LEGACY: Kwanini hili kongamano kitumike kizungu badala ya Kiswahili?

TODAYS

JF-Expert Member
Apr 30, 2014
13,762
21,228
IMG_20220714_105015.jpg

Wadau wa legacy leo tunalegacy yetu hapa Zanzibar inayotokana aliyekuwa rias wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa inayofanyika kwa mara ya pili na sasa inafanyika nchini Zanzibar kisiwani Unguja.

DSC_0060.JPG

PHOTO: aliyekuwa Rais wa Msumbuji Joachim Chisano akiongea katika kongamano hilo.

Rais wa Tanzania Mama Samia Suruhi Hassan ndiye mgeni rasmi kwenye hili kongamano la pili juu ya kumbukumbu ya rais Benjamin Mkapa Zanzibar.

Wakati nchi yetu ikijinasibu kutumia kugha ya kiswahili na kukipa hamasa kutumika katika nyanja za kimataifa na OAU tayari inakitambua kuwa ya lugha kubwa inayokuwa kwa kasi, leo hii kuna jambo la kushangaza hapo ukumbuni.

Ndani ya kongamano hili kuna wageni mbalimbali wa kimataifa na wageni kutoka hapa nyumbani Tanzania, wageni waliotoka nje ni wachache kuliko wa hapa hapa ndani ya nchi.

Na hata wageni wa hapa hapa ndani wengi ni mabalozi ambao wanazungumza kiswahili, ila kwa hali iliyopo hapo ukumbuni kinasikika kilugha cha kizungu japo ndg MC balozi Mazura anajaribu kuchanganya Kiswahili na Kizungu.

Wakubwa waliopo hapo mmeshindwa wapi kukipa kiswahili power of kutumika ilihali hata balozi wa marekani anakiongea japo cha kuibia?.



Moderator naomba hii mada isiunganishwe na ile ya live hapa content ni kiswahili siyo tukio.
 
Wa Kiswahili wachangie kwa Kiswahili,halikadhalika wa Kiingereza.
 
..Watz tusiogope Kiingereza.

..Vijana wetu wanakosa fursa za kazi ktk taasisi za kimataifa kwasababu ya kutokujua Kiingereza.

..Hata Bilionea Laizer kaamua kujifunza Kiingereza. Pamoja na mabilioni yake ameona anahitaji kujua Kiingereza.
 
..Watz tusiogope Kiingereza.

..Vijana wetu wanakosa fursa za kazi ktk taasisi za kimataifa kwasababu ya kutokujua Kiingereza.

..Hata Bilionea Laizer kaamua kujifunza Kiingereza. Pamoja na mabilioni yake ameona anahitaji kujua Kiingereza.
Sidhani kama dhana ni kuogopa kizungu, ila kukipa nafasi kubwa kuliko lugha mama.

Mataifa yaliyotutawala bado yanatutawala kwa mfumo huo mpaka kesho na hatuondoki, kweli hatuwezi kuondoka ila tunapaswa kujenga himaya yetu na sisi japo haitazama chini ila kwa taratibu.
 
Sidhani kama dhana ni kuogopa kizungu, ila kukipa nafasi kubwa kuliko lugha mama.

Mataifa yaliyotutawala bado yanatutawala kwa mfumo huo mpaka kesho na hatuondoki, kweli hatuwezi kuondoka ila tunapaswa kujenga himaya yetu na sisi japo haitazama chini ila kwa taratibu.

..Ni jambo la manufaa kama vijana wetu watazungumza kwa ufasaha lugha za kimataifa zaidi ya moja.

..kama tunataka kuyatawala mazingira yetu na ya dunia kwa ujumla ni lazima vijana wetu wajue lugha za kimataifa.

..Waliotutawala sio kwamba walitufundisha lugha zao tu, bali hata wao walijifunza lugha zetu. That is how they managed to manipulate our ancestors.

..Mimi kwa maoni yangu lugha inayohitaji uwekezaji na msisitizo ni lugha ya Kiingereza. Lugha ya Kiswahili tayari tunaimudu, na imesambaa vya kutosha.

..Hayo ni mawazo yangu. Samahani kama nimekukwaza.
 
JokaKuu mkuu upo sahihi, ila hapa tunazungumzia uwasilishwaji wa kiswahili kwenye tukio ambalo wahusika kwa asilimia kubwa wote ni waswahili na eneo lilipo tukio ndiyo kitovu cha kiswahili!.
 
Back
Top Bottom