Lembeli: CCM si Mama yangu

Lembeli: CCM si Mama yangu

lembeli.jpg


Mbunge wa Kahama (CCM),James Lembeli

Na Ashton Balaigwa

1st April 2014


Mbunge wa Kahama kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),James Lembeli
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba ambaye pia ni Mbunge wa Kahama kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), James Lembeli, amesema msimamo wake kwenye mchakato wa kutunga Katiba mpya ni kuona Muungano wa Tanzania unakuwa wa muundo wa serikali tatu.


Lembeli alitoa msimo huo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma baada shughuli za Bunge kuahirishwa.
Alisema licha ya chama chake kuwa na msimamo wa kuwa na muundo wa serikali mbili, yeye binafsi hayuko tayari kwa hilo na kwamba atapambana ndani ya Bunge hilo kutaka muundo wa serikali tatu upitishwe.


Alisema miongoni mwa kazi atakazozifanya ili kufanikisha lengo hilo ni pamoja na kuwashawishi wabunge wenzake wakubali muundo wa serikali tatu kwa lengo la kumaliza kabisa kero za Muungano ambazo alisema nyingi zimesababishwa na muundo wa serikali mbili.


Lembeli alisema kuwa hata Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alikwisha kusema kupitia hotuba zake kuwa Watanzania wanahitaji mabadiliko na wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM.
“Tukifuata hata maelekezo ya Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, alituasa kuwa Watanzania wanahitaji mabadiliko na akasema wazi kuwa wasipoyapata mabadiliko ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM, sasa mimi naona hii ilikuwa ni fursa kwa chama changu kuwapatia Watanzania mabadiliko, lakini bado msimamo wake siyo wa mabadiliko ndiyo sababu mimi nimeona nianze kuonyesha njia ya kuelekea kwenye mabadiliko,” alisema Lembeli.


Alisema hayuko tayari kuunga mkono na kupitisha Rasimu ya Katiba yenye muundo wa serikali mbili kama chama chake kinavyotaka kwa sababu hayo siyo mabadiliko, hivyo atahakikisha anashawishi wajumbe wenzake wafanye mabadiliko kwa kuingia kwenye muundo wa serikali tatu.


Alisema hata Rais Jakaya Kikwete katika hotuba ya uzinduzi wa Bunge hilo Machi 21, mwaka huu alisema kuwa wajumbe wasikubali kufuata mawazo ya kuambiwa pekee, bali watumie pia na akili zao, hivyo yeye pamoja na misimamo ya kuambiwa na chama chake pia atakuwa na msimamo wa serikali tatu ambao ni akili zake mwenyewe.


“Katika hotuba yake Rais Kikwete alisema kuwa akili za kuambiwa changanya na zako upate majibu, sasa chama changu kimeniambia kuwa msimamo ni serikali mbili, nimechanganya na akili zangu na nimeona msimamo wangu ni serikali tatu,” alisema Lembeli.


Lembeli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, alisema Muungano wa sasa una changamoto nyingi na malalamiko kutoka pande zote, hivyo ili kuondoa malalamiko na changamoto hizo ni lazima ziwepo serikali tatu za Tanganyika, Zanzibar na ya Muungano.


“Mimi ni mmoja wa waumini wa kudai serikali ya Tanganyika, hilo naliweka wazi na wala siogopi, nataka Watanzania wajue kuwa tunachopigania ni Muungano wa usawa kwa pande zote za Muungano, kama ipo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, sioni sababu ya kuikataa Serikali ya Tanganyika,” alisema Lembeli.


Rasimu ya Katiba iliyopendekezwa na iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kuwasilishwa kwenye Bunge Maalum la Katiba na Mwenyekiti wake, Jaji Joseph Warioba, Machi 18, mwaka huu inapendekeza kuwapo kwa muundo wa serikali tatu ambazo zitaondoa kero za Muungano.


Hata hivyo, Rais Kikwete katika hotuba yake ya kulizindua Bunge hilo, aliweka msimamo wake wazi kwamba muundo wa serikali tatu hauwezi kutekelezeka kwa kuwa serikali ya Muungano haitakuwa na mapato ya kuiendesha, hali inayoweza kusababisha Jeshi kuiangusha serikali.


Suala la muundo wa Muungano limeibua mjadala nchini pamoja na kusababisha mgawanyiko miongoni mwa Wajumbe wa Bunge la Katiba.
Wajumbe kutoka CCM wanatetea serikali mbili wakati wa kutoka upinzani na baadhi ya wawakilishi wa makundi na taasisi wanataka serikali tatu.


Ni kutokana na mgawanyiko huo Bunge hilo lililazimika kuziweka kiporo kanuni za 37 na 38 ambazo zinahusu utaratibu wa kura za kupitisha vifungu vya rasimu kama uwe wa kura ya siri au ya wazi.
Wajumbe wa CCM walitaka itumike kura ya wazi, msimamo ulioonyesha kwamba lengo lake lilikuwa ni la kuepusha wajumbe wake wasikisaliti chama hicho wakati wa kupigia kura muundo wa Muungano huku wajumbe wa upinzani na baaadhi kutoka makundi, asasi wakitaka kura ya siri.


Hata hivyo, kanuni hizo zilipitishwa Ijumaa iliyopita baada ya Kamati ya Mashauriano kuamua zitumike kura zote, za wazi na siri na Bunge liliridhia.


CHANZO: NIPASHE
 
Si Lembeli tu, wapo wengi mno na wengine wapo ndani ya Serikali ila hawana nafasi ya kuipinga CCM waziwazi.
 
Wote tutakufa lakini historia yetu itatuhukumu.Tanganyika kwanza vyama baadae
 
Leo ni tarehe 1 mwezi wa 4
so usiamini kila kinachoandikwa kwenye magazeti

Magazeti zaidi ya mawili hayawezi kuandika jambo moja linalofanana kama ni suala la hii sikukuu.
 
- Yale yale kama upo kwenye chama hakina msimamo kama wako si utoke tu uende kule kwenye chama chenye msimamo kama wako, Rais Reagan alikuwa Democrat mpaka mwaka 1962 alipoona hawana msimamo kama wake akaingia Republican sasa hawa kwa nini wanapiga piga kelele ndani ya chama ambacho hakina msimamo kama wao watoke tu waone kama CCM itayumba!!

Le Mutuz

hakuna, huo sio msimamo wa wana ccm bali msimamo wa nec ambayo imebakiza muda mdogo kuondoka. na sana zaidi ni msimamo wa ccm znz.
 
Hii safi sana. Tunahitaji wajumbe wengine 10 wa CCM wenye independent mind kama Mh. Lembeli ili kufanya mabadiliko kwa kuwaondoa uoga hao wengine ambao wanajali maslahi binafsi (yaani kuganga njaa) kuliko kueleza kile ambacho dhamira yao inachokiamini.
 
Wanao ikataa Tanganyika ni watu kama Lusinde na Komba ambao hata ukiwauliza sababu watakuambia "sii mwenyekiti kasema?" Hawa wengine hawajui hata kwa nini wapinzani walikuwa wanapigia chapua kura za siri? Ilikuwa kuwaokoa hao CCM waoga wa maamuzi.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Khaa!!! Huyu kaona ameanza kueksipaya sisiem na anatafuta fursa sidiem. Akaidanganye mibavicha huko
 
mabadiliko ya kweli taifa hli yatakuja baada ya watu type ya kina lembeli kuzaliwa wengi, na watu type ya sendeka kufa wengi...
kwel kabisa mkuu wakifa wakina mwigulu,lusinde,sendeka wengi itakuwa poa sana
 
Nani aliyemkataza kudai Tanganyika, yeye ni mbunge ana ana haki ya kudai akionacho sawa, lakini akijengee hoja si vitisho.
 
Hivi katiba inayotengenezwa ni ya CCM au Watanzania wote?!

- TOO BAD Katiba inatengezwa kwa mujibu wa sheria zilizopo sasa ambazo zipo wazi kwamba chama kinachotawala ndio chenye nafasi kubwa ya kuandika Sheria na sio vinginevyo!!

Le Mutuz
 
hakuna, huo sio msimamo wa wana ccm bali msimamo wa nec ambayo imebakiza muda mdogo kuondoka. na sana zaidi ni msimamo wa ccm znz.

- Kaka NEC ndio Mkutano wa mwisho wa CCM wa kuamua msimamo wa CCM kama Lembeli hautaki ajiondoe mara moja kwenye chama ambachi hakikidhi mahitaji yake!1

Le Mutuz
 
Back
Top Bottom