa ukongwe wako utagundua kwamba baadhi ya wana JF ukiwauliza wanaamini Lissu ni mtume wa ufahamu. Tufikie hatua tuwaokoe wanaolilia kila leo juu ya ufahamu wa Lissu. Vijana wetu wengi ufahamu ni mdogo na ndo maana unasikia ushabiki ukihama kumfuata mpiga kelele, siyo mwenye ufahamu. Wanamuelewa haraka Lissu na Mange kuliko Marando au Kijo au mwanaharakati yeyote anayetetea mambo ya maisha yao. Hili ni tatizo ktk media zote, hadi huko redioni na TV.

Ukiwasikiliza wahabarishaji ktk vyombo vyao ni aibu tu! Mtu anajadili kwa sura ya kutojua kabisa dunia inavyokwenda na akitoka hapo anaishia kuangalia mechi za ulaya hadi kesho. Je, umejiuliza kwa nini wanamshabikia Lissu kwenye mambo ya uchummi wakati hajui lolote.
 
Naanza kwa kukubali title yangu ndiyo, kabudi ni level nyingine kwa kina Lissu na mdee,

Najua nitapigiwa kelele baada ya uzi huu wengine watasema umetumwa, wengine watasema heshima yako inashuka no sina heshima hapa, nipo kuwasilisha mawazo yangu,

Kwa uwezo wa kabudi wa uwasilishaji wa mazungumzo na mijadala huwezi kumlinganisha Lissu hata siku moja,
Lissu uonekana anajua sheria kwa wasioelewa,

Kwa kifupi lissu hupiga kelele kwa kutaja vifungu n.a. watu wanashangilia bila kujua,

Kwa ufupi nimefuatilia hata baadhi ya hoja za kibatala nikaona Lissu uanasheria wake anacheza na jukwaa tu,
Hajafika hata level za kina Marando, au Advocate Mukono, ila kwakuwa hawana platform ya kuonekana watu hawagundui

Angalia presentation style ya kabudi na relevance ya anachokisema kutokana na sheria, mwangalie LIssu presentation na relevance ya anachoongea, kwa kifupi Lissu sheria yake haijafika level hizo mnapomuweka,

Akiacha kuongea kwa kupiga kelele akiwa ametulia atakuwa mwanasheria mzuri , bado Ana nafasi afanye mazoezi
Sijawahi kumpenda Lissu katika kujenga hoja na kuelewa mambo, naona kinachotokea kuhusu mtu kama Lissu ni ile kanuni ya kukiwa hakuna kitu (vacuum) binadamu tutaunda cha kuziba pengo hata kama hakina sifa stahiki. Prof Kabudi anaonekana mwelewa wa mambo na mzuri kwenye presentation. Ingawa simjui kwa ukaribu lakini sitashangaa kujua kuwa he is weak in character. Na hiyo inaonekana sasa katika kulinda tumbo lake hata ikibidi kupotosha au kupindisha kanuni. The guy is a blatant opportunist hiyo inamshusha chini kabisa.
 
Tukubali hapa ni jukwaaa la siasa. Kwa ukongwe wako utagundua kwamba baadhi ya wana JF ukiwauliza wanaamini Lissu ni mtume wa ufahamu. Tufikie hatua tuwaokoe wanaolilia kila leo juu ya ufahamu wa Lissu. Vijana wetu wengi ufahamu ni mdogo na ndo maana unasikia ushabiki ukihama kumfuata mpiga kelele, siyo mwenye ufahamu. Wanamuelewa haraka Lissu na Mange kuliko Marando au Kijo au mwanaharakati yeyote anayetetea mambo ya maisha yao. Hili ni tatizo ktk media zote, hadi huko redioni na TV.

Ukiwasikiliza wahabarishaji ktk vyombo vyao ni aibu tu! Mtu anajadili kwa sura ya kutojua kabisa dunia inavyokwenda na akitoka hapo anaishia kuangalia mechi za ulaya hadi kesho. Je, umejiuliza kwa nini wanamshabikia Lissu kwenye mambo ya uchummi wakati hajui lolote.
Kabisa umeeleza vema
 
Mkuu britanicca , with due respect, hukuwa na haja ya kuanzisha mada hii hapa JF hata kama ni muanzishaji mzuri na mkongwe wa mada-hata zile zinazokinzana. Hakuna mahali popote ambapo kuna mabishano kuwa ni nani kati ya Prof. Kabudi na Lissu yuko 'vizuri' kuliko mwenzake. Hao ni wanasiasa na wanajibizana kisiasa. Hakika, huna hoja wala hukuwa na haja ya kuanzisha mada hii ambayo inaweza kuishia kumtweza mmoja wa hao. Kama huna hoja, si lazima uanzishe mada. Muda mwingine soma za wenzako!
Hahaaa, Imekutachi kwa kuwa imemdemote lissu unayedhani kuwa yuko juu ya everybody!
Ni mada zipi unadhani zinastahili kuanzishwa hapa jukwaani? Zinazoendana na matashi ya maoni yako? Mi nilidhani jukwaa hili linatupa uhuru wa kujitusha kila mtu kwa kadri ya uwezo na upendo wake, ilimradi havunji sheria na taratibu?
Tulindeni demokrasia yetu.
 
Mkuu britanicca , with due respect, hukuwa na haja ya kuanzisha mada hii hapa JF hata kama ni muanzishaji mzuri na mkongwe wa mada-hata zile zinazokinzana. Hakuna mahali popote ambapo kuna mabishano kuwa ni nani kati ya Prof. Kabudi na Lissu yuko 'vizuri' kuliko mwenzake. Hao ni wanasiasa na wanajibizana kisiasa. Hakika, huna hoja wala hukuwa na haja ya kuanzisha mada hii ambayo inaweza kuishia kumtweza mmoja wa hao. Kama huna hoja, si lazima uanzishe mada. Muda mwingine soma za wenzako!
Kaka una hekima sana. Sijui kama atakuelewa. Hoja nyingine sijui hata lengo lake
 
Correct! They are all megalomaniac. LIssu haamini kama kuna mwingine, hajui kama nchi haihitaji sheria tu, kuna mengine ya muhimu kuliko sheria. Kila kitu anaamini ni yeye anayejua na akiona sifa zinakwenda kwa mwingine atazua jambo. Sifa anazitafuta hadi kitanda cha hospitali.

Kabudi naye ni balaa hilo hilo. Anahangaika kunyamazisha watu kwa mambo yasiyohusiana na mijadala. Anataka wabunge wote wawe wanafunzi wa sheria wakati yeye hataki kujifunza taaluma za wengine. Nahisi anatamani wabunge wote wawe wanasheria. Ukimuangalia usoni haoneshi kama anaamini kuna wanasheria wengine wanaomfikia. Nimeona akitishia kusema marks za wanasheria lakini hajaomba majibu ya magonjwa yake hospitalini!
Atleast tunaongea lugha moja mzee yule anakwambia ni 4.8 GPA
 
Kabudi hua haelezi kile anachoulizwa bali hua anaeleza kile anachokijua yeye mwisho wa siku anakuja kuongea vitu mpaka unashangaa rejea mambo ya kuwaambia wabunge wakasome legal anthropology, mara sijui ooh we were in the times when president was president..nigga who asked about all that stick to the point...
Chuki zako haziondoi ukweli kwamba Lisu ni bogus.
 
Mwambie atengeneze namna nzuri ya kuwasilisha maoni yake si kwa kuifokea na kui-command serikali...

Ataendelea kuwa ignored ingawa tunatambua anayo mazuri ya kusaidia nchi.

Mnam-ignore halafu nchi inashtakiwa?
 
Mkuu britanicca , with due respect, hukuwa na haja ya kuanzisha mada hii hapa JF hata kama ni muanzishaji mzuri na mkongwe wa mada-hata zile zinazokinzana. Hakuna mahali popote ambapo kuna mabishano kuwa ni nani kati ya Prof. Kabudi na Lissu yuko 'vizuri' kuliko mwenzake. Hao ni wanasiasa na wanajibizana kisiasa. Hakika, huna hoja wala hukuwa na haja ya kuanzisha mada hii ambayo inaweza kuishia kumtweza mmoja wa hao. Kama huna hoja, si lazima uanzishe mada. Muda mwingine soma za wenzako!
Umeongea taratibu na vema sana mkuu Petro E. Mselewa sidhani kama kuna mahali utakuta mjadala "serious" juu ya nani ni nani kati ya hawa. Sikumbuki hata wao kuleta hoja ili kumtweza mwingine, mara zote hushindana na kurekebishana kwa vifungu katika kada yao. Asante
 
Ingekuwa hivyo wala serikali ya ccm isinge mpiga risasi maana hakuna utawala uliojaza wasomi kwenye wizara kama huu wa awamu ya tano,wangemkabiri kwa hoja tu wakamtuliza
 
Ingekuwa hivyo wala serikali ya ccm isinge mpiga risasi maana hakuna utawala uliojaza wasomi kwenye wizara kama huu wa awamu ya tano,wangemkabiri kwa hoja tu wakamtuliza
 
Prof.Kabudi ni muongeaji mzuri, Lisu ni mchambuaji mzuri... wote sheria wanaijua...

Ila Chenge mbona hatiagi maneno...


Cc: mahondaw
 
britanicca,nimefanya kazi na Prof Kabudi kwa vipindi viwili tofauti na sehemu mbili tofauti.
Yeye ni sawa na Prof. P. Limumba, "tongue twister".
Mh. T. Lissu sijapata bajati ya kufanya naye kazi au kuwa karibu naye zaidi ya kumfahamu kupitia kaka yangu waliyesoma naye na harakati zake tangu enzi hizo za 1990's.
Naomba uniambie wewe na wengine wote hapa jukwaani,ni nani aliyekuwa anatetea rasilimali za Taifa kabla ya mwingine!?
Naomba niambie,ni nani kati ya Mh. T. Lissu na Kabudi ameweka rehani uhai wake na wa kizazi chake kwa kutetea ukweli katika tasnia yao ya sheria?
Naomba utoe ushahidi wa "kimatokeo" wa jambo ambalo kila mmoja alilisimamia kisheria hadharani na akafanikiwa ama bado anaendelea nalo na msimamo wake ule ule wa awali kuhusu kambo hilo.
Ukiweza kunijibu hayo,utaniaminisha kuwa wewe si tu ni "msemakweli", bali pia ni "iwee originali" .
Tafadhali.
 
Back
Top Bottom