The Palm Tree
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 7,950
- 12,549
Tundu Lissu akiwa Alabama nchini USA wakati anazungumza na watanzania waishio huko ,ameulizwa swali kama Freeman Mbowe alihusika kwa namna moja au nyingine kutokana na kupigwa risasi kwake, akawajibu hata yeye hajui huenda alihusika kweli!.
Lissu ametaka uchunguzi huru wa kuwachunguza Mbowe, Makonda ,Magufuli kama wamehusika kwenye tukio lake la kupigwa risasi.
My take:
Kitendo cha Lissu kutaka hata Mbowe achunguzwe kitakuwa mwiba mchungu kwa BAVICHA wanaopenda kumkingia kifua Mbowe ,huku wakimtaka Lisu agombee urais wa Tanzania.
Kama kweli Mbowe atachunguzwa kama Lisu anavyotaka ,basi huenda yakaibuka mengi na hata hatima ya mauaji ya Chacha Wangwe ambayo Mbowe amekuwa akihusishwa bila uchunguzi kwa miaka mingi sasa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Yeyote mnayedhani anahusika achunguzwe tu....
Yeah, inawezekana Mbowe ndiye aliyetoa amri walinzi wote siku ile na saa ile ya shambulizi waondolewe...!!
Yeah, inawezekana Mbowe ndiye aliyetoa amri CCTV cameras zing'olewe immediately baada ya shambulizi.....!!
Yeah, inawezekana Mbowe ndiye aliyetaka Tundu Lissu apelekwe Muhimbili National Referral Hospital badala ya Nairobi usiku ule wa trh 7/9/2017 ili kuokoa uhai wake....!!
Hata Paul Makonda a.k.a Daudi Albert Bashite, Cyprian Musiba, Jerry Muro, Dr Tulia Ackson, Medard Kalemani na kila anayehisiwa akiwemo Jiwe a.k.a Magufuli (JPM) mwenyewe na ukiwemo wewe uhojiwe tu.....
Kwani kuna shida gani bhana?? Si ndiyo uchunguzi wenyewe bwana maana kama huhusiki, kwa upelelezi huo utagundulika tu!!
