Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,566
Kwenye Mkutano huo ambao ulifanyika katika kata ya Korongwe jimbo la Nkasi Kaskazini ambako anaelezwa kuwa alitamka kuwa wanaume wa Kijiji Korongwe asilia wamuue Mtendaji wa Kijiji hicho Daud Ismail.
Hata hivyo Lema amekanusha madai ya uchochezi huo akisema alitamka kuwa wanaume ‘wamuoe’ mtendaji huyo akidai ni lugha za kisiasa na wala hakuna madhara yoyote kuhusiana na utendaji wake.
Imedaiwa Lema akiwa na baadhi ya viongozi, wanachama na wafuasi wa Chadema kwenye mkutano huo katika Vitongoji vya Forodhani na Fipa, Kata ya Korongwe, kwa makusudi alitoa kauli ya vitisho kwa mtumishi huo baada ya wananchi kulalamika kwenye mkutano huo kuwa wanasumbuliwa na Mtendaji huyo.
DC Lijualikali alisema haiwezekani kiongozi mwenye ushawishi kuachiwa atambe kwenye kauli hiyo ambayo imepeleka taharuki kubwa kwa wananchi na Mtendaji huo ambaye kwa sasa maisha yake yako hatarini.