Shine
JF-Expert Member
- Feb 5, 2011
- 11,481
- 1,364
Ma.ga.mba at work again,baada ya Lema kuwa kivutio pale msibani kiasi cha kila mtu hasa vijana kutaka kushikana mkono na Lema mpaka Katibu wa CCM wilaya ya Arumeru kuanza kuwazuia na kutaka kusabisha tafrani CCM walitishika sana...sasa wameona wawatumie hao wazee ili tu Lema asishiriki kampeni kwa kuhofia mvuto alio nao...
kwanini hao wazee wasinge mwita katika kikao chao waka mweleza alivyowakwaza(kama ni kweli) na kumpa nafasi ya kujitetea...ninavyoamini sifa na kazi za wazee ni pamoja na kushauri,kuonya na kusamehe...sasa napata shaka na aina hii ya wazee wakukaa kikao na kutoa adhabu moja kwa moja...kidogo ninge amini kama ingelisikika kuwa...Wazee wamemtaka Lema awaombe radhi..akakaidi..then wafanye uamuzi kama huu.
Kikatiba pia hawa wazee hawana mamlaka kama hayo na ikizingatiwa pia marehemu Sumari hakuwa mbunge wa wazee pekee,alikuwa mbunge wa makundi yote(vijana,wazee,wasomi,wasio wsomi nk),na ndivyo atakavyokuwa mbunge atakayechaguliwa tena hapo 1 April...sasa sijui hawa wazee wanapata wapi mamlaka ya kuwasemea wana Arumeru wote.
Lema tia timu Arumeru muda ukifika ni haki yako kikatiba kamanda.
Kama ishara zote kama hizo zishajionyesha ccm wanajisumbua ya nini si wangejiweka pembeni kama mkeo wao cuf tu?