Lissu ameanza kutema cheche

Lissu ameanza kutema cheche

Status
Not open for further replies.
Lissu anawavua nguo duhh!! hadi ushahidi wa emails zilizotumwa!!
 
Kamanda Lissu anaelezea ufisadi wa posho kwa wajumbe wa tume ya katiba!
 
Halafu mzee Warioba alikuwa anasema "tume itafanya maamuzi magumu" huu ni ujinga na umburula wa hali ya juu! Chadema tutoke tu!
 
Email ya Asha Migiro imekamatwa na CDM....ni aibu yule mama anajitia aibu ya bure tu...
Halafu mzee Warioba alikuwa anasema "tume itafanya maamuzi magumu" huu ni ujinga na umburula wa hali ya juu! Chadema tutoke tu!
 
Naomba Mtoi uendelee kutupa Key points za hotuba ya Bwana Lissu
 
Rose na email za kuhujumu katiba mpya, anajivunjia heshima yake.

Utajuta baadaye, chezea siasa.

Hizo pesa nyingi zinazotajwa na ndg Lissu inaonesha zimemchanganya Mzee Waryoba.

CCM wamejua hawa jamaa tukiwajaza mapesa watajisahau na kutenda yale wanayoyataka.
 
Lissu atema Cheche hadi Makinda asema...BASSSIIIIIIIIIIII INATOSHA.........alikua akisoma email ya Migiro kwenda kwana mtandano wenzio Mwigulu, Nape, na wengine........what a shame
 
Mawasiloano ya e-mails kati ya Asha Rose Migiro na Nape Nnauye yamenaswa wakieleza jinsi ya kufanya uchaguzi wa wajumbe wa mabaraza ya katiba ya wilaya.

Pia wametoa maelekezo ya watakaocjaguliwa wawe ni wanaCCM na si vinginevyo.
 
Lissu aseme longologno zake lakini ifike mahali katika hotuba yake atoe tamko rasmi kama chedema imejitoa kwenye mchakato au bado ipo. Na kama imejitoa je wamemuandikia barua Prof. Baregu ili asishiriki shughuli za tume kwa niaba ya chadema?
 
Ah! Kumbe Lissue? Mi nilidhani kuna mtu wa maana anayetoa hoja. Kumbe bwana maneno mengi?
 
Makinda hadi anashika tamah pale anaposikia madudu ya tume ya katiba lisu akiyafichua.
 
Dada Rose Migiro please please resign ulionde heshima yako. Wewe ni international figure kumbuka....nakuonea huruma sana maana unachafua image yako zaidi na zaidi na utadhihirisha kuwa kweli ulikua mtu wa Makundi kule UN kama ilivyowahi kuripotiwa............

Arusha Mambo FM Radio - Home
 
Nasubiri nione serikali jinsi itakavyotoa utetezi kwenye moja ya kifungu cha pesa kilichoombwa na tume ya kupokea maoni ya wananchi kuhusu katiba,kwa ajili ya kuhudumia wajumbe watakaoathirika na virusi vya ukimwi wakati wakiwa katika kazi ya kupokea maoni.
Kwani hivi virusi vya ukimwi vimeanza kuambukizwa kwa njia ya hewa au kusalimiana?

Hii kali aisee...yaani tuanze kulipia watumishi wa Serikali wasijua kufunga zipu zao wakati wakiwa kwenye safari za kikazi! Ha ha haa...Bongo hatuishi vituko! Nunulia kondomu lori moja moja kila mjumbe...kumbafff!
 
Halafu mzee Warioba alikuwa anasema "tume itafanya maamuzi magumu" huu ni ujinga na umburula wa hali ya juu! Chadema tutoke tu!

Vijana wa bavicha kweli hamna nidhamu. Mpaka mzee Warioba mnamtupia matusi namna hii!!!

Mzee Warioba na utumishi wake uliotukuka wa miaka mingi ni mtu anayeheshimika sana duniani. Bavicha jifunzeni adabu...
 
Mama Makinda kawa mpoleeeeeee, Lisu kammaliza kabisaaaaaa anaongea kwa upole sana maana Lisu kawamwagia maji...nyooo siasa si hasa!!!!!
 
''another silly season'' Kwa kiingereza cha kinyiramba.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom