Lema, umewapa nini wana-Arusha?

Lema, umewapa nini wana-Arusha?

Kuna kipindi niliwahi kusema siasa za Arusha wanaozijua ni wana-Arusha wenyewe kwamaana wananchi hao hao wanaeleza kuwa wanakabiliwa na matatizo lukuki kwasababu hakuna utendaji mzuri wa Mbunge wao.

Jambo ambalo linasifiwa na wananchi ni kuhusiana na suala la machinga, angalau kidogo wanaeleza kuwa wamefanikiwa kukaribia kutimiza malengo yao (aliwapigania kwa kiasi flani kwamaana wkuna watu wanaouza bidhaa kwa kujihami ili wasije wakanyang'anywa mali zao) Pia angalia kilio cha akina Mama kufukuzwa nje ya Soko la Kilombero, Soko Kuu walipokuwa wanafanyia shughuli zao wanavyonyanyaswa na mamlaka husika hadi sasa, Mbunge halioni hili ili wafanyabiashara wadogo wafanye kazi zao kwa uhuru?

Ilifikia kipindi wananachi walimchukia Lema na baadhi ya viongozi wa Chadema kutokana na hali ya usalama jinsi ilivyokuwa na mauaji yaliyotokea, sasa tujiulize kuwa walioathiriwa na vurugu za maandamano, mabomu na lile tukio la mkutano wa Chadema Soweto, sasa hivi wamesaidiwaje na Mbunge tukiachilia nafasi ya Chama?

Nimefikiria hayo machache tu, mengi wanayo wana-Arusha.
mkuu Mbunge ni mwakilishi wa wananchi na sio kama unavyodhani wewe.Kazi zake soma katika utaona.Vijana wa arusha ni vijana ambao wanajua wajibu wa mbunge wao
 
Kati ya mji ambao haukustahili kuwa jiji ni Arusha yani hakuna mji wenye barabara nyembamba kama Arusha hasa hile ya Moshi -Arusha au Dar -Arusha! Kwakweli siasa zina haribu mji huo na kuuchelewesha!
 
mimi nilikuwa Nairobi nimelala ARUSHA sikutatu nimerudi jana usiku,nipo Dar, hamna lolote,taa zilizowekwa bararabarani haziwaki,ahadi zote hamna kitu,Lema kama unampenda muulize yule Meya waliemkataa na kusababisha maafa kwanini leo wanafanyanae kazi.alisababisha mauaji ya kijinga kabisa,Wajane na Yatima wamewaacha kwenye mataa.

Chalii yangu usiwe unapita chuga usiku kuangalia taa, njoo uishi Chuga.
Kama unapenda taa nenda maeneo ya kirumba usiku itaona mabugando kibao ukiamka asubuhi utafurahi
 
Lema ni Alfa na Omega wa jimbo la Arusha..

tumemkubali na kwa pamoja tutajenga Arusha...

Lema hana mchango wowote kwenye mji wa Arusha! Muda mwingine huwa naamini kuwa wana Arusha wanao mchagua Lema wana matatizo kabisa ya kufikiri maana hata ukiwauliza Lema kawafanyia nini hawana la kufanya.
 
ni aibu kwa mtu unaejiita mwanasheria kutumika kiasi hiki. hii ni afadhali hata ya condom.

Nipo hapa Arusha kuhudhuria Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika. Nimefika hapa jana na nitakuwa hapa hadi Jumapili. Naomba kukuuliza Godbless Jonathan Lema,Mbunge wa Arusha Mjini tulipo Mawakili kwa sasa.

Lema,leo tuambie hapa nini hasa kinachowafanya wana-Arusha wakuamini na kukuheshimu? Wananchi wako wanakuimba kwa mema kwelikweli.

Hata sisi Wasomi wa sheria tunajiona tuko huru na salama kwenye jimbo lako. Lema kiukweli ameiteka na kuikamata Arusha.
 
Kuna kipindi niliwahi kusema siasa za Arusha wanaozijua ni wana-Arusha wenyewe kwamaana wananchi hao hao wanaeleza kuwa wanakabiliwa na matatizo lukuki kwasababu hakuna utendaji mzuri wa Mbunge wao.

Jambo ambalo linasifiwa na wananchi ni kuhusiana na suala la machinga, angalau kidogo wanaeleza kuwa wamefanikiwa kukaribia kutimiza malengo yao (aliwapigania kwa kiasi flani kwamaana wkuna watu wanaouza bidhaa kwa kujihami ili wasije wakanyang'anywa mali zao) Pia angalia kilio cha akina Mama kufukuzwa nje ya Soko la Kilombero, Soko Kuu walipokuwa wanafanyia shughuli zao wanavyonyanyaswa na mamlaka husika hadi sasa, Mbunge halioni hili ili wafanyabiashara wadogo wafanye kazi zao kwa uhuru?

Ilifikia kipindi wananachi walimchukia Lema na baadhi ya viongozi wa Chadema kutokana na hali ya usalama jinsi ilivyokuwa na mauaji yaliyotokea, sasa tujiulize kuwa walioathiriwa na vurugu za maandamano, mabomu na lile tukio la mkutano wa Chadema Soweto, sasa hivi wamesaidiwaje na Mbunge tukiachilia nafasi ya Chama?

Nimefikiria hayo machache tu, mengi wanayo wana-Arusha.

Labda nikujuze kitu kimoja tu, Hapa Chuga watu ni waelewa wa kila kinachofanywa na serikali yako ya mabavu.

Ni lini Lema alileta bomu akawarushia wananchi wake? Jibu unalo na wanachuga tunaelewa vizuri sana.

Ni lini Lema aliwafukuza kina mama wa kilombero au soko kuu, wamama kule boma road, india road, goliondoi road n.k? Jibu unalo na wanachuga tunajua.

Soko la kilombero limegharimu hela nyingi ambazo siyo kweli.

Sokokuu tangia limejengwa kumefanyika upanuzi mdogo sana tena wa kitoto wakati mahitaji yameongezeka maradufu lkn hakuna jitihada zilizochukuliwa na halmashauri ya jiji zaidi ya kutafuna hela.
Lema aliwaambia wamachinga na wamama wasibugudhiwe, cha kufanya ni kuwatafutia sehemu yao Ya kufanya biashara.

Lilipokuwa soko original la kilombero mafisadi mkaja mkalimega mkaanza sijui ujenzi gani, Lema aliwaambia machinga na wamama eneo lenu la biashara ni hili hapa, watu wakajipangia sehemu zao mbona mlinywea?
Holo eneo ndiyo TIB wameridhika kuja kutoa mkopo wa kujenga soko pale. Sasa hiyo ni kidogo tu.

Kikubwa ni kwamba Lema katupa wigo mpana zaidi wa kuweza kufikiri, kujua na kukabiliana na maisha haya mnayotunyonga nayo.

Kumbuka:Mbunge hakupi hela, dawa, maji ya azam, barabara, hakupelekei mtoto shule. Mbunge anaisimamia serikali itoe na kuboresha huduma zote za jamii ktk eneo lake.
Nitaanza shule hapa nadhani
 
mahali popote ambapo kuna kiongozi anayeziba mirija ya wizi lazima achukiwe naamini hivyo kama lema ni kiongozi wa aina hiyo lazima atapata upinzani wa juu kwa wale waliozoea ubadhirifu

If that is the case gooooo lema
 
mahali popote ambapo kuna kiongozi anayeziba mirija ya wizi lazima achukiwe naamini hivyo kama lema ni kiongozi wa aina hiyo lazima atapata upinzani wa juu kwa wale waliozoea ubadhirifu

If that is the case gooooo lema

Ukizuia ilani ya CCM(wizi ) lazima wakuchukie
 
ni aibu kwa mtu unaejiita mwanasheria kutumika kiasi hiki. hii ni afadhali hata ya condom.

Huyu jamaa kutumika ni kawaida yake ukija hapa dar nenda pale mlimani au pale pwani wanamjua sana kwa kutumika kwa kupewa hata elfu kumi tu.
 
Huyu jamaa kutumika ni kawaida yake ukija hapa dar nenda pale mlimani au pale pwani wanamjua sana kwa kutumika kwa kupewa hata elfu kumi tu.

Dada gsu ungekuwa na uwezo wa kujenga hoja na msimamo kama mimi sijui ingekuwaje. Nikirudi dar nitakutafuta nikufundishe jambo
 
Last edited by a moderator:
Huyu jamaa kutumika ni kawaida yake ukija hapa dar nenda pale mlimani au pale pwani wanamjua sana kwa kutumika kwa kupewa hata elfu kumi tu.
nimemshangaa sana huyo jamaa mwanasheria hewa. hajui kuwa lema zaidi ya umaarufu wake pale arusha hasa wa kuhamasisha fujo hamna chochote cha maana alichokifanya kwa machalii wale.
hizi njaa zitatupeleka pabaya kwa kweli.
 
MUSSA ALLAN,mimi ni mwanasheria kweli na nipo hapa Arusha. Kama unajiamini tutafutane tujadiline kuhusu nchi yetu hata kwa dakika tano. Nitaondoka Jumapili
 
Last edited by a moderator:
Kati ya mji ambao haukustahili kuwa jiji ni Arusha yani hakuna mji wenye barabara nyembamba kama Arusha hasa hile ya Moshi -Arusha au Dar -Arusha! Kwakweli siasa zina haribu mji huo na kuuchelewesha!
Hizo barabara nyembamba alitengeneza Lema?
 
Lema hana mchango wowote kwenye mji wa Arusha! Muda mwingine huwa naamini kuwa wana Arusha wanao mchagua Lema wana matatizo kabisa ya kufikiri maana hata ukiwauliza Lema kawafanyia nini hawana la kufanya.

Katusaidia kuiondoa ccm arusha kwa sasa nimekuwa wapinzani mwaka huu tutawakimbiza kabisa Arusha
 
nimemshangaa sana huyo jamaa mwanasheria hewa. hajui kuwa lema zaidi ya umaarufu wake pale arusha hasa wa kuhamasisha fujo hamna chochote cha maana alichokifanya kwa machalii wale.
hizi njaa zitatupeleka pabaya kwa kweli.

Mkuu Abunuas, wewe jenga majungu tu. Wewe ni kati ya waoga wa ID feki. Mimi si mtu wa mchezo ndugu. Endelea kujidanganya na kujificha
 
Last edited by a moderator:
Mwanasheria Mwenye akili timamu siku zote hawezi kuongea kama ww hususani kwnyr jimbo lenye changamoto kama hilo .

Umeongea as if kuna mtu kakupa namna ya kuandika.
Maneno yako yamejaa ushabaki na kujipendekeza .

umechukia mno bila sababu za msingi.
 
Back
Top Bottom