Licha ya kuwa kitovu cha mambo ya kimataifa hapa nchini jiji la Arusha lipo hoi kwenye miundombinu

Beginning

JF-Expert Member
Aug 21, 2023
879
2,361

Miundombinu mibovu ndani ya jiji la Arusha.

  • Barabara za lami,ndani ya jiji la Arusha barabara nyingi za lami ni nyembamba na haziendani kabisa na wingi wa magari yaliyopo.
  • Barabara za vumbi,jiji la Arusha limezungukwa na barabara za vumbi kila kona,hii ni aibu kubwa sana kwa jiji ambalo ndiyo kitovu cha utalii nchini .
  • Stendi za daladala,hapa sio aibu tu bali ni fedhea ya hali ya juu mfano stendi ya hiace ya kilombero,samunge,kisongo,ngaramtoni,mbauda etc stendi zote hizi ni mbovu mno.
  • Stendi kuu,hapa ni zaidi ya aibu,stendi hii ni ndogo,chafu etc
  • Masoko,hapa pia pana kazi kubwa ya kufanya! Masoko yote yaliopo ndani ya jiji la Arusha yana-miundombinu mibovu kupitiliza.
Aibu kubwa pia ni kwamba makusanyo ya mapato ndani ya jiji la Arusha ni makubwa mno lakini fedha hazijulikani zinaenda wap?? Mkurugenzi wa jiji yupo,meya wa jiji yupo,mwenyekiti wa halmashuri yupo!!
Wengi mtakubaliana na mimi kwamba ukiondoka Arusha ukarudi hata baada ya miaka mitano utalikuta jiji lipo vilevile hakuna mabadiliko yoyote ya maana!!


Mamlaka husika chukueni hatua tafadhali hili jiji lipo overrated sana,kuna kazi kubwa ya kufanya ili hili jiji liendana na sifa linazopewa.
 
Arusha jengo la posta juzi kati , bunge la East ? Nyie ndio mnamaliza pesa kwa kujengewa majengo daily ..Bado serikali inajenga uwanja mkubwa wa mpira ,kuna halls na supermarket zipo kweny plans za kujengwa kwa ajili wa utalii.
Wewe akili zipo sawa?? Hilo bunge serikali ndo imejenga? Hilo jengo serikali tu ndo imejenga?
 
Mvua ikinyesha hilo soko la kilombero na Samunge ni tope utadhani wapo kwenye bwawa...hiyo Stand ya hiace hapo Kilombero haieweleki ila ushuru wanachukua kila siku ukishuka huko Majengo chini mvua ikinyesha maji yanasambaa bara barani wameshindwa kujenga mitaro mikubwa kidogo sijui huko Jiji shida nini..
 
Mvua ikinyesha hilo soko la kilombero na Samunge ni tope utadhani wapo kwenye bwawa...hiyo Stand ya hiace hapo Kilombero haieweleki ila ushuru wanachukua kila siku ukishuka huko Majengo chini mvua ikinyesha maji yanasambaa bara barani wameshindwa kujenga mitaro mikubwa kidogo sijui huko Jiji shida nini..
Hili jiji linaongoza kwa ubadhirifu wa fedha
 
Back
Top Bottom