Kiboko ya Jiwe
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 12,702
- 36,141
Moja kwa moja kwenye mada.
Jana wakati naingia ofisini nakuta kadi ya mchango wa harusi mezani nikaambiwa na mfanyakazi mwenzangu kuwa ni yangu.
Nafunua ndani nakuta haina hata jina Iko plain na wanaooana siwajui. Nikamuuliza yule mfanyakazi mwenzangu vipi mbona haina jina? Akasema wewe andika jina lako kadi kasambaza mama mmoja wa pale canteen mtoto wake anaoa.
Nilimuuliza ni mama yupi? Akanipa maelezo kuhusu huyo mama bado sijamjua, yawezekana tunaonana tu ila ndo vile simjui.
Niliwaza nikagundua kuwa huyu mama ananifahamu kidogo tu ndio maana hata jina langu kashindwa kuandika kwenye hii kadi. Nikamuuliza yule dada kwanini huyu mama atoe kadi kiholela? Mada ikaiashia hapo.
Hivi watu kama hawa ukiwaita wajinga unakosea? Kwanini mtu asifanye sherehe kwa kipato chake?
Kuwachangia mamilioni vijana kisha kuwafanyia sherehe kubwa baadaye wanaishi maisha ya kuungaunga na kuanza kutafuta ajira ni sawa na kusema walianza maisha ya fahari kisha wakaishi maisha ya kimaskini.
Binafsi michango ya hharusi na send off nachanga ila naangalia ni nani namchangia.
Ndoa nilifungia kwa DC Ilala kuepuka kashkashi zisizo na sababu. Nitaanza vipi kumdai mtu nisiyemkopesha? Maana kukusanya michango vita yake ni kama unamdai mtu.
Kijana anza maisha kwa level yako kisha pambana, inuka. Ukiwa na pesa utaweza kufanyia harusi hata Juu ya puto kwenye hifadhi ya Tarangire au Serengeti na watu watakuzawadia mamilioni mengi.
Mimi kijana akija kwangu na wazo zuri la kumwinua nawiwa kumsaidia. Nimetoa support kwa vijana kadhaa mitaani, hata hapa JF nilianzisha kamchezo nilianza kutoa mitaji midogomidogo rejea account yangu ya zamani niliyopigwa ban ya BONDE LA BARAKA.
Jana wakati naingia ofisini nakuta kadi ya mchango wa harusi mezani nikaambiwa na mfanyakazi mwenzangu kuwa ni yangu.
Nafunua ndani nakuta haina hata jina Iko plain na wanaooana siwajui. Nikamuuliza yule mfanyakazi mwenzangu vipi mbona haina jina? Akasema wewe andika jina lako kadi kasambaza mama mmoja wa pale canteen mtoto wake anaoa.
Nilimuuliza ni mama yupi? Akanipa maelezo kuhusu huyo mama bado sijamjua, yawezekana tunaonana tu ila ndo vile simjui.
Niliwaza nikagundua kuwa huyu mama ananifahamu kidogo tu ndio maana hata jina langu kashindwa kuandika kwenye hii kadi. Nikamuuliza yule dada kwanini huyu mama atoe kadi kiholela? Mada ikaiashia hapo.
Hivi watu kama hawa ukiwaita wajinga unakosea? Kwanini mtu asifanye sherehe kwa kipato chake?
Kuwachangia mamilioni vijana kisha kuwafanyia sherehe kubwa baadaye wanaishi maisha ya kuungaunga na kuanza kutafuta ajira ni sawa na kusema walianza maisha ya fahari kisha wakaishi maisha ya kimaskini.
Binafsi michango ya hharusi na send off nachanga ila naangalia ni nani namchangia.
Ndoa nilifungia kwa DC Ilala kuepuka kashkashi zisizo na sababu. Nitaanza vipi kumdai mtu nisiyemkopesha? Maana kukusanya michango vita yake ni kama unamdai mtu.
Kijana anza maisha kwa level yako kisha pambana, inuka. Ukiwa na pesa utaweza kufanyia harusi hata Juu ya puto kwenye hifadhi ya Tarangire au Serengeti na watu watakuzawadia mamilioni mengi.
Mimi kijana akija kwangu na wazo zuri la kumwinua nawiwa kumsaidia. Nimetoa support kwa vijana kadhaa mitaani, hata hapa JF nilianzisha kamchezo nilianza kutoa mitaji midogomidogo rejea account yangu ya zamani niliyopigwa ban ya BONDE LA BARAKA.