Lembeli: CCM si Mama yangu

Lembeli: CCM si Mama yangu

Nachukia sana mapenzi ya chama kwenye keyboard,
Lets be real guys.
 
- Yale yale kama upo kwenye chama hakina msimamo kama wako si utoke tu uende kule kwenye chama chenye msimamo kama wako, Rais Reagan alikuwa Democrat mpaka mwaka 1962 alipoona hawana msimamo kama wake akaingia Republican sasa hawa kwa nini wanapiga piga kelele ndani ya chama ambacho hakina msimamo kama wao watoke tu waone kama CCM itayumba!!

Le Mutuz

Le Mutuz unajua hakuna mwenye hati miliki ya ccm,sasa kama mwanachama anaona kuna mambo ya kipimbavu yanaendelea ya chama dawa si kuhama isipokuwa kusema ukweli dhidi ya unafiki,upuuzi na kadhia zote ambazo hazijengi chama.Humo ccm kuna wanafiki kama kina Lukuvi,Wasira,Mwigulu na wengine wengi tu ambao kinyesi cha Mwenyekiti au Katibu mkuu wao watakiita KEKI mchana kweupe wa jua la saa 6.Kwa hvo Lembeli anawaonyesha kwamba atapambana nao hao wanafiki akiwa ndani ya Chama ili wenye akili wajue na kutambua ukweli kati yake na wanafiki.Hata wewe uki-differ na Mzee Chigwiyemici dawa si kumkana kama yeye si babako na ukaamua kwenda kutafuta baba mwingine,itakubidi kukomaa na kumwonyesha alipokosea
 
- Kaka NEC ndio Mkutano wa mwisho wa CCM wa kuamua msimamo wa CCM kama Lembeli hautaki ajiondoe mara moja kwenye chama ambachi hakikidhi mahitaji yake!1

Le Mutuz

Wewe Baharia wa zamani Tanzania hii ya leo si ile ya kina Mzee wetu JSM.Kwa hiyo hata wana ccm(wenye akili tu) wanajua kwanini ccm inakomaa na kura za wazi.Hakuna hata chembe ya siri kwamba zikipigwa kura za siri hao wanaotaka kura za wazi watakuwa against msimamo wa chama chao ccm.Mtu kama Wasira hawezi kuthubutu kunena kama Lembeli coz anajua JK amemwokoa kutoka kwenye dhiki ya kutisha,lakini nakuhakikishia kama kura ni ya siri Wasira atakuwa against msimamo wa ccm wa serikali 2.Kwa bahati mbaya sana namjua huyo Wasira kuliko hata anavyojijua mwenyewe
 
[FONT=courier new said:

“Mimi ndiye Lembeli na nitabakia kuwa hivyo, ndiyo maana
nilikuwa nataka itumike kura ya siri ili kuhifadhi uhuru wa mawazo yetu. Nyerere alituambia kuwa wananchi wanataka mabadiliko na wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM,” alisisitiza.

Lembeli aliwataka wajumbe wenzake kuacha
woga wa kufungwa na misimamo ya vyama au makundi yao kwani hata Rais Jakaya Kikwete aliwahi kusema: “Akili za kuambiwa changanya na zako
[/FONT]

Hayo maneno ya kwenye red nimeyapenda sana, CCM wamewekewa ukomo wa kufikiri, kamati kuu ishafikiri kwa niaba yao. Uhuru katika bunge unakuwepo mjumbe anapojadili kwa uwazi na kupiga kura kwa siri na si vinginevyo.
 
[FONT=courier
new]JUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba, James
Lembeli (CCM), amesema kuwa yuko tayari kufanyiwa lolote na chama chake
lakini kamwe hatatengua msimamo wake wa kudai Serikali ya Tanganyika.

Kauli hiyo nzito ya Lembeli, mmoja wa wabunge wa CCM wenye msimamo
mkali, ilipata kutolewa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere miaka ya 90 wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo
chama hicho kilikuwa kikituhumiwa kwa rushwa na hivyo kupoteza mwelekeo.

Katika mazingira hayo, Mwalimu alisema kama chama hicho
kisipojirekebisha, anaweza kurudisha kadi yao, kwani CCM haikuwa mama
yake.

Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu huku akitumia maneno
hayo ya Mwalimu, Lembeli ambaye pia ni Mbunge wa Kahama alisema baadhi
ya wajumbe ni waoga na wanafiki kwa kuogopa kusimamia kile
wanachokiamini.

“Historia haikarabatiwi, mimi naweza kufa au kuadhibiwa na chama changu
kutokana na msimamo huu lakini historia itaandikwa.

“Pale Ikulu si kuna picha ya hayati Oscar Kambona, huyu si alifungwa kwa
makosa ya uhaini, mbona picha yake haikuondolewa katika viongozi wa
historia ya nchi hii?” alihoji.

Lembeli alidai kuwa Watanzania wasubiri wamuone wakati wa mjadala wa
pamoja wa rasimu ya Katiba bungeni huku akitamba kuwa hatabadili msimamo
hata kama unakinzana na wenzake wa CCM.

“Sina wa kumfurahisha zaidi ya wapiga kura wangu, hawa ndio wenye uwezo
wa kunishughulikia endapo nitaunga mkono jambo ambalo litakuwa kinyume
na wao.

“Mimi ndiye Lembeli na nitabakia kuwa hivyo, ndiyo maana nilikuwa nataka
itumike kura ya siri ili kuhifadhi uhuru wa mawazo yetu. Nyerere
alituambia kuwa wananchi wanataka mabadiliko na wasipoyapata ndani ya
CCM watayatafuta nje ya CCM,” alisisitiza.

Lembeli aliwataka wajumbe wenzake kuacha woga wa kufungwa na misimamo ya
vyama au makundi yao kwani hata Rais Jakaya Kikwete aliwahi kusema:
“Akili za kuambiwa changanya na zako.”
[/FONT]

Chanzo:
Tanzania Daima
mimi binafsi namkubali sana huyu mzee ni mzalendo na kama wasukuma wote wangekuwa kama huyu mzee nchi ingekuwa na maendeleo makubwa sana kwa kweli
 
Every existence has a reason. Kama Lembeli amesukumwa na hali yoyote kusema asemayo anatekeleza tu sentensi ya kwanza kwamba kila kitu kinakuwapo kwa makusudi fulani.
 
mimi binafsi namkubali sana huyu mzee ni mzalendo na kama wasukuma wote wangekuwa kama huyu mzee nchi ingekuwa na maendeleo makubwa sana kwa kweli

Hata huku Bariadi hawa wabunge wetu wamechoka mwingine ana stroke mwingine kisukali CHADEMA tunawakaribisha mtukomboe tumechoka.
 
Every existence has a reason. Kama Lembeli amesukumwa na hali yoyote kusema asemayo anatekeleza tu sentensi ya kwanza kwamba kila kitu kinakuwapo kwa makusudi fulani.
 
Wewe Baharia wa zamani Tanzania hii ya leo si ile ya kina Mzee wetu JSM.Kwa hiyo hata wana ccm(wenye akili tu) wanajua kwanini ccm inakomaa na kura za wazi.Hakuna hata chembe ya siri kwamba zikipigwa kura za siri hao wanaotaka kura za wazi watakuwa against msimamo wa chama chao ccm.Mtu kama Wasira hawezi kuthubutu kunena kama Lembeli coz anajua JK amemwokoa kutoka kwenye dhiki ya kutisha,lakini nakuhakikishia kama kura ni ya siri Wasira atakuwa against msimamo wa ccm wa serikali 2.Kwa bahati mbaya sana namjua huyo Wasira kuliko hata anavyojijua mwenyewe

- Kaka baba yako simjui ila one thing habari za kura ya siri na wazi sio ishu tena imeisha tuwe progressive tuongelee mapya ya kura za siri na wazi yamepitwa na wakati sasa!! na Kidumu chama cha mapinduzi

Le Mutuz
 
kwa Tanganyika ccm wanafunika kombe mwanaharamu apite,lakini ukweli unabakia pale pale! wakitaka amani katiba ya zanzibar ya 2010 ifutwe ndiyo hapo watanganyika wataacha kudai nchi yao!
 
- Kaka baba yako simjui ila one thing habari za kura ya siri na wazi sio ishu tena imeisha tuwe progressive tuongelee mapya ya kura za siri na wazi yamepitwa na wakati sasa!! na Kidumu chama cha mapinduzi

Le Mutuz

Hukijui kile kibabu kiitwacho J.Malecela kilikuwa PM wetu lakini Nyerere mwishoni alikipiga chini kwa sababu alitaka kuuza nchi yetu kwa waarabu na alislimu na kuitwa Jumanne
 
JUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba, James Lembeli (CCM), amesema kuwa yuko tayari kufanyiwa lolote na chama chake lakini kamwe hatatengua msimamo wake wa kudai Serikali ya Tanganyika.

Kauli hiyo nzito ya Lembeli, mmoja wa wabunge wa CCM wenye msimamo mkali, ilipata kutolewa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere miaka ya 90 wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo chama hicho kilikuwa kikituhumiwa kwa rushwa na hivyo kupoteza mwelekeo.

Katika mazingira hayo, Mwalimu alisema kama chama hicho kisipojirekebisha, anaweza kurudisha kadi yao, kwani CCM haikuwa mama yake.

Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu huku akitumia maneno hayo ya Mwalimu, Lembeli ambaye pia ni Mbunge wa Kahama alisema baadhi ya wajumbe ni waoga na wanafiki kwa kuogopa kusimamia kile wanachokiamini.

“Historia haikarabatiwi, mimi naweza kufa au kuadhibiwa na chama changu kutokana na msimamo huu lakini historia itaandikwa.

“Pale Ikulu si kuna picha ya hayati Oscar Kambona, huyu si alifungwa kwa makosa ya uhaini, mbona picha yake haikuondolewa katika viongozi wa historia ya nchi hii?” alihoji.

Lembeli alidai kuwa Watanzania wasubiri wamuone wakati wa mjadala wa pamoja wa rasimu ya Katiba bungeni huku akitamba kuwa hatabadili msimamo hata kama unakinzana na wenzake wa CCM.

“Sina wa kumfurahisha zaidi ya wapiga kura wangu, hawa ndio wenye uwezo wa kunishughulikia endapo nitaunga mkono jambo ambalo litakuwa kinyume na wao.

“Mimi ndiye Lembeli na nitabakia kuwa hivyo, ndiyo maana nilikuwa nataka itumike kura ya siri ili kuhifadhi uhuru wa mawazo yetu. Nyerere alituambia kuwa wananchi wanataka mabadiliko na wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM,” alisisitiza.

Lembeli aliwataka wajumbe wenzake kuacha woga wa kufungwa na misimamo ya vyama au makundi yao kwani hata Rais Jakaya Kikwete aliwahi kusema: “Akili za kuambiwa changanya na zako.”


Chanzo:
Tanzania Daima

Safi sana Jembe,nuru lazima iwekwe juu ya kiango
 
- Kaka baba yako simjui ila one thing habari za kura ya siri na wazi sio ishu tena imeisha tuwe progressive tuongelee mapya ya kura za siri na wazi yamepitwa na wakati sasa!! na Kidumu chama cha mapinduzi

Le Mutuz

nakumbuka ushauri wako kwa CHADEMA kipindi Zito ukitetea kuwa sio dhambi watu kutofautiana mawazo.sasa nimeelewa kuwa kutofautiana cdm sawa,ccm sio sawa
 
Kwa msimamo huo,si ajabu akaunga mkono mswada wa kuruhusu mashoga.
 
- TOO BAD Katiba inatengezwa kwa mujibu wa sheria zilizopo sasa ambazo zipo wazi kwamba chama kinachotawala ndio chenye nafasi kubwa ya kuandika Sheria na sio vinginevyo!!

Le Mutuz

Duh hii ndo akili yako kaka yangu W. J. Malecela au ya kuambiwa? Kama ya kuambiwa basi fuata ushauri wa mwenyekiti wako kwamba uchanganye na ya kwako.
 
Back
Top Bottom