Lema ukicheza utapoteza Arusha mjini for good

Lema ukicheza utapoteza Arusha mjini for good

Dr. Slaa ni mtu mzima na atumie hekima na busara kulishughulikia hili suala haraka iwezekanavyo na kwa manufaa ya wananchi waliowachagua hawa madiwani. Tutaendelea kumheshimu Dr. Slaa kama atatuheshimu na kuelewa wale madiwani wana watu nyuma yao waliowachagua.

Sioni dhambi kukaa meza moja na CCM wakati huko bungeni mko na CCM na mnacheka nao. Sisi tuko nao pia huku mitaani, mahotelini, kwenye mabasi, kwenye nyumba za ibada n.k. Hawa ni wenzetu na tumetofautiana tu itikadi lakini hatuna uadui mkubwa kiasi hicho ambacho Lema anataka kuonyesha hapa Arusha. Ninamuomba Lema akue na aache mambo ya kuonyeshana ubabe ili tujenge nchi yetu kwani safari iliyoko mbele ni ndefu na kazi bado ni kubwa. Nitakuwa na uchungu mkubwa sana kama uzembe wa CDM utalifanya jimbo hili kurudi tena mikononi mwa CCM na mtakuwa mmepoteza sana credibility na support kwa jinsi ambayo itakuwa ngumu ku- reverse.
Kwenye nyekundu tukopamoja kabisa...
Kuhusu kukaa meza moja na CCM siyo tatizo kwa CHADEMA kwani CHADEMA ndiyo walikuwa wakitafuta mwafaka tatizo kubwa ni maamzi ya mwisho ya mwafaka huo..CHADEMA taifa wanasema hawakujua nini kinaendela lakini ukiongea na waliokuwa kwenye kamati ya mwafaka huo wanasema walikuwa wanapelekewa kila kilichokuwa kinaendelea na katibu alitoa mapendekezo yakiwemo 1. uchanguzi ufanyike upya 2. kugawana uongozi...hivyo waliokuwa kwenye kamati wanajiona kama waondiyo wana saritiwa na chama Taifa, Tukija kwenye ubabe wa Lema kama ulivyosema hapo juu binafsi sioni ubabe wa Lema hapo kwani alichokidai ilikuwa ni msimamo wa chama taifa na si kugawana madaraka na kama walibadiliaka basi inaelekea hakukuwa na mawasilianao ya Lema na madiwani waliokuwa kwenye kamati ya mwafaka.........Naomba nimuombe Dr. Slaa alifanyie kazi swala hili madiwa tuliwachagua sisi na mbunge tulimchangua sisi, tunakuwa kwenye wakati mungu kutenganisha watu hawa labda tuhakikishiwe kuwa makosa ya huyu ni a,b,c... hatutasita kuchukua maamzi...
 
Nimesoma hii thread nikabaki najiuliza kama kweli mwandishi ni mkazi wa Arusha au ni mtetezi tu wa Mallah. Swala kubwa hapa ni namna walivyoingia muafaka na muafaka wenyewe! Wameingia muafaka ambao haujibu maswali yetu sisi wakazi wa Arusha ambao tupo tunawatunza ndugu zetu waliopigwa risasi na polisi tar 5/1. Nimeongea na Diwani aliyekuwa kwenye kamati ya muafaka na amenihakikishia kuwa makubaliano yao sio yalioletwa kusainiwa. Walipokataa na kueleza hilo wenzao wakawageukia. Kwanini tusidhani ni rushwa ilitembea. Hapa hakuna wananchi wanaoukubali huo muafaka feki. Mi nipo Arusha na hata huko Kimandolu hawaukubali na wanatilia mashaka kwamba rushwa imetembea. Ndio maana hata sherehe ya kupongeza muafaka ilikosa watu. Lazima chama kifuate taratibu na kama watu hawataki hilo waondolewe. Na Lema kama akiendekeza ujinga wa akina Mallah ndio atalipoteza jimbo maana hatutamchagua tena.

Mimi ni mkazi wa Arusha ila wewe ndio siyo au labda uko ktk ya mji kwenye magorofa na wahindi.Ukiwasikiliza hawa madiwani wanasema Lema alikuwa well informed kuhusu process zote hadi kufikia muafaka na alipoona amefanya kosa bila kuwafahamisha mabosi wake aka retreat peke yake. Unatakiwa basi ukiretreat unyamaze ila yeye alifanya hivyo na kuwageuka wenzake na mbaya zaidi akijifanya haelewi chochote. Hatuwezi kubisha hayo mpaka hizi pande mbili zitakapokutanishwa na kusikilizwa.
Kinachoonekana hapa zaidi ni Lema kutotaka kushuka akifikiri ushujaa utakwisha wakati sometime unatakiwa ushuke na kukubali kwa kutokubaliana ili ushujaa uongezeke . Hivi Lema angekuwa Mandela baada ya kuachiwa then akawa rais unafikiri angewafanyia nini makaburu? Mandela alikubali yaishe na kuwasamehe makaburu na kuamua kufanya nao kazi ingawaje walimbagua na kumtesa na hili ndilo lililompa umaarufu na heshima kubwa duniani mwote.
 
Madiwani wameisha sema kama hawawajui basi safari hii watawajua na hasa hasa Lema na hawako tayari kutumiwa kwa manufaa ya wachache yakujitafutia umaarufu wa kisiasa, Lema safari hii ameingia choo cha kike
kama ni mawazo ya kupimana mabavu kama uvccm basi upande wa Lema bado unaungwa mkono na watu wengi..juzi kulifanyika maandamano ya kuunga mkono mwafaka unajua kulikuwa na watu wangapi...kwataarifa yako ni 57 mpaka mkuchika akaingia mtini...lakini CHADEMA sidhani kama wataendelea kutunishiana msuli kama style ya magamba....
 
mkuu naunga mkono hoja 100% Lema analeta bange na uhuni wake katika siasa sisi kama wakazi wa arusha tushaanza kuwa na wasiwasi wake, kwanza sisi wakazi wa kaloleni tulimchaguwa yeye baada ya diwani wetu kutuomba sana tumchague lakini sisi tunamjua tangu yuko TLP alishawahi kuongwa pesa ili ccm ishinde,chondechonde Lema eshimu madiwani wetu ukijua kwmba wewe ni source ya vurugu za arusha, ni muda muafaka wa wewe kutimiza ahdi zako ulizotuahidi na sio kulumbana na madiwani wetu Arusha sio Udom bwana ambako unashawishi watoto wagome
Acha kutulisha maneno Kama ni wasiwasi tafadhali utaje kwa nafsi yako wewe Kama wewe sio kutuchanganya.Kama unao ushahidi kuwa alihongwa alipokuwa TLP anika hapa adharani acha habari zako za uchochoroni huko.Unamtaka Lema atimize wajibu upi ulioshindwa kutimizwa na ccm miaka 50 sasa au hadha ya umeme tu yenyewe hauioni!?
 
Mimi ni mkazi wa Arusha ila wewe ndio siyo au labda uko ktk ya mji kwenye magorofa na wahindi.Ukiwasikiliza hawa madiwani wanasema Lema alikuwa well informed kuhusu process zote hadi kufikia muafaka na alipoona amefanya kosa bila kuwafahamisha mabosi wake aka retreat peke yake. Unatakiwa basi ukiretreat unyamaze ila yeye alifanya hivyo na kuwageuka wenzake na mbaya zaidi akijifanya haelewi chochote. Hatuwezi kubisha hayo mpaka hizi pande mbili zitakapokutanishwa na kusikilizwa.
Kinachoonekana hapa zaidi ni Lema kutotaka kushuka akifikiri ushujaa utakwisha wakati sometime unatakiwa ushuke na kukubali kwa kutokubaliana ili ushujaa uongezeke . Hivi Lema angekuwa Mandela baada ya kuachiwa then akawa rais unafikiri angewafanyia nini makaburu? Mandela alikubali yaishe na kuwasamehe makaburu na kuamua kufanya nao kazi ingawaje walimbagua na kumtesa na hili ndilo lililompa umaarufu na heshima kubwa duniani mwote.
na sita kusema alikuwa anajua kuwa wanagawana madaraka...sikuchache kabla ya bunge la budget kuanza lema aliitisha mkutano pale karibu St. Thomas Hosp wakiwepo madiwani na baadhi yao ndiyo waliokuwepo kwenye kamati ya muafaka hapa namzungumzia malla na rasta diwani wa kaloleni..Lema alipa kutokukubali kupewa madaraka kama suruhu hivyo haiingii akili wiki moja baadae anakubali kitu alicho kikataa kata...na akasema hata koo za Lema na Lyimo(Meya) zilijaribu kuwapatanisha Lema alikataa kabisa akitaka uchanguzi urudiwe
 
naunga mkono hoja,migogoro haifai,makubaliano yamefikiwa yapewe baraka na cdm makao makuu,shughuli za maendeleo ziendelee
 
mkuu naunga mkono hoja 100% Lema analeta bange na uhuni wake katika siasa sisi kama wakazi wa arusha tushaanza kuwa na wasiwasi wake, kwanza sisi wakazi wa kaloleni tulimchaguwa yeye baada ya diwani wetu kutuomba sana tumchague lakini sisi tunamjua tangu yuko TLP alishawahi kuongwa pesa ili ccm ishinde,chondechonde Lema eshimu madiwani wetu ukijua kwmba wewe ni source ya vurugu za arusha, ni muda muafaka wa wewe kutimiza ahdi zako ulizotuahidi na sio kulumbana na madiwani wetu Arusha sio Udom bwana ambako unashawishi watoto wagome
Naomba unijibu maswali 3. halafu nitakwekueleza a -z juu ya sakata hilo..
1. Mlalamikaji wa kesi iliyofutwa alikuwa nani?
2.TLP inadaiwa kiasi gani kwa kufuta kesi hiyo
3. Lema alihongwa kiasi gani
 
Naomba kujiburudisha na topic hii. Mnaoi support hamuoni kuwa hakuna haja ya malumbano , ninyi ni kuwataka hao madiwani wafanye kazi kinachowazuia wao nini, kama ni kamati kuu basi waisikilize kamati kuu. kama hawana haja na kamati kuu waendelee mbele. Vilevile hili jambo linakuzwa na wanamagamba ionekane CDM kuna mgogoro, si sawa kabisa kulinganisha TLP, NCCR na CDM, hawa walikuwa na mgogoro ndani ya uongozi mkuu, hapa ni mgogoro wa taratibu zimefuatwa? na kama ndio ziwekwe hadharani sio maneno matupu. Na pia kama watu wa Arusha mko nyuma ya madiwani wenu waambieni wajiuzulu muwachague tena kwa tiketi ya chama kingine, si imetokea kwa Mbunge wa Maswa na Kafulila? msipigizane kelele na Dr.
Mkuu, mimi binafsi ni wana-CHADEMA...swala siyo kuwaambia wahamie chama kiingine halafu tuwachangue kupitia chama hicho bali tunataka kujua ukweli kama wamekula rushwa tutawachomea moto hata vibanda vyao maana haiwezekani tuwasaidie kwa hari na mali kipindi cha kampeni na siku ya kura halafu miezi 7 baadae watutende....yaani naimanisha kuwafukuza peke yake haitoshi...
 
Aisee mwanakwetu umenigusa hasa. Jana nilisikitika sana nilipoangalia TV kumbe hawa madiwani wetu bado hawajaanza kazi. Barabara walizoahidi kutengeneza ziko taabani na ahadi nyingine nyingi bado hata kuanza kuzitendea kazi bado. Wananchi ni kweli tumechoka kusikia magomvi na sasa tunataka kusikia mipango na mikakati ya utekelezaji. La sivyo tutawaweka kiporo hadi 2015 tuashangaze CDM tuwape CUF nao wajaribu.
Mkuu, kuna barabara moja ya kwenda Ngusero ni mahandaki lakini diwani wa kata hiyo ni kutoka CCM anagalau barabara ya kwenda sokoni one ni nzuri kiasi lakini diwani wake ni upinzani...na ili diwani aweze kufanikiwa inatakiwa wenyeviti wa vitongoji wawe-chama chake vingine watakukwamisha kwasababu huwezi pitisha kitu bila wao na hapa Arusha wenyeviti wa vitongoji wengi ni CCM...
 
naunga mkono hoja,migogoro haifai,makubaliano yamefikiwa yapewe baraka na cdm makao makuu,shughuli za maendeleo ziendelee
Ningependa sana kusikia mwafaka kama nilivyoshangilia siku nilipo sikia kuna mwafaka lakini niliishiwa nguvu baada ya kutokupata majibu mhimu juu ya upatikanaji wa mwafaka huo....
 
watu waliwachangua....
Kama waarusha wengi waliwachagua CCM,what makes you think CDM inaweza kuunda halmashauri bila kuwa na muafaka na CCM?
Wewe binafsi unafikiri CDM wanaweza kuunda halmashauri wao wenyewe bila kuungana na CCM?
 
Tukumbushane tena, kwamba "binti yako akiwa shule akaja nyumbani amebebeshwa mimba utamfanyaje?" kimsingi kwa maneno haya Mallah alishakiri kuwa wamefanya kosa kufikia muafaka bila kuihusisha kamati kuu ya chama. Lakini vile vile haipendezi kufuta kosa kwa kosa lingine. Wananchi waliowachagua wanahitaji maendeleo. Kamati kuu ya chama kwa upande wake inataka mapendekezo yake yatimizwe kwenye muafaka ule. Hapa ndipo ngoma inapokuwa ngumu kuchezwa. Ingependeza sana Dr. Slaa akatumia busara sana katika kutatua mgogoro wa Arusha kuliko ubabe. Ninachoona hapa ni kama Dr. Slaa kapewa maelezo ya upande moja akatoa tamko, bila kusikiliza upande wa pili. Kama ndiyo ukweli, in decision making atakuwa hajatenda haki. Cha kuangaliwa zaidi ni kwamba nini hatima ya malumbano haya in the near future.
 
na sita kusema alikuwa anajua kuwa wanagawana madaraka...sikuchache kabla ya bunge la budget kuanza lema aliitisha mkutano pale karibu St. Thomas Hosp wakiwepo madiwani na baadhi yao ndiyo waliokuwepo kwenye kamati ya muafaka hapa namzungumzia malla na rasta diwani wa kaloleni..Lema alipa kutokukubali kupewa madaraka kama suruhu hivyo haiingii akili wiki moja baadae anakubali kitu alicho kikataa kata...na akasema hata koo za Lema na Lyimo(Meya) zilijaribu kuwapatanisha Lema alikataa kabisa akitaka uchanguzi urudiwe

Inabidi Lema afike mahali akubali mambo mengine ila najua kusema uchaguzi wa meya urudiwe itakuwa vita nyingine hapa Arusha na wale walioshika mpini lazima watatuumiza. At least naona hata ku share madaraka tumewashinda CCM ingawaje sio kwa kiwango tulichotaka. Next time 2015 tujipange vizuri zaidi ili tuwaondoa wote tuongoze halmashauri kwani kuna shida gani kufanya hivyo. Lema ana resort kwenye option ambayo haitakuwa opted for na serikali ambayo inalo jeshi la polisi na kufanya huu mgogoro usimalizike na wala madiwani wasifanye kazi. Basi kama msimamo wa Lema ndio huo basi CDM taifa waamue in favour ya wangi wape na kama hilo nalo Lema hatalitaka basi akae na ubishi wake.
 
Inabidi Lema afike mahali akubali mambo mengine ila najua kusema uchaguzi wa meya urudiwe itakuwa vita nyingine hapa Arusha na wale walioshika mpini lazima watatuumiza. At least naona hata ku share madaraka tumewashinda CCM ingawaje sio kwa kiwango tulichotaka. Next time 2015 tujipange vizuri zaidi ili tuwaondoa wote tuongoze halmashauri kwani kuna shida gani kufanya hivyo. Lema ana resort kwenye option ambayo haitakuwa opted for na serikali ambayo inalo jeshi la polisi na kufanya huu mgogoro usimalizike na wala madiwani wasifanye kazi. Basi kama msimamo wa Lema ndio huo basi CDM taifa waamue in favour ya wangi wape na kama hilo nalo Lema hatalitaka basi akae na ubishi wake.
Huu ndiyo uonga ambao ndiyo unalitafuna taifa hili niliongea na Kivuyo nae aliongea kama ulivyo shauri...lakini nikuulize hivi leo ukawaita watu wa Arusha ukawaelezea kilichofanyika yaani sababu mpaka mwafaka kupatikana unaamini wataunga mkono mwafaka?...
 
Tukumbushane tena, kwamba "binti yako akiwa shule akaja nyumbani amebebeshwa mimba utamfanyaje?" kimsingi kwa maneno haya Mallah alishakiri kuwa wamefanya kosa kufikia muafaka bila kuihusisha kamati kuu ya chama. Lakini vile vile haipendezi kufuta kosa kwa kosa lingine. Wananchi waliowachagua wanahitaji maendeleo. Kamati kuu ya chama kwa upande wake inataka mapendekezo yake yatimizwe kwenye muafaka ule. Hapa ndipo ngoma inapokuwa ngumu kuchezwa. Ingependeza sana Dr. Slaa akatumia busara sana katika kutatua mgogoro wa Arusha kuliko ubabe. Ninachoona hapa ni kama Dr. Slaa kapewa maelezo ya upande moja akatoa tamko, bila kusikiliza upande wa pili. Kama ndiyo ukweli, in decision making atakuwa hajatenda haki. Cha kuangaliwa zaidi ni kwamba nini hatima ya malumbano haya in the near future.
Kuna baadhi ya madiwa waliitwa Dar(makao makuu) lakini nilishangaa kuwaona mitaani....Busara zitumike kwa pande zote mbili yaani uongozi taifa na madiwani tena ingekuwa vizuri kuwa kutanisha.....
 
Hawezi kwenda CCM kwani huku ni kuwalisha wananchi matapishi kwani bado hatujasahau aliyotufanyia Lawrence Hedi wa CCM aliyekuwa Meya ya Manisapaa ya ARusha . Mkakati ni kusonga mbele na siyo kurudi nyuma kuvaa magamba tena. Tayari Magamba walishapata F na alishapewa fursa nyingi za ku-resit bado akashindwa.

Take it from me: akienda CUF, TLP, NCCR....hiyo kata tunaichukua kilaiini. Subiri tuone mwisho, utakumbuka hili jibu.
 
Back
Top Bottom