Lazaro Mambosasa aondolewe Dar es Salaam

Lazaro Mambosasa aondolewe Dar es Salaam

Huu ni wito ambao naupeleka kwa IGP Sirro .

Anayotenda RPC Mambosasa DSM hayana tofauti na aliyotenda Aliyekuwa RPC wa Iringa aliyeitwa Michael Kamuhanda , huyu alisimamia kikamilifu mauaji ya mwandishi wa Channel 10 marehemu Mwangosi , Na kwa kutumia busara ya hali ya juu IGP wa wakati ule bila ya kuchelewa alimng'oa Kamuhanda na kumpeleka Makao Makuu.

Kila mwenye macho amejionea mwenyewe kauli ya jeshi la polisi kukiri kuhusika na mauaji ya mwanafunzi wa NIT , haya ni miongoni mwa mauaji ya kishamba sana kuwahi kufanywa na jeshi la polisi , yaliojaa uzembe wa kiwango kisichopimika , ni mauaji ambayo hata jambazi bwege hawezi kuyafanya .

Ni wakati sasa wa IGP kumpeleka Mambosasa Makao Makuu ili kurudisha amani jijini DSM , ambayo imetoweka moja kwa moja tangu kuingia kwa Mambosasa.

Angalizo - Si kila polisi anaweza kuwa IGP wa DSM .
Kwani Mambo now ndiye alimuua huyo marehemu?
 
Uyo muda si mrefu anapandishwa kua Kamishna kumbuka Mkuu aa Kanda Maalum mara nyingi anakuaga Kamishna....so hapo uyo SACP Mambosasa anasubiria kupandishwa kua CP
Nakubaliana na wewe. Jamaa anaweza akaruka cheo cha DCP na kuwa CP moja kwa moja. Utendaji wake ni lazima utakuwa unaendana na kasi ya bwana yule
 
Nakubaliana na wewe. Jamaa anaweza akaruka cheo cha DCP na kuwa CP moja kwa moja. Utendaji wake ni lazima utakuwa unaendana na kasi ya bwana yule
Karibu tena mkuu , Adui yako DR SLAA kaula , wewe ndala bado zinakukatikia njiani .
 
Hivi Mambosasa ana elimu gani? Au ile ya hapa na pale?
 
Naunga mkono hoja kwa asilimia 100

Huyu Kamanda Mambosasa ahamishwe Dar kabla hajaleta maafa makubwa jijini hapa

Inawezekanaje aone kifo cha mwanafunzi Akwilina, kama kifo cha sisimizi??

Yeye tulimnukuu akikiri wazi siku ile ya tarehe 17/2/2018 kuwa mmoja wa askari wake ndiye aliyehusika na mauaji ya yule mwanafunzi Akwilina, ambaye wala hakuwa mwandamaji, Bali alikuwa kwenye daladala!

Sasa inashangaza kusikia ememwachia huru yule Muuaji wa Akwilina, kwa kile alichodai kuwa hana ushahidi wa kutosha wa kumuanganisha Muuaji huyo l katika tukio lile la kuuawa Akwilina!
 
Naunga mkono hoja kwa asilimia 100

Huyu Kamanda Mambosasa ahamishwe Dar kabla hajaleta maafa makubwa jijini hapa

Inawezekanaje aone kifo cha mwanafunzi Akwilina, kama kifo cha sisimizi??

Yeye tulimnukuu akikiri wazi siku ile ya tarehe 17/2/2018 kuwa mmoja wa askari wake ndiye aliyehusika na mauaji ya yule mwanafunzi Akwilina, ambaye wala hakuwa mwandamaji, Bali alikuwa kwenye daladala!

Sasa inashangaza kusikia ememwachia huru yule Muuaji wa Akwilina, kwa kile alichodai kuwa hana ushahidi wa kutosha wa kumuanganisha Muuaji huyo l katika tukio lile la kuuawa Akwilina!
" waliomteka MO ni wazungu wawili " - Mambosasa
 
Back
Top Bottom