Leo Asubuhi Nikiwa Ubungo bus terminal....

Leo Asubuhi Nikiwa Ubungo bus terminal....

Mwambie anatakiwa agegedwe kwanza kama fikra zake zilivyomtuma wakati anakuzodoa then atapewa.Hawezi kubana
 
Give her her ----ing phone and her concious will teach her a lesson
 
jifunze kusamehe, mpe simu yake ajione mjinga mwenyewe na kwa njia hiyo atakuwa na nidhamu, yaani hapo aliwaza mengine na kichwani mwake alikuwa ana yake yalomkera so mpe tu ndg yangu na Mungu atakubariki
 
huyo ni limbukeni mrudishie tu simu yake haina haja ya kusumbua akili yako
 
Hii hekaya napata shida sana kuiamini, yaani mtu akuzabe kibao kwa kuwa tu umemgusa bega, kusonya labda lakini sio kibao labda kama na wewe ulimgusa kihuni huni sana.
 
hii habar nimeiona sehem flani hivi hivi ila kule mdau alisema stand ya mwanza hapa mdau kabadili ikawa ubungo
Copy and paste
 
story yako imekosa mashiko pale ulipoingiza mambo ya kutandikana vibao.

kwa eneo kama ubungo na asubuhi ile mtu kupigwa kibao inge-draw attention ya watu wengi, isingekuwa rahisi simu hiyo kutokuwa sandakalawe.

pia isingekuwa rahisi upigwe kibao unyamaze na kujikunyata kama umefumaniwa!!!!!

umedhihirisha kuwa hii ni tungo.
 
Leta tuiflash...umpe ndg yako..wanawake wamejaa ushetani..vichwa vyao vimejaa bifu/vita..mashindano.km huna ndugu..piga moto.....
 
Hii hekaya napata shida sana kuiamini, yaani mtu akuzabe kibao kwa kuwa tu umemgusa bega, kusonya labda lakini sio kibao labda kama na wewe ulimgusa kihuni huni sana.

Hata mimi nimekosa jibu...yaani mtu arushe na kibao kisa kaguswa bega au kaitwa? Basi huyo dada atakuwa wa ajabu kweli kweli ati....
 
Stay positive mkuu, inaweza kuwa ndo mwanzo wa tamthiliya yenu mpya!

Onana nae, mrudishie cmu yke ili tusubiri part two yenu!

Pana fursa hapo mkuu
 
Hata mimi nimekosa jibu...yaani mtu arushe na kibao kisa kaguswa bega au kaitwa? Basi huyo dada atakuwa wa ajabu kweli kweli ati....

Hujawajuwa wadada wa bongo hii kwa nyodo, hapa mjini kuna watu lakini VIATU ndo wengi. Mi sishangai, Tena kama sie wengine wenye sura ngumu yanatukuta mengi.
 
me simlaumu huyo dada dunia ya leo IMEHARIBIKA sana WABAYA ni wengi kuliko WEMA, ukijifanya wakusikiliza kila anaekuita huko barabarani yatakukuta makubwa, nahisi hata mm ninge react vibaya japo nisingeweza kukufyonya na kukupiga ila tu nisingegeuka wala kutaka kukusiliza ningeingia tu kwenye gari langu na kuondoka, manake sasahivi hata kumsaidia mwenye shinda imekuwa ngumu sababu wenye shida na matapeli wote wanafanana huwezi kujua yupi ni yupi
 
mpatie simu yake bila kumpa sharti lolote, ndio walivyo baadhi yao......
 
Stay positive mkuu, inaweza kuwa ndo mwanzo wa tamthiliya yenu mpya!

Onana nae, mrudishie cmu yke ili tusubiri part two yenu!

Pana fursa hapo mkuu
 
Mkuu, zima simu, toa laini na umupotezee milele, watu kama hao wanaodhani wao ni wa pekee dawa yao ni hiyo
 
Leo asubuhi nikiwa stand ya mabasi ya ubungo;
mdada mmoja wakati anapanda kwenye kagari
kake akadondosha simu;
mimi nikamuita ili nimweleze kilichotokea,ak
anisonya tena msonyo wa dharau sana na
nikajuta kumgusa bega ka sababu ya kibao
alichonipiga.
Alipoondoa gari nikaiokota hiyo simu
nakuondoka zangu;
wala sikuizima.


Nafika town simu hiyo ikaita
nikapokea kwa shauku ya kujua nani....
haya ndo ya kawa maongezi yetu na mpigaji..

mimi;Hallo habari yako...
yeye;Nzuri;
mimi;nani wewe ...
yeye;Mimi ndo mwenye hiyo simu ....
mimi;Na mimi ndo nilokuita na ukanizaba kibao
pale stand ya ubungo leo na ukanisonya ....
yeye;Basi kaka nisamehe naomba unambie
ulipo nije tuelewane ....

Mimi;Nitakwambia baadaye ..
(nikakata simu na kuzima)
Swali nimwambie napatikana wapi au
nimpotezee ili liwe fundisho kwake?

Nimeikuta Facebook hii . Cut & paste
 
Kuna vitu vinatia hasira hata kuvisoma tu. Lakini mrudishie simu yake atajiona mjinga sana na atabaki na ujinga wake.
 
Back
Top Bottom