Siyo kejeli, tufanye kweli . Tukishindwa chini ya uongozi mpya tujue ndiyo basi tena. Mkoloni mweusi ataendelea kutugandamiza.
Tulibadilisha safu ya uongozi ili uweze (ku mobilize) kukusanya umma kufikia malengo tuliyogombea tangu 1992 tupate matokeo tofauti na yale uongozi uliopita ulipofikia.
Tusiposimama kidete kuonesha hii ni CHADEMA yetu ya mabadiliko, tumekwisha.
Upinzani una majukumu makuu matatu: 'kupinga serikali, kuikosoa na kutafuta kuchukua dola'.
Tukishindwa
kuipinga serikali kwa hatua hizi za mwanzo ambazo ndiyo mchakato wenyewe kuelekea madai yetu ya mabadiliko ya kabla ya Uchaguzi Mkuu 2025 (No Reforms No Election 2025)
Tutashindwa
kuikosoa, kutokana na kushindwa uthubutu.
Mwishowe kupata mabadiliko itakuwa ni ndoto, hivyo dola itabaki mikononi mwa chama dola kongwe.
Tukio la leo ni vyombo vilivyo chini ya CCM kutujaribu kuona kama tutaweza kuipinga, kuikosoa ili tuweze kuchukua dola au ni maneno matupu.
Kukosekana reaction (majibu magumu) ndani ya saa 24 kufuatia tukio la leo, itaipa kiburi serikali ya CCM, bunge na kuona upetevu wetu.
TOKA MAKTABA :
ROMANIA
Kundi la Tökés walikuwa na historia ndefu ya kukosoa utawala na hivyo rais alipokataa kuacha IKULU yake, ikawa sababu kuvuta hisia za polisi wa siri wa Ceausescu, Securitate mashuhuri kuacha umma uamue hatima ya nchi .
Kufikia Desemba 1989, kundi la Tökés hawakuwa wafuasi wake pekee waliokuwa wakilinda ikulu yake, wakiunganisha mikono kuzunguka eneo hilo kushindikiza mabadiliko , bali nguvu ya umma ya Waromania ambao walitengeneza umati wa watu waliojaza mitaa jirani na Ikulu ikamtia woga dikteta akakimbia Ikulu
Serikali ilishindwa kwenye huo mjadala au wewe ndio unaamini ilishindwa?
ANGUKO LA CHAMA DOLA KULE NCHINI ROMANIA, BAADA YA HOTUBA 'IILIYOSHANGILIWA' NA WENGI
View: https://m.youtube.com/watch?v=TcRWiz1PhKU
Nicolae Ceaușescu (matamshi ya Kiromania: [nikoˈla.e t͡ʃe̯a.uˈʃesku]; 26 Januari 1918 -- 25 Desemba 1989) alikuwa mwanasiasa wa Kikomunisti wa nchini Romania.
Alikuwa Kiongozi mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha Romania kuanzia 1965 hadi 1989, na kwa hivyo alikuwa kiongozi wa pili na wa mwisho wa Kikomunisti nchini humo.
Pia alikuwa mkuu wa nchi kutoka 1967 hadi 1989. Utawala wake uliwekwa alama katika muongo wa kwanza na sera ya wazi kuelekea Ulaya Magharibi na Marekani, ambayo ilikengeuka kutoka kwa mataifa mengine ya Warsaw Pact wakati wa Vita Baridi.
Aliendelea na mtindo ulioanzishwa kwanza na mtangulizi wake, mwendazake Gheorghe Gheorghiu-Dej, ambaye kwa busara alishawishi Muungano wa Sovieti kuondoa wanajeshi wake kutoka Rumania mwaka wa 1958. , serikali kali zaidi ya Stalinist katika kambi ya Soviet.
Ilikuwa pia awamu ya muendelezo wa kuitupilia mbali Sera ya utu na kuingiza sera ya mkono wa chuma wenye damu iliyoenea kila mahali, uzalendo uchwara na kuzorota kwa uhusiano wake na wadau wa maendeleo wa kimataifa na madola ya Magharibi na Umoja wa Kisovieti.
Serikali ya Ceaușescu ilipinduliwa katika mapinduzi ya Desemba 1989, na yeye na mke wake kuhukumiwa adhabu ya juu kufuatia kikao cha mahakama cha saa mbili kilichorushwa na televisheni na kwa haraka.
ENGLISH:
Nicolae Ceaușescu (Romanian pronunciation: [nikoˈla.e t͡ʃe̯a.uˈʃesku]; 26 January 1918 -- 25 December 1989) was a Romanian Communist politician.
He was Secretary General of the Romanian Communist Party from 1965 to 1989, and as such was the country's second and last Communist leader. He was also the country's head of state from 1967 to 1989.
His rule was marked in the first decade by an open policy towards Western Europe and the United States, which deviated from that of the other Warsaw Pact states during the Cold War.
He continued a trend first established by his predecessor, Gheorghe Gheorghiu-Dej, who had tactfully coaxed the Soviet Union into withdrawing its troops from Romania in 1958.
Ceaușescu's second decade was characterized by an increasingly brutal and repressive regime—by some accounts, the most rigidly Stalinist regime in the Soviet bloc.
It was also marked by an ubiquitous personality cult, nationalism and a deterioration in foreign relations with the Western powers as well as the Soviet Union.
Ceaușescu's government was overthrown in the December 1989 revolution, and he and his wife were executed following a televised and hastily organised two-hour court session.