Lembeli: CCM si Mama yangu

Lembeli: CCM si Mama yangu

baba lebeli tunajua mungu atawalipa tu baada ya kazi ngumu hii ya kutusemea sisi wanyonge tusio na sauti baba wewe ni musa utashinda
 
Kashakusanya hela za kumtosha? Uchumia tumbo tu ndio unawapoza hawa watu
 
Mbunge wa kahama
james lembeli amesema CCM si mama yake Yupo tayari kuidai Tanganyika popote ndo mana alikua anataka kura ya siri ili kulinda haki ya uhuru wa mtu
adai ata nyerere alisema usipoipata democrasia ndani ya CCM utaipata popote pale
chanzo: magazeti leo

- Yale yale kama upo kwenye chama hakina msimamo kama wako si utoke tu uende kule kwenye chama chenye msimamo kama wako, Rais Reagan alikuwa Democrat mpaka mwaka 1962 alipoona hawana msimamo kama wake akaingia Republican sasa hawa kwa nini wanapiga piga kelele ndani ya chama ambacho hakina msimamo kama wao watoke tu waone kama CCM itayumba!!

Le Mutuz
 
wabunge wengi wa ccm mpaka kikwete wana serikali tatu mioyoni mwao.wanakuwa wanafiki kuipinga midomoni mwao.take it from me
 
Leo ni tarehe 1 mwezi wa 4
so usiamini kila kinachoandikwa kwenye magazeti
 
Wabunge wa kutoka tanganyika unganeni na lembeli kuidai tanganyika yetu! Watanganyika wenzangu mbunge kama huyu ni wa kuenziwa kwelikweli! Viva lembeli, tanganyika kwanza! Vyama baadae!
 
sawa kabisa....naamini wajembe wengi watabadili misimamo yao na hatimaye watasema liwalo na liwe..... tunawasubiri kwa hamu kubwa...... FILIKUMJOMBE NAE VIPI? CCM bado ni MAMA YAKE? mtizamo tuu.... ila seriali moja ndo bora zaidi

WABUNGE WATANGANYIKA AMKENI KATIKA UKWELI...INAKERA KUTUETEA HOJA ZA KUBURUZWA...
 
- Yale yale kama upo kwenye chama hakina msimamo kama wako si utoke tu uende kule kwenye chama chenye msimamo kama wako, Rais Reagan alikuwa Democrat mpaka mwaka 1962 alipoona hawana msimamo kama wake akaingia Republican sasa hawa kwa nini wanapiga piga kelele ndani ya chama ambacho hakina msimamo kama wao watoke tu waone kama CCM itayumba!!

Le Mutuz

Hivi katiba inayotengenezwa ni ya CCM au Watanzania wote?!
 
Kwa hiyo ina maana baada ya kauli yake CCM ilijirekebisha ndiyo maana mpaka Mwl. Nyerere anafariki hakurudisha kadi ya CCM!.

Huyu Mwl. Nyerere kama kweli CCM haikuwa Baba na Mama yake, kulikuwa na umuhimu gani wa yeye mpaka kushinikiza watu wajiuzuru, kuandika kitabu kuhusu hao watu na kutoa machozi kwenye mikutano ya ndani ya chama.

Kama CCM haikuwa Baba na Mama yake, mazingira yanaonyesha asingejisumbua kwa kiasi hicho, bali angewapa kadi yao hao viongozi waliokuwa wanadhani CCM haikuwa Baba na Mama yao.

Toka lini kupingana kwa mitazamo ikawa ni kufukuzana ndani ya vyama au ndiyo yale yale ya wanasiasa wa bongo katika kutafuta umaarufu na kupigana vijembe kimakundi ya kuusaka Urais.

I wonder, if this is not A conflict of interest!. Kwa siasa za Tanzania kila kitu kinawezekana.


attachment.php
 

Attachments

  • image.jpg
    image.jpg
    122.9 KB · Views: 678
Asante mzee Rembel kusaidia chama chetu ccm ili kiongoze harakati za mabadiliko.tulioko vijijini tunasononeka sana tuonapo viongozi wetu wa CCM wanaposhindwa kujenga chama na kuongoza mabadiliko na kuviachia vyama vya upinzani vikijenga hoja nzito mpaka tumashindwa kumini. Kwa nini chama chetu kinashindwa kusoma alama za nyakati na kuongoza mabadiliko na kuendelea kushikilia misimamo ya kale! Hongera J Rembel.Kangi Lugora.na Deo Filikunjombe kwa kusaidia chama chetu kwenda na wakati.
 
Baaada ya maneno ya Lembeli naamin wapo wengi watakaojitoka ndani ya CCM na kusema hadharan kua wanataka serikali tatu...tusubiri kidogo tuu..
 
Back
Top Bottom