kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,931
- 7,828
Mwanasheria Lissu anafikiri siasa ni sheria tu. Anataka kutuaminisha haki ni sawa na sheria. Lengo la kuwepo sheria ni ili kuwepo utawala wa haki. Ili kupata haki kunapotokea mtu kuvunja sheria kunakuepo wanasheria kutafsiri sheria.
Haki ni sawa na kweli, ipo tu. Uanasheria ni taaluma ya kutafsiri sheria ili kujua haki au kweli iko wapi. Kwa bahati mbaya taaluma hiyo hutumika pia kudhulumu haki na kweli. Wapo wanasheria hugeuza kweli kuwa uongo na kupora haki ya mtu. Mara nyingi ni kutokana na rushwa au kumpa haki asiyostahili mteja wao. Kuna watu wachache kutokana na uwezo wao wa kuhonga wanapora haki ya wasiokua na uwezo wa kuhonga.
Kwa hiyo siasa sio sheria tu ila inahusu pia kupambana na dhuluma. Lissu anafikiri kuwaacha watu dhulumati kuishi na mali ya dhuluma ni utawala wa sheria na hasa kama mali iliyodhulumiwa ni ya umma. Anataka watu wenye tuhuma za kudhulumu mali ya umma waachiwe toka gerezani kwa kua uchunguzi wa kesi zao unachukua muda mrefu.
Anataka tusiwaite mabeberu kwa jina lao beberu kwa kua eti wanatufadhili wakati wa njaa na kutukopesha hela. Kwakua eti vitu tunavyotumia vinatengenezwa na wao. Anataka tuwasujudie wazungu. Hivyo ndio vipaumbele vya Lissu.
Haki ni sawa na kweli, ipo tu. Uanasheria ni taaluma ya kutafsiri sheria ili kujua haki au kweli iko wapi. Kwa bahati mbaya taaluma hiyo hutumika pia kudhulumu haki na kweli. Wapo wanasheria hugeuza kweli kuwa uongo na kupora haki ya mtu. Mara nyingi ni kutokana na rushwa au kumpa haki asiyostahili mteja wao. Kuna watu wachache kutokana na uwezo wao wa kuhonga wanapora haki ya wasiokua na uwezo wa kuhonga.
Kwa hiyo siasa sio sheria tu ila inahusu pia kupambana na dhuluma. Lissu anafikiri kuwaacha watu dhulumati kuishi na mali ya dhuluma ni utawala wa sheria na hasa kama mali iliyodhulumiwa ni ya umma. Anataka watu wenye tuhuma za kudhulumu mali ya umma waachiwe toka gerezani kwa kua uchunguzi wa kesi zao unachukua muda mrefu.
Anataka tusiwaite mabeberu kwa jina lao beberu kwa kua eti wanatufadhili wakati wa njaa na kutukopesha hela. Kwakua eti vitu tunavyotumia vinatengenezwa na wao. Anataka tuwasujudie wazungu. Hivyo ndio vipaumbele vya Lissu.