Kuna kipindi niliwahi kusema siasa za Arusha wanaozijua ni wana-Arusha wenyewe kwamaana wananchi hao hao wanaeleza kuwa wanakabiliwa na matatizo lukuki kwasababu hakuna utendaji mzuri wa Mbunge wao.
Jambo ambalo linasifiwa na wananchi ni kuhusiana na suala la machinga, angalau kidogo wanaeleza kuwa wamefanikiwa kukaribia kutimiza malengo yao (aliwapigania kwa kiasi flani kwamaana wkuna watu wanaouza bidhaa kwa kujihami ili wasije wakanyang'anywa mali zao) Pia angalia kilio cha akina Mama kufukuzwa nje ya Soko la Kilombero, Soko Kuu walipokuwa wanafanyia shughuli zao wanavyonyanyaswa na mamlaka husika hadi sasa, Mbunge halioni hili ili wafanyabiashara wadogo wafanye kazi zao kwa uhuru?
Ilifikia kipindi wananachi walimchukia Lema na baadhi ya viongozi wa Chadema kutokana na hali ya usalama jinsi ilivyokuwa na mauaji yaliyotokea, sasa tujiulize kuwa walioathiriwa na vurugu za maandamano, mabomu na lile tukio la mkutano wa Chadema Soweto, sasa hivi wamesaidiwaje na Mbunge tukiachilia nafasi ya Chama?
Nimefikiria hayo machache tu, mengi wanayo wana-Arusha.