Nyalotsi
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 6,989
- 5,066
Nakumbuka nilikuwa na miaka mitano kituko hiki kilivyotokea. Siku hiyo alikuja mgeni toka Mbeya na debe la mchele. Wali ulipikwa siku hiyo tofauti na tulivyozoea kwani ilikuwa ni wakati wa sherehe tu.! Chezea wali wa sikukuu wewe!! Basi kaka yangu aliyenitangulia alikula siku hiyo mpaka akavimbiwa. Usiku bwana!! Si akatoa haja kubwa kitandani! Nilipozidiwa na harufu nikahamia wanakolala kina sister. Mpaka leo tukirudi home huwa namtania wali ukipikwa.! Je umewahi kutana na vituko vya aina hii ukiwa mdogo?