Wanawake CHADEMA wamshukia Tendwa

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
BARAZA la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mkoani Kilimanjaro (Bawacha), limemtaka Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, John Tendwa, kuacha siasa na badala yake awaamuru polisi kuwakamata na kuwafikisha mahakamani watu wanaodaiwa kumtishia maisha mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema.

Wiki iliyopita, Tendwa alikaririwa na vyombo vya habari akimuonya Lema kutokanyaga kwenye kampeni za uchaguzi mdogo katika jimbo la Arumeru Mashariki, kwani angefanyiwa vurugu.

Tendwa alidia Lema alitoa matamshi ambayo yalionekana kuwakera wazee wa kimila wa kabila la Wameru (Washila) katika mazishi ya marehemu Jeremiah Sumari na hivyo wakamtaka akawaombe radhi kwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Mwenyekiti wa Bawacha Mkoa wa Kilimanjaro, Lucy Owenya, alisema kauli hiyo ya Tendwa ni ya kushangaza hasa ikizingatiwa imetolewa na Msajili wa Vyama vya Siasa ambaye ndiye mlezi wa vyama vyote nchini na tena ni mwanasheria aliyebobea.

Owenya alimtaka Tendwa kuwaarifu polisi kuwapo kwa watu wanaodaiwa kumtishia Lema kama anao ushahidi, ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Alisema CHADEMA ni chama chenye usajili wa kudumu na kina haki kisheria kushiriki uchaguzi mdogo Arumeru Mashariki bila kutishiwa na mtu au taasisi yoyote kinyume cha sheria; na kuongeza kuwa kauli ya Tendwa inalenga kukidhoofisha chama hicho.

Owenya ambaye pia ni mbunge wa Viti Maalum, aliongeza kuwa kutishia kuua kwa maneno ni kosa la jinai kwa mujibu wa sheria, hivyo Tendwa anawajibika kuwalinda viongozi wote wa vyama vya siasa kutokana na vitisho vya aina yoyote kwa kuwaripoti polisi mara moja kwa kuwa ana ushahidi na wazee hao waliotishia kumuua Lema.

Wakati huo huo, Bawacha imelaani mauaji ya raia watatu waliouawa na askari wa jeshi la polisi mjini Songea, mkoani Ruvuma, hivi karibuni na kudai kuwa vitendo hivyo visipodhibitiwa vitachochea uvunjifu wa amani kwani wananchi watakosa uvumilivu.
 
Hakika baada ya jana kutolewa malalamiko hapa kuhusu BAWACHA na Dr Slaa kutoa mwongozo hakika BAWACHA wameanza kazi.Nimeamini JF ni shule na chuo cha mafunzo.Keep it up JF
 
Nakupongezeni kwa kuzinduka kwenye usingizi, msilalelale tena, jaribuni kuwa front line kukomboa Tanzania yetu..
 
Naona BAWACHA wameanza kuamka na hii inaweza ikawa baada ya malalamiko ya wadau haoa JF kuwa hatuoni kazi ya BAWACHA....safi sana BAWACHA-Kilimanjaro.
 
Tendwa sheria wazifahamu mbona umeanza siasa za upande upande tena tulia ndungu usivunje sheria kwa siasa linda vyama vyote usije ukatako kwenye msingi wako utaharibu
 
YES,Sasa kumekucha BAWACHA mkianza hivyo watu kama hao akina Tendwa hawatatuchezea
watanzania wanajua wapo wapiga kelele.Maana mwanamke akiamua kupiga kelele au kulia jamii
yote lazima itaharuki.Tunataka Mwenyekiti wa BAWACHA asikike kuliko akina Helen Bisimba na Ananilea
Nkya Pleaseee......Mwanzo mzuri BAWACHA. KEEP IT UP!!!
 
jana niliona replay ya Daktari akisema kuwa wamenote ushauri wa jamaa na wataufanyia kazi....inawezekana ndo sasa wameanza ila I think wanatakiwa kuwaunganisha wanawake wote.....unajua kama wanawake wakianza kuimba CHADEMA kama wafanyavyo vijana, watu wa makamo na baadhi ya wazee wasio wakiritimba basi mwisho wa CCM hata 2015 haifiki...and its simple sasa hivi maisha ni ngumu vibaaya
 
Safisana hawa BAWACHA ndiyo saizi ya tendwa,akileta za kuletwa mtokeena sufuria,mwiko,...mpaka kieleweke
 
Kwa mara ya kwanza ndio nasikia tamko la BAWACHA! Msonge mbele![/QUOTE
Kamanda Mnyisansu si kweli, unless hatusomi magazeti. Katika sakata la madaktari BAWACHA walitoa tamko. Juzi juzi pia walitoa tamko juu ya Mwanasoka Sofia Mwasikili. Siku ya wanawake pia walizungumza na vyombo vya habari.
 
Kwa mara ya kwanza ndio nasikia tamko la BAWACHA! Msonge mbele!


Kamanda Mnyisansu si kweli, unless hatusomi magazeti. Katika sakata la madaktari BAWACHA walitoa tamko. Juzi juzi pia walitoa tamko juu ya Mwanasoka Sofia Mwasikili. Siku ya wanawake pia walizungumza na vyombo vya habari.
 
Back
Top Bottom