Ni mongoni mwa majiji sita ya nchi hii. Inajulikana pia kama Geneva ya Afrika na pia kitovu cha utalii Tanzania.
Lakini ukweli ni kuwa, ni miongoni mwa miji mibovu na ya hovyo hapa Tanzania. Nimeishi Arusha mwaka wa saba sasa. Tanzania hii nimeizunguka takribani mikoa yote isipokuwa Ruvuma, Mtwara na Lindi.
Tofauti na inavyosifiwa, huu mkoa wa Arusha (na hapa naongelea Arusha Jiji) ni pabovu mno. Miundombinu yake inatia kichefuchefu. Ukitoka barabara kuu, ndani ya mita chache tu hapatamaniki. Mathalani, ukiwa katika barabara ya kuelekea Babati, labda maeneo ya Ngarenaro ni kinyaa kitupu. Nenda Matejoo ni uozo mtu. Nenda Mbauda au Morombo. Kipindi cha masika madimbwi ya maji kila eneo. Nenda uswahilini, Muriet hadi intel, ndio usiseme. Barabara mbovu hata kwa pikipiki hapafikiki. Nenda Ngusero, mamaaaa!! Hapafai. Hata Njiro wanapokaa mataita, barabara zake ni za hovyo sana.
Mbunge yupo. Madiwani wapo. Wenyeviti wa mitaa wapo. TARURA ipo. Shida ni nini?
Arusha ni pazuri ukiwa katikati ya mji. Kwingine, hapana
Lakini ukweli ni kuwa, ni miongoni mwa miji mibovu na ya hovyo hapa Tanzania. Nimeishi Arusha mwaka wa saba sasa. Tanzania hii nimeizunguka takribani mikoa yote isipokuwa Ruvuma, Mtwara na Lindi.
Tofauti na inavyosifiwa, huu mkoa wa Arusha (na hapa naongelea Arusha Jiji) ni pabovu mno. Miundombinu yake inatia kichefuchefu. Ukitoka barabara kuu, ndani ya mita chache tu hapatamaniki. Mathalani, ukiwa katika barabara ya kuelekea Babati, labda maeneo ya Ngarenaro ni kinyaa kitupu. Nenda Matejoo ni uozo mtu. Nenda Mbauda au Morombo. Kipindi cha masika madimbwi ya maji kila eneo. Nenda uswahilini, Muriet hadi intel, ndio usiseme. Barabara mbovu hata kwa pikipiki hapafikiki. Nenda Ngusero, mamaaaa!! Hapafai. Hata Njiro wanapokaa mataita, barabara zake ni za hovyo sana.
Mbunge yupo. Madiwani wapo. Wenyeviti wa mitaa wapo. TARURA ipo. Shida ni nini?
Arusha ni pazuri ukiwa katikati ya mji. Kwingine, hapana