Xi Jinping
JF-Expert Member
- Jun 14, 2023
- 8,102
- 23,690
Aliyekuwa Godfather wa mitindo nchini Italia, gwiji na nguli wa mitindo duniani bilionea Giorgio Armani aliyezaliwa katika mji wa Pianceza nchini Italia amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 91.
Alianza kazi zake miaka 50 iliyopita jijini Milan jirani na mji aliozaliwa kwa kuanzisha Giorgio Armani SpA mwaka 1975.
Baadaye alijipatia umaarufu mkubwa duniani kwa kudesign, kutengeneza na kuuza bidhaa mbalimbali zenye chapa ya Giorgio Armani kama nguo, viatu, accesories na home interiors.
Luxottica eyewear na vipodozi na manukato ya L'Oréal ni miongoni mwa bidhaa ambazo ziko chini ya licenses ya Giorgio Armani.
Giorgio Armani ni brand ya tatu kwa ukubwa katika mitindo nchini Italia na duniani ikiwa nyuma ya Gucci na Prada.
Ndio kampuni pekee ya mitindo ya Ulaya ambayo bado inaendelea kufanya biashara zake nchini Urusi licha ya makampuni mengine ya Ulaya kufunga biashara zao, kufuatia kile wanachoita uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.
Kwa nini Waitaliano wamejipata sana kwenye luxury brands?
Sio tu kwenye fashion kama Giorgio Armani,Gucci na Prada.
Hata kwenye ndinga za kifahari wako vizuri wana brands kama Lamborghini, Ferrari, Maserati na Alfa Romeo.
Alianza kazi zake miaka 50 iliyopita jijini Milan jirani na mji aliozaliwa kwa kuanzisha Giorgio Armani SpA mwaka 1975.
Baadaye alijipatia umaarufu mkubwa duniani kwa kudesign, kutengeneza na kuuza bidhaa mbalimbali zenye chapa ya Giorgio Armani kama nguo, viatu, accesories na home interiors.
Luxottica eyewear na vipodozi na manukato ya L'Oréal ni miongoni mwa bidhaa ambazo ziko chini ya licenses ya Giorgio Armani.
Giorgio Armani ni brand ya tatu kwa ukubwa katika mitindo nchini Italia na duniani ikiwa nyuma ya Gucci na Prada.
Ndio kampuni pekee ya mitindo ya Ulaya ambayo bado inaendelea kufanya biashara zake nchini Urusi licha ya makampuni mengine ya Ulaya kufunga biashara zao, kufuatia kile wanachoita uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.
Kwa nini Waitaliano wamejipata sana kwenye luxury brands?
Sio tu kwenye fashion kama Giorgio Armani,Gucci na Prada.
Hata kwenye ndinga za kifahari wako vizuri wana brands kama Lamborghini, Ferrari, Maserati na Alfa Romeo.