Leo nafunga pingu za maisha

Hongera sana na kila la kheri. Mungu awalinde, awatunze na kuwaweka pamoja hata uzima wa milele.
 

Habari za jumapili wana JF leo tarehe 17 June 2012 nafunga ndoa na mpenzi wangu ambaye tumekuwa na mahusiano since 2007 tukiwa chuoni. Ndoa itafungwa katika kanisa la SDA Njiro wote mnakaribishwa. Namshukuru Mungu kuifikia siku hii

asante sana mdau,,,ALLAH awafnyie wepes kwenye JAMBO lako na aibariki NDOA YENU,,,,hope usiku wa leo utajifaragua kwa raha zako
 
hongera sana,na ukaanze kulila tunda ulilonyimwa toka 2007 na pia Mwenyezi Mungu akupe nguvu,pia akujalie siha njema.
 
Hongera kaka kwa kuukubali huo msalaba mpaka goligoti...mungu akujalie wepesi katika kuubeba na akupe uvumilivu katika kuufikisha goligoti. Amen!
 
nice step ubarikiwe kwa kuvumilia to JF ina mwaka 1 hadi sasa miaka 6 ndo mnahalalisha kanisani..
 
Hongera sana ndugu..Nawatakia maisha mema ya Ndoa na Mungu wabariki sana..
 
Kwanza mwenyezi mungu apewe sifa na utukufu kutulinda na kutufikisha leo, mshukuruni kwa kuwapa uvumilivu kwa mda wote huo,

Ndoa na iheshimiwe na watu wote! Nawatakieni maisha mema yenye baraka,furaha na heshima ili muwe familia yenye kumtukuza mungu mda wote.

Mwenyezi mungu awatangulie
 
Mkuu @Puduku naamini JF kupitia MMU imekufunza vya kutosha kuhusu maisha ya ndoa na mahusiano na watu waliokuzunguka......
Hatutarajii siku uje hapa uanze kulalamika kwmaba ndoa ngumu au inataka kukushinda................

Hongera sana na ninawatakia maisha mema ya Ndoa.
 
  • Thanks
Reactions: mka
hongera sana ..ila na ww ulianza uzinifu wakati bado mdogo bwana ...mungu hapendi mambo hayo...hongera lakini kwa kuingia kwenye chama cha kujitakia BP na Heart attacks na brain concusions za bure.....
 
Pukudu, mbona hukutuletea kadi mkuu, ndio maana hautualiki tafrija.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom