LHRC yamtaka Dkt. Magufuli kufuta kauli zake

mansoorsaid

JF-Expert Member
May 31, 2014
1,498
284
Mnadai Magufuli kasema Polisi akiuwa jambazi hashitakiwi, sawa hilo amepotoka; je, hili la Lowassa la ubaguzi wa dini.

LHRC kauli iliyotolewa na Lowassa kanisani mbona hamjalikemea?

Kuhusu Libya ni kweli walitaka mabadiliko leo wanajuta huo uwongo?

Acheni nyinyi vineno nyinyi ndio wachonganishi
LHRC yamtaka Dkt. Magufuli kufuta kauli zake


Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimekemea kauli zenye kuwajengea hofu wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kidemokrasia unaoendelea kwa kutoa mifano isiyoshabihiana na hali iliyopo nchini ikiwemo kufananisha na nchi zenye machafuko.

Katika taarifa yake iliyotolewa kwa vyombo vya habari imemtaka mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM, Mh. John Magufuli kufuta kauli zake ikiwemo ya kufanisha mchakato wa uchaguzi na vuguvugu la mabadiliko ya Libya pamoja na serikali yake kuwapiga risasi wahalifu wa kutumia silaha.

Kituo hicho kimesema kauli hizo zinatoa vitisho kwa wapiga kura kinyume na demokrasia kwa kuwa huwezi kufananisha mabadiliko ya kimapinduzi ya Libya na umwagaji damu uliotokea huko na mabadiliko ya amani kwa kupitia mchakato wa uchaguzi za kidemokrasia.

SOURCE: EATV NA EAST AFRICA RADIO
 
Magamba yanaruka nakukanyagana,mwaka huu ccm wanalia? Hizi ni dalili za kuachia ikulu.
 
mnadai magufuli kasema polisi akiuwa jambazi hashitakiwi sawa hilo amepotoka je hili la lowasa la ubaguzi wa dini.
LHRC kauli iliotolewa na lowasa kanisani mbona hamjalikemea kuhusu libya ni kweli walitaka mabadiliko leo wanajuta huo uwongo? acheni nyinyi vineno nyinyi ndio wachonganishi

Na hili la Magufuli la Lowasa akishinda itaingia katika machafuko kama Libya,Misri'
 
LHRC ni wa kupuuzwa.mgonbea wao alisema atamtoa babu seya na sheikh farid na genge lake hawakutoa tamko

wewe ndo wa kupuuzwa kwani hujui kitu,alichosema lowasa ni kwa nini kesi ya akina Shekh Farid haifiki mwisho watu wanateseka na pia akasema ni kwa nini watu wanalalamika kuhusu babu seya,kwa hiyo kama atapata ridhaa ya wananchi ataliangalia upya suala hilo,kwa mujibu wa sheria sasa anakosa gani hapo.
 
Kuuwatoa masheikh walio na kesi, na kumtoa bau seya aliyehukumiwa sio kuingilia uhuru wa mahakama??? mapunguani kweli hao
 
mnadai magufuli kasema polisi akiuwa jambazi hashitakiwi sawa hilo amepotoka je hili la lowasa la ubaguzi wa dini.
LHRC kauli iliotolewa na lowasa kanisani mbona hamjalikemea kuhusu libya ni kweli walitaka mabadiliko leo wanajuta huo uwongo? acheni nyinyi vineno nyinyi ndio wachonganishi

Wewe na Magufuli ndio wachonganishi. Lybia walifanya fujo kumwondoa rais wao. Walitaka mabadiliko ya vurugu kwa sababu rais wao alikuwa dikteta. Sasa Tanzania nchi ya kidemokrasia sasa hivi tuko kwenye mchakato wa uchaguzi. Ikitokea Chadema wakashinda na CCM wakaachia madaraka kidemokrasia na kwa amani kabisa, hayo machafuko yatatoka wapi? Machafuko yatatokea endapo CCM wakishindwa halafu wakang'ang'ania madaraka. Labda hiki ndicho anachomaanisha Magufuli. Labda ndio goli la mkono la Nape. Hapa Tume ya Uchaguzi hawakustahili kukaa kimya.
 
wewe ndo wa kupuuzwa kwani hujui kitu,alichosema lowasa ni kwa nini kesi ya akina Shekh Farid haifiki mwisho watu wanateseka na pia akasema ni kwa nini watu wanalalamika kuhusu babu seya,kwa hiyo kama atapata ridhaa ya wananchi ataliangalia upya suala hilo,kwa mujibu wa sheria sasa anakosa gani hapo.

ww ndio bure ghali leo ndio unajua akina faridi wawe wanamwagiwa tindikali viongozi wa dini umefurahi ona sasa toka wamewekwa ndani zanzibar ipo salama kabisa sera zenu hazina maana ni zilezile za kinafiki
 
mnadai magufuli kasema polisi akiuwa jambazi hashitakiwi sawa hilo amepotoka je hili la lowasa la ubaguzi wa dini.
LHRC kauli iliotolewa na lowasa kanisani mbona hamjalikemea kuhusu libya ni kweli walitaka mabadiliko leo wanajuta huo uwongo? acheni nyinyi vineno nyinyi ndio wachonganishi

Basi sawa naye kapotoka!
 
wewe ndo wa kupuuzwa kwani hujui kitu,alichosema lowasa ni kwa nini kesi ya akina Shekh Farid haifiki mwisho watu wanateseka na pia akasema ni kwa nini watu wanalalamika kuhusu babu seya,kwa hiyo kama atapata ridhaa ya wananchi ataliangalia upya suala hilo,kwa mujibu wa sheria sasa anakosa gani hapo.

Kosa ni kusema ataliangalia upya wakati kesi ya sheikh ipo mahakamani bado na yule mlawiti kafika hadi mahakama ya rufaa lakini hukumu pale pale.sasa huyo mzee atapata wspi ubavu wa kuingilia mahakama
 
Lowassa kasema safari hii ni zamu ya Lutheran eti apewe yeye kwa kua wenzake walikua wakatoliki.LHRC kimyaaaa au ndio hila za walutheri?halafu kumbe kaskazini ina walutheri wengi kuliko sehemu yoyote ya jamhuri hii.wallahi tayari nimeamua nasubiri siku tu
 
LHRC wametufanyisha kazi za uangalizi wa BVR na hawajatulipa haki zetu mbona ilo hawatolei tamko
 
Back
Top Bottom