LATRA yakamata mabasi yanayochezea mifumo ya usalama Mkoani Arusha

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989


Baadhi ya wahusika wa mabasi ya abiria wanaochezea mifumo ya usalama na mwendo katika mabasi wamenaswa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) Mkoa wa Arusha.

Afisa Mfawidhi wa LATRA Mkoa wa Arusha, Joseph Michael ameongoza zoezi la ukaguzi katika maeneo tofauti katika maegesho ya magari Jijini hapo ambapo amesema madereva wanaofanya hivyo wanahatarisha maisha ya abiria ambao wamekuwa na imani kwa vyombo hivyo.

Ameongeza kuwa mamlaka hiyo haitamuonea muhali mtu yeyote ambaye atakiuka taratibu zinazosimamiwa na mamlaka hiyo.
 
Kwann body za magari siku hizi ni nyepesi jibu ili kupunguza madhara ya ajali ikipiga mzinga vifo haviwi vingi sana kama body za sufuria madhara huwa ni makubwa sana
 
Mimi nawapongeza sana LATRA na Polisi, naona sasa Akili itawasogoea Hawa Jamaa, maana unakuta mtu anaendesha gari kama vile kapakia mahindi kumbe Ni watu... Hadi unawaza wanaonekana kweli?? Kumbe wamechezea king'amuzi🙌🏾🙌🏾
 
1. Mfumo huu unawekwa na mawakala binafsi wa LATRA wasiowajibika popote.

2. Latra, Dereva au mwenye basi hawana ufahamu wowote wa kiufundi wa mfumo huo wala umadhubiti vifaa husika.

3. Kwanini katika mazingira hayo matatizo kwenye mfumo huo walaumiwa dereva au mwenye basi tu?

4. Hata simu ya mtu huharibika sembuse kifaa cha kielectroniki kilicho kwenye mazingira ya mikiki mikiki ya safari kila siku?

5. Kwani manufacturer wa vifaa hivyo anasema huwa haviharibiki au huwa vimetoka mbinguni?

"IIifaa LATRA wangekuwa na mabasi yao kuzijua changamoto za wenye mabasi wanaochagua kuwasumbua na bila sababu."

Biashara za serikali si ni hizi mwendokasi, TRC, ATCL, tanesco, ttcl na za namna hIyo?

LATRA - oneni aibu!
 
Back
Top Bottom