Lema ukicheza utapoteza Arusha mjini for good

Maridhiano ya ARUSHA ni batili cdm taifa haiwezi kuyaridhia.Kama swala ni wanainchi na madiwani wao inakuwaje hao madiwani waliomba at first CDM makao makuu mpaka ikaandaa maandamano?
Marytina umenena sina la kuongeza, chama kibaki na hadhi hata jimbo likipotea
 
Madiwani wameisha sema kama hawawajui basi safari hii watawajua na hasa hasa Lema na hawako tayari kutumiwa kwa manufaa ya wachache yakujitafutia umaarufu wa kisiasa, Lema safari hii ameingia choo cha kike
Si ni hawa madiwani waliotumbua macho noteli Safari wakashindwa kwenda ukumbi wa manispaa kusheherekea sherehe ya mwafaka ,si ni hawa walimuacha Chiligati akiishia kwenda Shinyanga badala ya kuwa mgeni rasmi, Madiwani wameingia kwenye mtego wa CCM,na hawatachomoka,inaonyesha walikuwa CDM kwa majaliwa tuu lakini waumini wa chama hicho,madiwani wanatishia chama kwa tuhuma ambazo hazipo hatari sana ,Taarifa iliyotolewa kwenye vyombo vya habari baada ya kamati haisemi walikura rusha hii inamaanisha chama kimewasafisha,sasa wao wanag'ang'ana eti wasafishwe wasafishwe mara ngapi madiwani wameamua kupambana na chama ,vizuri Chadema wakaliona hilo mapema waondoke salama kwa sababu hata wakisimama hawapiti
 
Limbukeni mkubwa wewe,kibaraka wa CCM,CDM hawapo kwa ajili ya kugawana vyeo wanachopigania ni haki itendeke na utaratibu wa sheria ufatwe mana utaratibu ulivunjwa wa kumtafuta meya,viongozi wengi wa Africa ni waroho wa madaraka ndiyo mana kila kukicha wanavunja sheria then wanalazimisha kugawana madaraka.Madiwani wa ARUSHA NI MAADUI WA HAKI NA UKWELI.
 
Naomba kujiburudisha na topic hii. Mnaoi support hamuoni kuwa hakuna haja ya malumbano , ninyi ni kuwataka hao madiwani wafanye kazi kinachowazuia wao nini, kama ni kamati kuu basi waisikilize kamati kuu. kama hawana haja na kamati kuu waendelee mbele. Vilevile hili jambo linakuzwa na wanamagamba ionekane CDM kuna mgogoro, si sawa kabisa kulinganisha TLP, NCCR na CDM, hawa walikuwa na mgogoro ndani ya uongozi mkuu, hapa ni mgogoro wa taratibu zimefuatwa? na kama ndio ziwekwe hadharani sio maneno matupu. Na pia kama watu wa Arusha mko nyuma ya madiwani wenu waambieni wajiuzulu muwachague tena kwa tiketi ya chama kingine, si imetokea kwa Mbunge wa Maswa na Kafulila? msipigizane kelele na Dr.
 
Nazungumza kama supporter mkubwa wa CHADEMA na niliyemchagua Godbless Lema kama mbunge wangu. Niko mjini na niko mobile sana huwa nazunguka katika kata kadhaa za hapa mjini. Wananchi wengi ukiwasikia wanasema lazima waonyeshe support kwa madiwani wao waliowachagua kutokana na uamuzi waliotangaza jana. Mambo ya kamati kuu ya CDM haimsaidii mwananchi wa Kata ya Kimandolu, Sekei, Kaloleni n.k. ambao wanachotaka ni maendeleo na si migogoro ambayo haimaliziki. Wananchi walio wengi including viongozi wa dini wanaunga mkono muafaka na dhamira safi ya madiwani ya kutaka kuendelea mbele katika kuwatumikia wananchi na kuachana na malumbano.

Kutokana na mgogoro huu Lema ameanza si tu kupoteza umaarufu bali hata ushawishi kwa wakazi wa manispaa ya Arusha. Wengi tunaanza kumwona yeye na CHADEMA taifa kama watu wanaotafuta mambo yao binafsi na si kuwatumikia waliowachagua.
Naomba wajue wananchi wamechoka na hakuna mtu yuko tena interested na mvutano ambao siyo tu hauna mwisho bali ambao hauchangii hata asilimia 1% ya maendeleo katika kata zao.
Madiwani wameshikamana na wananchi kuliko Kamati kuu ya CDM inavyofikiri na kama watakosea wakawafukuza hawa madiwani basi wajue wamepoteza jimbo la Arusha kwa sababu watu hawa hawa ndio waliompigia Lema kura na hawatakuwa tayari kumpigia tena 2015.

Watu wanataka iwepo way forward na wasahau ya nyuma tujenge manispaa yetu na siyo kila wakati kutaka kuonyeshana misuli ya kisiasa kana kwamba ndilo lengo kuu la kuingia madarakani.

Please Lema anza kushughulikia malengo makuu ya maendeleo kama mbunge kwa mustakabali wa watu waliokuchagua kinyume na hapo tutakuona uliingia kwenye ubunge kwa personally motivated agenda na si vinginevyo. Kama hautafanya kazi kwa matakwa ya wananchi ndugu yetu hatutakuwa na jinsi zaidi ya kumtafuta mtu atakayeweza kufanya hiyo kazi.

Lastly but not the least namuomba sana Dr. Slaa asiwatishe tishe madiwani tuliowachagua kwani hakuwachagua yeye na hii ni sawa na kututisha sisi tuliowachagua. Dr. Slaa ni mtu mzima na atumie hekima na busara kulishughulikia hili suala haraka iwezekanavyo na kwa manufaa ya wananchi waliowachagua hawa madiwani. Tutaendelea kumheshimu Dr. Slaa kama atatuheshimu na kuelewa wale madiwani wana watu nyuma yao waliowachagua.

Sioni dhambi kukaa meza moja na CCM wakati huko bungeni mko na CCM na mnacheka nao. Sisi tuko nao pia huku mitaani, mahotelini, kwenye mabasi, kwenye nyumba za ibada n.k. Hawa ni wenzetu na tumetofautiana tu itikadi lakini hatuna uadui mkubwa kiasi hicho ambacho Lema anataka kuonyesha hapa Arusha. Ninamuomba Lema akue na aache mambo ya kuonyeshana ubabe ili tujenge nchi yetu kwani safari iliyoko mbele ni ndefu na kazi bado ni kubwa. Nitakuwa na uchungu mkubwa sana kama uzembe wa CDM utalifanya jimbo hili kurudi tena mikononi mwa CCM na mtakuwa mmepoteza sana credibility na support kwa jinsi ambayo itakuwa ngumu ku- reverse.

Mungu Ibariki Tanzania

unachoongea ni kweli, Lema hashauriki hata kidogo maana hata wale machalii waliyompigania kwasasa kawatupa na kuanzisha kundi lingine la watu walizonazo wakati kipindi cha kampeni walimuita mwizi, kajisahau watu walitoa magari yao huku yeye akiwa hana kitu, watu walisimamisha magari yao kutofanya kazi ya utalii ili Lema ashinde kwakuwa waliamini anaendakusimamia ukweli.

kuhusu hili la madiwani nilimshauri Lema sana kuwa ARUSHA siyo CDM wamekuchagua wewe kwakuwa uliweza kuwashawishi kwahiyo kujifanya kuwa eti wewe unasikiliza chama taifa kinasema nini itakuja kukugharimu chukua maamuzi mapema. Lema alinibishia sana.

watu wanaopiga ujumbe huu na na kuuita ni wamamluki wao ndiyo mamluki kwakuwa hawataki kuambiwa ukweli
 
unachoongea ni kweli, Lema hashauriki hata kidogo maana hata wale machalii waliyompigania kwasasa kawatupa na kuanzisha kundi lingine la watu walizonazo wakati kipindi cha kampeni walimuita mwizi, kajisahau watu walitoa magari yao huku yeye akiwa hana kitu, watu walisimamisha magari yao kutofanya kazi ya utalii ili Lema ashinde kwakuwa waliamini anaendakusimamia ukweli.

kuhusu hili la madiwani nilimshauri Lema sana kuwa ARUSHA siyo CDM wamekuchagua wewe kwakuwa uliweza kuwashawishi kwahiyo kujifanya kuwa eti wewe unasikiliza chama taifa kinasema nini itakuja kukugharimu chukua maamuzi mapema. Lema alinibishia sana.

watu wanaopiga ujumbe huu na na kuuita ni wamamluki wao ndiyo mamluki kwakuwa hawataki kuambiwa ukweli
Acha uongo munaremba na kuchonga sana kama vile wananchi hatufuatilii mambo ya Arusha ,hata wiki haijapita wananchi wamekataa kwenda kusheherekea mwafaka,Wananchi wanashiriki shughuli zote zinazohusu mbunge wao ,mbona mumekazana mukiomba mkono udondoke muudake kama Fisi kuna mbunge anachaguliwa leo akitegemea kwamba atakuwa mbunge wa maisha cha munawatetea madiwani walio asi wamejipambanua kwamba hawako katika kufuata utaratibu wa chama chao Diwani anamyukana katibu mkuu wa chama chake halafu unatuambua utumbo hapo
 
Acheni vitisho. Suala hapa la msingi ni lazima CDM wafuate kanuni na sera za chama, wakienda kwa mwendo wa kuwafurahisha madiwani na wananchi ndio kwanza watadharaulika. HAO MADIWANI WAFUKUZWE KABISA KWENYE CHAMA, HAWAWEZI WAKABISHANA NA KAMATI KUU YA CHAMA WAKATI HATA HUO UDIWANI WENYEWE WAMEUPATA KWA KUWA WANACHAMA WA CDM. Dr Slaa msipoteze muda waondoeni haraka kabla mambo hayajaharibika. Maendeleo ya Arusha yatakuja tu, after all maendeleo ya TZ kwa ujumla yamechelewa sana.



Kwa wageni na wenyeji siasa za Arusha.
Je unafahamu Lema hakuwa wanazungumza na Diwani Malla na Diwani Bayo muda wote wa uchaguzi hadi walipowaomba wazee wenye busara ili kutogawanya chama?Je unafahamu sio mara ya kwanza Lema kuwatishia kuwafukuza Malla na Bayo kwa kupitia shemeji yake mkuu wa chama?
Je unafahamu Bayo na Malla walishawahi kumpiga marufuku Lema kwenye mikutano yao ya kampeni?
Je unafahamu kuwa Lema alituhumiwa kuwaweka rafiki zake kuwapinga Diwani Malla,Diwani Bayo,Diwani Mpanda(Rasta) pamoja na Diwani Ngowi pamoja na kupitishwa na chama?Ni baada ya kuona maji yamezidi unga ndipo alipoenda mwezi wa mwisho kujidai kuwauza kwa wananchi?
Je unafahamu slaa alipokuja arusha alifikia kufanya mkutano kwa diwani Malla sio kwa kuwa alikuwa anahitaji msaada ila ni kwa kuwa ndiye alikuwa na nguvu zaidi kwa madiwani wote wa chadema?Je unafahamu Diwani Malla pekee aliipa chadema kura 5,000+..
Je unafahamu kuwa hawa ndio madiwani ambao walitumia fedha zao na nguvu zao binafsi kufanikisha kupata udiwani bila hata senti tano toka kwa Chadema?
Je unafahamu kata zote lema alifanya vikao vingi vya kampeni ikiwemo sombetini na mjini kati Chadema ilipoteza?
Je unafahamu Lema ndiye aliyevuruga mchakato wa kupata viti maalum arusha kinyume na utaratibu wa Chadema?
Je unafahamu kuna tuhuma rushwa za ngono zilitumika kwenye uchaguzi wa viti maalum?
Tafakari

 
Ndugu MwanaKwetu,

Nimekusoma.

Muafaka feki huo, kwanini hao madiwani hawakufauata utaratibu?

KWa Rushwa Hizo madiwani hao walizokula si itakuwa rahisi kushirikiana na Chama la magamba kula rushwa na kuuzwa kwa viwanja kama kawa??

No way, They must go these Blood Betrayors
Na hapo ndipo tatizo kubwa lilipo - rushwa. If proved, they must go, whatever the political consequences.
 
Kwa wageni na wenyeji siasa za Arusha.
Je unafahamu Lema hakuwa wanazungumza na Diwani Malla na Diwani Bayo muda wote wa uchaguzi hadi walipowaomba wazee wenye busara ili kutogawanya chama?Je unafahamu sio mara ya kwanza Lema kuwatishia kuwafukuza Malla na Bayo kwa kupitia shemeji yake mkuu wa chama?
Je unafahamu Bayo na Malla walishawahi kumpiga marufuku Lema kwenye mikutano yao ya kampeni?
Je unafahamu kuwa Lema alituhumiwa kuwaweka rafiki zake kuwapinga Diwani Malla,Diwani Bayo,Diwani Mpanda(Rasta) pamoja na Diwani Ngowi pamoja na kupitishwa na chama?Ni baada ya kuona maji yamezidi unga ndipo alipoenda mwezi wa mwisho kujidai kuwauza kwa wananchi?
Je unafahamu slaa alipokuja arusha alifikia kufanya mkutano kwa diwani Malla sio kwa kuwa alikuwa anahitaji msaada ila ni kwa kuwa ndiye alikuwa na nguvu zaidi kwa madiwani wote wa chadema?Je unafahamu Diwani Malla pekee aliipa chadema kura 5,000+..
Je unafahamu kuwa hawa ndio madiwani ambao walitumia fedha zao na nguvu zao binafsi kufanikisha kupata udiwani bila hata senti tano toka kwa Chadema?
Je unafahamu kata zote lema alifanya vikao vingi vya kampeni ikiwemo sombetini na mjini kati Chadema ilipoteza?
Je unafahamu Lema ndiye aliyevuruga mchakato wa kupata viti maalum arusha kinyume na utaratibu wa Chadema?
Je unafahamu kuna tuhuma rushwa za ngono zilitumika kwenye uchaguzi wa viti maalum?
Tafakari
Je unafahamu kuwa muafaka wa madiwani wa cdm na ccm umegubikwa na vitendo vya rushwa?
Tafakari zaidi
 
Nazungumza kama supporter mkubwa wa CHADEMA na niliyemchagua Godbless Lema kama mbunge wangu. Sioni dhambi kukaa meza moja na CCM wakati huko bungeni mko na CCM na mnacheka nao.
Mazingira ya kucheka na ccm huko bungeni yamegubikwa na rushwa?
Ndugu zangu tusicheke na rushwa. Kama madiwani wamechukua rushwa, then waondoke tu. Ni heri kupoteza jimbo na kata zote kuliko kuendekeza rushwa. Ukiendekeza rushwa leo eti usipoteze jimbo, utakuwa na tofauti gani na ccm?
 
Acheni vitisho. Suala hapa la msingi ni lazima CDM wafuate kanuni na sera za chama, wakienda kwa mwendo wa kuwafurahisha madiwani na wananchi ndio kwanza watadharaulika. HAO MADIWANI WAFUKUZWE KABISA KWENYE CHAMA, HAWAWEZI WAKABISHANA NA KAMATI KUU YA CHAMA WAKATI HATA HUO UDIWANI WENYEWE WAMEUPATA KWA KUWA WANACHAMA WA CDM. Dr Slaa msipoteze muda waondoeni haraka kabla mambo hayajaharibika. Maendeleo ya Arusha yatakuja tu, after all maendeleo ya TZ kwa ujumla yamechelewa sana.



Kwa wageni na wenyeji siasa za Arusha.
Je unafahamu Lema hakuwa wanazungumza na Diwani Malla na Diwani Bayo muda wote wa uchaguzi hadi walipowaomba wazee wenye busara ili kutogawanya chama?Je unafahamu sio mara ya kwanza Lema kuwatishia kuwafukuza Malla na Bayo kwa kupitia shemeji yake mkuu wa chama?
Je unafahamu Bayo na Malla walishawahi kumpiga marufuku Lema kwenye mikutano yao ya kampeni?
Je unafahamu kuwa Lema alituhumiwa kuwaweka rafiki zake kuwapinga Diwani Malla,Diwani Bayo,Diwani Mpanda(Rasta) pamoja na Diwani Ngowi pamoja na kupitishwa na chama?Ni baada ya kuona maji yamezidi unga ndipo alipoenda mwezi wa mwisho kujidai kuwauza kwa wananchi?
Je unafahamu slaa alipokuja arusha alifikia kufanya mkutano kwa diwani Malla sio kwa kuwa alikuwa anahitaji msaada ila ni kwa kuwa ndiye alikuwa na nguvu zaidi kwa madiwani wote wa chadema?Je unafahamu Diwani Malla pekee aliipa chadema kura 5,000+..
Je unafahamu kuwa hawa ndio madiwani ambao walitumia fedha zao na nguvu zao binafsi kufanikisha kupata udiwani bila hata senti tano toka kwa Chadema?
Je unafahamu kata zote lema alifanya vikao vingi vya kampeni ikiwemo sombetini na mjini kati Chadema ilipoteza?
Je unafahamu Lema ndiye aliyevuruga mchakato wa kupata viti maalum arusha kinyume na utaratibu wa Chadema?
Je unafahamu kuna tuhuma rushwa za ngono zilitumika kwenye uchaguzi wa viti maalum?
Tafakari

Nataka mkuu nikuamini kwa kiasi kikubwa kwa sababu Malla ninamfahamu na niko karibu na marafiki zake. Kama ulivyosema ni kweli Malla alipiga kampeni kwa gharama zake na alikuwa anatumia magari yake kama majukwaa siku zote za kampeni. Kwa hiyo huyu ni mwananchi mpenda watu wake na akajitoa kuwatumikia na nataka niamini anachopigania siyo kurudisha gharama kama watu wengi wanavyosema bali kutimiza ahadi alizotoa kwa wananchi wake.
 
kitendawili...
Hapo zamani za kale kulikuwa na mgombea wa urais toka chadema ambae alishindwa urais 2010.Mara baada ya kushindwa katangaza kutoutambua uchaguzi wa rais kwa kuwa ulichakachuliwa na usalama wa taifa.Pia aliamua kufanya maandamano nchi nzima ikifuatiwa na wabunge wa chadema kutoka nje ya bunge alipoingia rais kuhutubia bunge mwishoni wa mwaka jana.Kisa hawamtambui Rais aliyechaguliwa kwa kura za wizi na udanganyifu.
Kilichotokea sifahamu ila kimya kimya walianza kumtambua tambua na kuanza kusaini posho bungeni ,kupewa nafasi katika kamati mbalimbali za bunge na kupokea ruzuku ambayo ndiyo inaendesha makao makuu pale Kinondoni mtaa wa mfipa na kutoa mishahara za mgombea huyo zinazofanania na za wabunge a jamhuri ya muungano.
Sasa kama wao walifikia muafaka na Rais wa CCM au hawakufikia hadi kukubali kushiriki wote katika siasa za ngazi za juu itabidi mumuulize yeye kamanda mkuu mtakapomuona.

Ninachouliza kuna tofauti gani kilichotokea uchaguzi wa rais na hili la umeya Arusha.Mbona nyie mlikubali kuendelea na bunge na kusaini ruzuku kama hamumtambui rais.Msitudanganye kuwa kuna utofauti kati ya Rais na Urais..maana lugha naifahamu.Tunafahamu Mhe Marando aligombea Uspika wakati hamuitambui serikali iliyopatikana kwa udanganyifu na kama angeshinda angekuwa spika wa bunge hivi leo.

Kama muafaka ya madiwani ulisababishwa na njaa,nahofia ukaribu wa chadema kwa ngazi ya taifa pia unasababishwa na njaa.
Umeya na Uspika una tofauti gani? Kama wapiganaji kwelikweli msingeingia bungeni na msingemkubali Rais mpaka sasa hivi kama mnavowashauri wana Arusha kwa suala la Meya.
Maslahi ya taifa mbele siasa uchwara nyuma daima.Kuna tofauti kati ya siasa na uanaharakati..
Tafakari na chagua moja
 
Mwana Kwetu, nadhani umeandika hii makala kwa hisia zako binafsi kuliko uhalisia wa mambo. Siamini hata kama kweli umepata mawazo ya kutosha ya wakazi wa Arusha waliomchagua Mbunge Lema na Madiwani wake.

Mwana Kwetu mambo lazima yaende kwa sheria na kanuni. Tanzania tumefika hapa tulipo kwa sababu tumefanya mambo mengi bila kufuata maadili,sheria na kanuni. Kila jamii ina kiongozi wake anayewaelekeza wafanye nini, waamue nini, waseme nini na kdhalika. Bila hivyo kutakuwa na mvurugano, kila mmoja atafanya la kwake na amani itapotea, hili lipo wazi kabisa. Sasa Madiwani wa CDM walipata wapi huu mwongozo wa kukaa na wa CCM na kufikia huo muafaka bila Mbunge wao na viongozi wengine kujua? Mwana Kwetu huoni kuna jambom lililojificha hapa?

Unazungumza habari za Lema kupoteza jimbo 2015, unachotuambia ni kwamba Lema akiona uovu unatendwa na Diwani wake asiukemee kwa sababu atapoteza jimbo uchaguzi ujao. Kama ni mwadilifu atakuwa tayari kuupoteza huo ubunge na umma utaamua.

Wakati ccm walipopindisha sheria na kuchagua Meya kinyemela wote tulisema hapana hilo siyo sahihi. Tukawaunga CDM mkono katika kilo chao, tukaiambia serikali ya CCM kwamba waangalie upya njia iliyotumika kumpata Meya, wakakataa kata kata.Tukaomba maandamano ya amani, wakatugeuka na kuua watu na kutia vilema wengine.
Baada ya hapo hatujasikia mengi kuhusu suala hili, lakini ni imani yetu kuwa, lazima kuna mchakato ambao CDM, CCM na serikali walikuwa wanaufanya ili kufikia muafaka.

Kuingia muafaka wa namna hii, ambao haujulikani ulianza anzaje ni kuwasaliti watu wa Arusha waliokubali kumwaga damu kutafuta haki ilipo, hujawatendea haki wale waliolemazwa na ukatili wa hii syste.
Mwana Kwetu hatujasikia CDM wamakataa kukaa meza moja na CCM kufikia muafaka kama wewe unavyodai. Hili lingetokea kila mmoja angewaunga mkonoi Madiwani wa Arusha. Sasa kwa nini wafanye vikao ambavyo havina baraka za uongozi wa juu kama hakuna kitu kisicho cha kawaida hapo? Angalia Nape ameanza kutukana viongozi wa CUF ati ni njaa zao ziliwafanya waingie kwenye serikali ya mseto, baada ya muda na hili la Arusha utasikia maajabu
Mungu ibariki Tanzania.
 
All in all CDM Arusha mambo ni tete kuliko inavyoonekana. Madiwani ni watu wazima acheni kuwapiga mkwara kama watoto. Kamati kuu inatakiwa iwaonee huruma waliowaweka madiwani madarakani. Ukweli Mallah akifukuzwa aingie tu NCCR- Mageuzi au CUF tumpe kura zetu. Hatuko interested na procedures bali kazi ifanyike na ndio lengo la kuwachagua hawa madiwani.

Akiingia CCM ndo itakuwa rahisi zaidi kuibuka na ushindi manake CCM watampa kura za huruma pia. Hivyo vyama ulivyovitaja havina wafuasi wengi maeneo yake.
 
kwa mtu asiyejua anaweza kuona kuwa mtoa hoja ameongea vitu vya msingi kabisa. Pia kama wewe ni mtu usiyefuatilia mambo kwa makini si ajabu unaweza kukubaliana naye na kujikuta unampongeza kwa hoja aliyoitoa.

Kwa aina ya siasa na harakati za uchaguzi zilivyo hapa kwetu, chama cha siasa huwa zaidi ya mgombea. Ndo mana unaona wabunge wa CCM huwa wanaunga hoja mkono kwa asilimia 100 baada ya kutoa na kuainisha mapungufu ya maana kabisa kwenye hoja hizo. Sasa kwa suala la Arusha inabidi mtu utumie akili kidogo katika kulielezea.

Mh Lema ni mbunge wa Arusha mjini. Mazungumzo yaliyofanyika hadi kufikia muafaka nadhan yalifanyika hapo Arusha mjini jimboni kwake. Aidha Lema alikuwa mstari wa mbele sana katika kupinga uchaguzi uliofanyika wa Meya wa jiji la Arusha. Nakumbuka tulionyeshwa kwenye luninga namna alivyopigwa virungu na polisi katika harakati hizo. Kwa maoni yangu alipaswa kushirikishwa wakati wa mazungumzo hayo. Kama yalikuwa na nia nzuri ilikuaje yafanyike bila mbunge kujua?

Kwa kufikia muafaka na kupewa vyeo ambavyo wamepewa hao madiwani, je hili linaondoa dosari za uchaguzi zilizojitokeza? Tujaribu kufikiria kwamba kama taratibu zingeenda vizuri na CCM kushinda uchaguzi huo, madiwani wa CDM wangechukua uamuzi gani? Kwa hiyo maandamano ya Januari 5 yalikuwa ni ya kudai hivyo vyeo walivyopewa?

Mimi nina hakika kuwa mazungumzo kati ya CDM na CCM kuhusiana na sakata la Arusha yalikuwa na kasoro. Kasoro hizo nadhani ndo zinafanya hadi uongozi wa juu udhani kuwa kuna rushwa ilitembea. Mazungumzo kati ya chama kimoja na kingine ni lazima yahusishe ngazi za juu za chama hata kwa taarifa tu. Pia namsikitia mh Mallah na wenzie kwani wameingia kwenye mtego wa CCM. Kama tatizo lilikua ni kuvurugwa kwa utaratibu wa uchaguzi kwa nini uchaguzi huo wa meya usifanywe upya kwa kufuata taratibu? Kwani nadhani kama CCM watashinda vyeo vyote katika chaguzi halali basi Lema hatakua na hoja ya kusimamia.
 
Nimesoma hii thread nikabaki najiuliza kama kweli mwandishi ni mkazi wa Arusha au ni mtetezi tu wa Mallah. Swala kubwa hapa ni namna walivyoingia muafaka na muafaka wenyewe! Wameingia muafaka ambao haujibu maswali yetu sisi wakazi wa Arusha ambao tupo tunawatunza ndugu zetu waliopigwa risasi na polisi tar 5/1. Nimeongea na Diwani aliyekuwa kwenye kamati ya muafaka na amenihakikishia kuwa makubaliano yao sio yalioletwa kusainiwa. Walipokataa na kueleza hilo wenzao wakawageukia. Kwanini tusidhani ni rushwa ilitembea. Hapa hakuna wananchi wanaoukubali huo muafaka feki. Mi nipo Arusha na hata huko Kimandolu hawaukubali na wanatilia mashaka kwamba rushwa imetembea. Ndio maana hata sherehe ya kupongeza muafaka ilikosa watu. Lazima chama kifuate taratibu na kama watu hawataki hilo waondolewe. Na Lema kama akiendekeza ujinga wa akina Mallah ndio atalipoteza jimbo maana hatutamchagua tena.
 
mkuu naunga mkono hoja 100% Lema analeta bange na uhuni wake katika siasa sisi kama wakazi wa arusha tushaanza kuwa na wasiwasi wake, kwanza sisi wakazi wa kaloleni tulimchaguwa yeye baada ya diwani wetu kutuomba sana tumchague lakini sisi tunamjua tangu yuko TLP alishawahi kuongwa pesa ili ccm ishinde,chondechonde Lema eshimu madiwani wetu ukijua kwmba wewe ni source ya vurugu za arusha, ni muda muafaka wa wewe kutimiza ahdi zako ulizotuahidi na sio kulumbana na madiwani wetu Arusha sio Udom bwana ambako unashawishi watoto wagome
 
Akiingia CCM ndo itakuwa rahisi zaidi kuibuka na ushindi manake CCM watampa kura za huruma pia. Hivyo vyama ulivyovitaja havina wafuasi wengi maeneo yake.

Hawezi kwenda CCM kwani huku ni kuwalisha wananchi matapishi kwani bado hatujasahau aliyotufanyia Lawrence Hedi wa CCM aliyekuwa Meya ya Manisapaa ya ARusha . Mkakati ni kusonga mbele na siyo kurudi nyuma kuvaa magamba tena. Tayari Magamba walishapata F na alishapewa fursa nyingi za ku-resit bado akashindwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom